Ndugu wadau,
Kuna jambo linanitatiza katika mpangilio wa ufanyaji biashara wa hili shirika la umeme TANESCO. Mimi nahitaji kuunganishiwa umeme katika nyumba yangu umeme ambao nitakuwa naulipia kwa kadiri ya matumizi yangu. Lakini ninakerwa na huu utaratibu wa malipo ya vifaa vya kuunganishiwa umeme.
Kwa mfano natakiwa nilipie nguzo kadhaa, waya mita kadhaa, Transformer, na kadhalika jumla ya ngarama naambia ni Tshs Mil. 15, eti kwa ajili ya kuweka miundombinu ya kufikisha umeme ndani ya nyumba yangu. Lakini cha kushangaza baada ya kulipia vifaa hivi kwa Mil 15, vifaa husika vinageuzwa kuwa mali ya TANESCO Bila mimi muhusika kufahamishwa au kuombwa na Shirika hili.
Kupitia miundo mbinu hii niliyo nunua kwa pesa zangu za kudunduliza na mikopo, utaona TANESCO wakianza kuunganishia umeme watu wengine jirani yangu kwa bei nafuu bila kuulizwa au kuombwa na wahusika. Je hii ni haki? Shirika kujinufaisha kupitia mpango huu! Au kwa kuwa ni Shirika la Serikali linafanya litakavyo?
Je kujenga miundombinu ya umeme ni kazi ya mlaji au ni kazi ya msambazaji?