je hii ni halali?

je hii ni halali?

mdukuzi

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2014
Posts
22,312
Reaction score
56,011
tupo kwenye ndoa halali ya kanisani huu mwaka wa tano,
mimi na mke wangu wote ni wangu wote ni wafanyakazi na tumejaaliwa kupata watoto wawili ,tunaishi nyumba ya kupanga na kila mtu anagari yake ya kwendea kazini,mwaka jana mke wangu alichukua mkopo benki akataka kununua kiwanja ili tuanze ujenzi wa kibanda chetu,kilichonishangaza kwenye mkataba wa kuuziana hicho kiwanja aliandika jina lake

swali
je nichangie kwenye ujenzi wa nyumba hiyo?
je nani atakuwa mmiliki wa nyumba hiyo wakati makaratasi yana jina lake?
je hawezi kunifukuza kwenye nyumba hiyo siku mmoja ikizingatiwa anatoka kulee kwenye mlima mrefu kuliko yote afrika?
je nitapata amani ya ndoa kulala kwenye nyumba ambayo kiwanja kina jina la mke,usingizi upo hapo
 
wakat anaandika hayo majina ulikuwa wapi bandugu? kama vp nenda kwa wanasheria mmiliki wote hicho kiwanja
 
^^
Ulipomshirikisha hofu yako alisemaje?
^^
 
nimekaa kimya sijaongea kitu na mkataba tayari umeandikwa na malipo yote yameshafanyika ,nahofia kwenda kwa wanasheria atatake it serious inaweza kuharibu mahusiano na akaanza kufanya mambo yake kisirisiri
 
Ww mbona mkeo mstaarabu sana,mke wa kaka angu alinunua kiwanja kwa hela ya bro akaandika ni chake mama ake,bro alipojua huo mchezo,nusu amuufosaro.ila pole sana bro,wanawake wengne n pasua kichwa
 
Miaka 5 yote hamjaaminiana? Kwanza inawezekana yeye anakuamini, wewe tu humuamini. Angalia maana siku si nyingi utaanza kuwaza kama hao watoto wawili ni wako...
kaka kuna mambo mengi ila kwa leo naongelea hilo tu
 
Unamuamini mkeo mkuu?...
nshakwambia anatoka kwenye mlima mrefu wale watu ni kama homa za vipindi hawatabiriki ,uaminifu wako unaweza kukuponza coz ni wazuri kwa timing
 
mdukuzi Mzee, sio wa kwanza wewe kuoa milimani. Unless kuwe na sababu nyingine lakini hicho sio kigezo cha kushindwa kumuamini mkeo na kuishi maisha ya kimachale machale kama ngedere...
 
Last edited by a moderator:
tunaishi nyumba ya kupanga na kila mtu ana gari yake ya kwendea kazini

Hapa kama sielewi vile,

Yaani mwanaume mwenye korodani mbili, una mke na watoto wawili.

Badala ya kununua kiwanja unakimbilia kununua gari/magari.

Mwisho wa siku unakuja mbele yetu kulalama kuwa mkeo kaandika kiwanja kwa jina lake.

In short mkeo (ingawaje kakosa busara) kakuona huwezi kuchanganya akili yako vizuri.
 
nimekaa kimya sijaongea kitu na mkataba tayari umeandikwa na malipo yote yameshafanyika

Wanaume wengine sijui mnaingia kwenye ndoa mkiwa mmepitia vyema mafunzo ya ndoa au mnakurupuka tu.

Tukio la kununua kiwanja cha kwanza kwa wanandoa huwa ni hatua moja kubwa sana na muhimu.

Sasa nashangaa na pengine wengine wanisaidie kushangaa kuwa mume huna taarifa zozote za namna mkataba ulivyoandikwa, hivi kweli hapa tatizo ni mke au ni wewe (umekiri hapo juu kuwa hukuongea chochote).
 
huyo dada mroho sana mwanaume ndo kichwa atakama kanunua yeye lazima aandikwe mme,mtoto,au wote,iyo cyo dalili nzuri kabisa na ninjia yakumpashetan loophole yakumletea uyuda!kaa nae mpaka hati uwepo au watoto unless its dangerbut 2mia busara sana,xor
 
Hicho kiwanja achana nacho mjomba,tafuta hela.nunua chako,jenga nyumba yako ya heshima...achana na mambo ya wanawake mzee,hiyo issue italeta ugomvi...jenga vyako wala usimuulize,mwache afanye anachojisikia na vihela vyake...jenga mijengo yako,wee mlie kimyaaa.
 
Hapa kama sielewi vile,

Yaani mwanaume mwenye korodani mbili, una mke na watoto wawili.

Badala ya kununua kiwanja unakimbilia kununua gari/magari.


Mwisho wa siku unakuja mbele yetu kulalama kuwa mkeo kaandika kiwanja kwa jina lake.

In short mkeo (ingawaje kakosa busara) kakuona huwezi kuchanganya akili yako vizuri.

wakati tunaoana kila mtu alikuwa na gari yake ni gari yake ni vijigari vya bei rahisi na ni kawaida kwa dar es salaam si kila mtu mwenye gari ana nyumba labda kama unaishi mkoa tofauti na dar
 
Back
Top Bottom