Je GPA za NACTE na TCU ni tofauti?

Je GPA za NACTE na TCU ni tofauti?

clinician

JF-Expert Member
Joined
Mar 5, 2014
Posts
2,334
Reaction score
5,527
binafsi nimekuwa muathirika wa ongezeko la GPA kwa diploma holders wanaotaka kwenda Chuo Kikuu .Nina diploma ya clinical officer kwenye provisional transcript nina GPA ya 2.7.

Lakini kuna kitu nimegundua leo, ukijumlisha masomo yangu yote na kugawa kutafuta wastani unapata wastani wa 66,hii ni B plus ambayo ni sifa pia ya kwenda Chuo Kikuu. Pia nimegundua tofauti kwenye grades kati ya TCU na kwenye transcript, mfano kwenye transcript B plus ni 70-71 lakini TCU wao ni 65-74.

Sasa je kama nina average ya B plus maana yake si kwamba naweza kwenda Chuo Kikuu? Na je hii haimaanishi kwamba GPA yangu ya kwenye transcript na za TCU zinaweza kuwa tofauti?
 
hapana GPA inayotumika ni ile iliyopo kwenye cheti chako I.e 2.7 ,,,,ingekuwa GPA haipo kwenye cheti chako wangekuwa wamekuwekea average tu apo ungepopona
 
TCU wanakuwa na data base ya matokeo yako yani ukimaliza chuo wanapeleka matokeo NACTE na NACTE wanasubmit TCU hivyo ukiapply sawa wanadai vyeti na transcript kudhibitisha kama ndie mwenyewe aliyeapply ila matokeo yako wanayo yaliyopelekwa na chuo ndio maana unaweza anza application ukaambiwa ujakizi vigezo ivyo ndugu itategemea na chuo walikuwekea GPA ya ngapi kwa matokeo waliyo submit NACTE
 
binafsi nimekuwa muathirika wa oongezeko la gpa kwa diploma holders wanaotaka kwenda chuo kikuu .Nina diploma ya clinical officer kwenye provisional transcript nina gpa ya 2.7....lakini kuna kitu nimegundua leo,ukijumlisha masomo yangu yote na kugawa kutafuta wastani unapata wastani wa 66,hii ni B plus ambayo ni sifa pia ya kwenda chuo kikuu .Pia nimegundua tofauti kwenye grades kati ya TCU na kwenye transcript,mfano kwenye transcript B plus ni 70-71 lakini TCU wao ni 65-74...sasa je kama nina average ya B plus maana yake si kwamba naweza kwenda chuo kikuu? na je hii haimaanishi kwamba gpa yangu ya kwenye transcript na za tcu zinaweza kuwa tofauti?
Samahani ila hiyo ya kuwa TCU B+ ni kuanzia 65 umeiona wapi
 
Tcu wanakuwa na data base ya matokeo yako yani ukimaliza chuo wanapeleka matokeo nacte na nacte wanasubmit tcu ivyo uki apply sawa wanadai vyeti na transcript kudhibitisha kama ndie mwenyewe aliye apply ila matokeo yako wanayo yaliyopelekwa na chuo ndio maana unaweza anza application ukaambiwa ujakizi vigezo ivyo ndugu itategemea na chuo walikuwekea gpa ya ngapi kwa matokeo waliyo submit nacte

Nina ndugu yangu hapa ni C.O.Anamiliki pharmacy 3 na duka 1 la dawa muhimu

Yuko vizuri kuliko most of MDs .Nashauri wekeza kwenye biashara hautojuta
 
Dawa ni kuanzisha TAQRA (Tanzania Academic Qualifications Regulatory Authority).
GPA ya TCU, NACTE na wengine; sijui A ni 75-100 au la, na mikanganyiko kama hiyo itakoma.
Prof. Nadlichako kazi kwako...
 
nikuongopee ili iweje? mbona nimeweka wazi? kwenye transcript inaonesha nina b- tatu lakini kwenye muongozo wa tcu inaaonyesha nina b+ tatu..msingi wa swali langu upo hapo kama nacte na tcu wana grade tofauti,je haimaanish kwambaa na gpa inakuwa tofauti?
 
TCU wanakuwa na data base ya matokeo yako yani ukimaliza chuo wanapeleka matokeo NACTE na NACTE wanasubmit TCU hivyo ukiapply sawa wanadai vyeti na transcript kudhibitisha kama ndie mwenyewe aliyeapply ila matokeo yako wanayo yaliyopelekwa na chuo ndio maana unaweza anza application ukaambiwa ujakizi vigezo ivyo ndugu itategemea na chuo walikuwekea GPA ya ngapi kwa matokeo waliyo submit NACTE
Kwani unapofanya attachment ya qualifications ni kipi ambacho kinahitajika ,je ni transcript,cheti au vyote kwa pamoja?
 
Kwani unapofanya attachment ya qualifications ni kipi ambacho kinahitajika ,je ni transcript,cheti au vyote kwa pamoja?
kwa waliomaliza mwaka huu wana attach transcript tu kwani awana vyeti bado avijatoka ila miaka ya nyuma una attach vyote cheti na transcript kwani cheti wanakuwa wameishapewa uo ndio uelewa wng
 
Pole xana mkuu ndio hali ya nchi yetu xaxa , kubwa komaa kaxome hata nchi jiran kaka
 
Hongera, we apply tu ya Mungu mengi. Ila naomba unielekeze namna ya kupost information zangu kwenye jf, kila nikijaribu nashindwa mkuu...
 
Back
Top Bottom