Je, hili ni kosa katika ndoa?

Tunguja

JF-Expert Member
Feb 15, 2018
450
327
Dada yangu katimuliwa na mumewe,dada yangu ameolewa kwenye ndoa ya wake wawili na yeye ni mke mdogo,bahati mbaya sana mke mkubwa hajajaaliwa kupata uzazi,Ila dada yangu ana watoto wanne.

Sababu ya yeye kutimuliwa kwa mujibu wa maelezo ya shemeji ni kwamba ada yangu amekuwa akimwambia mwanaye mkubwa (15yrs) kwamba yeye ndio mrithi wa mali zote za baba yake kwasababu mke mkubwa hana watoto, kwa maelezo yake shemeji ni kwamba alishawahi kumuonya mkewe mara kadhaa kwamba anachokifanya sio sahihi kabisa, kwasababu

1: Watoto watabweteka wakitegemea mali za baba yao.
2: Hajui bibi mkubwa anawaza nini anaposikia hizo kauli, Inawezekana anaweza akafanya vitu ambavyo vinaweza kuwaletea madhara watoto ili wakose wote
3: Anahisi mkewe anamwombea kifo ili yeye na wanawe warithi mali zake

Anadai kwamba baada ya kuona hiyo tabia haikomi kaamua amtimue kabla madhara makubwa ambayo yeye anahisi yanaweza kutokea hayajatokea,kamwachia nyumba pia kampa mtaji milioni thelathini ili ,kamwambia alichopewa ndio urithi wa watoto yeye asimamie ikitokea akifa vitakavyokuwepo vyote ni vya mke mkubwa, najua ,je nani mwenye kosa kati yao?
 
Dada yako hana busara, hizo ni kauli zisizokuwa na afya katika mahusiano na ndoa.

Hata hivyo, shemeji yako hakupaswa kuachana naye maana ndoa (kama ni ya Kikatoliki) ikishafungwa haifunguliwi.

Anapaswa kuishi kiapo cha kuvumiliana kwenye shida na raha kama alivyoahidi mbele ya Mungu na watu.
 
Huyo shemeji yako aliyemuacha dada yako amefanya maamuzi ya busara sana.
Huyo dada yako alikanywa lakini hakusikia, kauli anazotoa kwa mke mkubwa ni za kichochezi kabisa na huenda zikazaa madhara makubwa pasipo kutarajia.
 
hio milioni thelathini mwambie atoe milioni moja abeti aston vila na west ham anaweza akatoboa ili mwanawe arithi (mwambie aache tamaa ndio maana ndoa wanafanya kuwa ngumu)
 
Mwenye kosa ni dd yako sababu alishaonywa mara kathaa pia akichokifanya ni sawa inabidi dd yako na yeye atafute chake asitegemee cha kurisilkn hata hivyo kafanya hivyo co kwa bahati mbaya anajua alikifanya na anajua wanawe amewawekea nini Mungu anusuru wanawe wasiwe na akili km za mamayao
 
Andika vizuri ueleweke.
Tumetofautiana uandishi pia tumetofautina uelewa,wewe unaona sijaandika vizuri mimi naona uelewa wako mdogo,ndio maana wewe hujaelewa nilichoandika halafu wengine wameelewa na wanacomment
 
Tumetofautiana uandishi pia tumetofautina uelewa,wewe unaona sijaandika vizuri mimi naona uelewa wako mdogo,ndio maana wewe hujaelewa nilichoandika halafu wengine wameelewa na wanacomment
Wanavumilia tabu tu. Wafanyeje sasa.
 
Hii inasababisha baba mwenye mali akifariki na mali zinapotea.
Kijana wa miaka 15 anatakiwa ajue mali za familia na kama biashara anatakiwa ajifunze aambatane na baba yake.

Mwambie shemeji aache ujinga na akifa kila kitu kinaenda.

Ujinga ujinga tu umemjaa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom