Arrangements za maisha ya ndoa zinatofautiana, but generally mke majukumu yake ni short term, chakula, afya za watoto, mahala mnapoishi pako sawa etc. Wewe mwanaume, long term projects kama ujenzi na miradi ya kuongeza uhakika wa kipato.
Sasa kaka after 5 years, hata mipango ya kiwanja ulikuwa huna? Maana yake kama ungekuwa nayo, basi at least mngekuwa wote kwenye process nzima. Hapo katumia principles za aliyelala usimwamshe
Nimeiona kwa Kaka yangu. Lakini kwa namna tofauti, mke alikuwa na kiwanja kabla hawajaoana, walipofikia hatua ya kuanza ujenzi Kaka yangu akamrudishia gharama nusu mke wake na akawa na umiliki wa 50%.
Na hiyo nusu aliyoipata Mke wake akaiingiza kwenye gharama za ujenzi kama mchango wake.
Kaka yangu alifanya hivyo kwa kuamini kwamba hatakuwa 'comfortable' kuishi kwenye nyumba ambayo Mke ni mmiliki
wa kiwanja kwa 100%. Na kwa sasa wameshahamia kwenye makazi mapya kiroho safi.
Hiyo ni scenario yao, sijui kama kwako inaweza kufanya kazi.
Ila kawaida katika maisha yetu ya Kiafrika...........Cha mume cha familia, cha mke ni chake. Hapa haitakiwi kuanzisha ugomvi kwa sababu amenunua kwa pesa yake. Tumia diplomasia kumaliza hii ishu.
Good luck.
huyo dada mroho sana mwanaume ndo kichwa atakama kanunua yeye lazima aandikwe mme,mtoto,au wote,iyo cyo dalili nzuri kabisa na ninjia yakumpashetan loophole yakumletea uyuda!kaa nae mpaka hati uwepo au watoto unless its dangerbut 2mia busara sana,xor
una kubali mmiliki gari mbili alafu hata kiwanya hamna? uyo mwana mke amekuona mzembe mpaka akaamuwa kukopa ili anunuwe kiwanja. akilini akijuwa mawazo hayo wewe huna...
Hicho kiwanja achana nacho mjomba,tafuta hela.nunua chako,jenga nyumba yako ya heshima...achana na mambo ya wanawake mzee,hiyo issue italeta ugomvi...jenga vyako wala usimuulize,mwache afanye anachojisikia na vihela vyake...jenga mijengo yako,wee mlie kimyaaa.
nema13 usiongee kishabiki,imagine mimi ni kaka yako then nyumba inaisha natimuliwa kwenye nyumbaMe sioni ubaya wa mkeo kuandika jina lake pengine aliona haina shida na ndio maana alikushirikisha suala la kununua pia, na isitoshe na yeye ana haki ya kumiliki acheni mambo ya ukandamizaji wa kijinsia. Kwani imeandikwa wapi mwanaume tu ndo mwenye haki ya kumiliki resorces?
shemejiii we chezea wanawake wa kichaga wana macho matatu
Wewe tatizo lako nini mkifa hiyo ni mali ya watoto au watoto sio wa kwako? hapo future ni watoto sio nyinyi tena hata mkifia kwenye hiyo ya kupanga ni poa tu. Nyumba ikiisha mwambie mpangishe mlipie watoto ada na kama vipi na wewe chukua mkopo mjenge kwenye kiwanja chenye jina lako muwe nazo mbili si faida hiyo? akitaka kukufunga bao wewe sawazisha atasuzika na roho yake.nimekaa kimya sijaongea kitu na mkataba tayari umeandikwa na malipo yote yameshafanyika ,nahofia kwenda kwa wanasheria atatake it serious inaweza kuharibu mahusiano na akaanza kufanya mambo yake kisirisiri