Je Cremation Ni Mbaya?!

Nafikiri hapa umeleta nadharia nzuri ya burial...
Mazishi hayafai kuwa gharama na pia yanafaa kutunza Mazingira

Hao wa Italy kwa Mfano wanapunguza matumuzi mabaya ya miti kuchonga majeneza( Umuhimu wa Jeneza Ni Nini) na pia wanatunza mazingira

Mfano Kumzika mtu nyumbani na kutengeneza kaburi kwa zege na mapambo lukuki inaonekana kama tumemuenzi Ndugu yetu ila baadae eneo ili litakuwa gumu kufanya nalo biashara au kuwa pendeleo la watu kuishi

Kwa sasa nafikiri kuchomwa sio vibaya
 
Kiungo changu simuachii mtu
Je figo au ini lako akipewa mwanamke malaya ?
Anaenda kudanga huko
 
kudonate viungo Kwa watu wenye nia njema si vibaya

Ila changamoto ni nia ya binadamu inapokuwa haihanurika..mtalazimishana kufa kisa viungo mpige hela.

Na hilo ndio linaloepukwa
 
Kabisa mkuu.
 
Na hili ndilo Jibu Sahihi.
 
Kiuhalisia ni kweli watu wanakufa,ila kwanini kila mtu hufikiri kuwa lazima atakufa?najua sie tuliyo hai tunaona watu wakifa na sie tunajisemea kuwa ipo siku nasi lazima tutakufa,lakini mbona tunaona watu wakiwa mafukara lakini hatusemi kuwa nasi lazima tutakuwa mafukara au tunaona watu waliyopata ulemavu lakini hatusemi nasi tutakuwa walemavu?

Je,kipi kinafanya wote tuone lazima tutakufa(na si vinginevyo) tena bila kujari ni aina gani ya kifo?

Je, huku kufikiri lazima tufe sio imani tu hii?
 
Nafikiri kisayansi mwili wa binadamu ni dhaifu na mortal... bacteria, viruses,protozoas..na aina nyingine ya vidudu(microbes) vina uwezo wakuuchukua uhai wa binadamu

Ila kadri navyo binadamu anapozeeka na seli zake zinazeeka,..

Kifo kipo na sio nadharia ya imani lakini ya kiuhalisia na kisayansi
 
kudonate viungo Kwa watu wenye nia njema si vibaya

Ila changamoto ni nia ya binadamu inapokuwa haihanurika..mtalazimishana kufa kisa viungo mpige hela.

Na hilo ndio linaloepukwa
Je ku-donate kwa mwenye nia nzuri akabadilika akawa mwenye nia mbaya

Nafikiri ata kama mtu ana nia mbaya....hamna sadaka kubwa atakuwa anajua anaishia nayo kama kiungo cha mtu

Ebu fikiri ata kama uyo 'Malaya' akajua kwamba izi sio figo zangu...niamini atabadilika
 
Upanga barabara ya Maliki kipande cha kutoka shule ya msingi Muhimbili kwenda juu pale palikuwa makaburi. Kwa kweli kipande kizima kile Upanga kuanzia makaburi ya Tambaza mpaka International School kuna makaburi ya zamani mengi sana pale yamejengewa juu yake. Lakini hiki kipande cha barabara ya Maliki nakiongelea kwa sababu wakati barabara inataka kujengwa palikuwa na makaburi.

Serikali ikafukua makaburi na kuyahamisha.

Maana yake ni kwamba unapozikwa leo, unawazibia nafasi wanaokuja kesho.

Katika kipindi cha miaka 100 kama kila mtu atazikwa hapa duniani, tutajaza sehemu kama nchi nzima ya Gambia kwa makaburi.

Mimi nilishasema kitambo wanichome moto tu. Majivu Long Island Sound.
 
Gharama za mazishi zimekua kubwa kutokana na watu kuiga na hasa mambo ya tamaduni za kimagharibi,
Siku hizi kwenye misiba unakuta mpaka watu wanashona sare! kila mtu akifikwa na msiba atataka anunue jeneza la gharama zaidi ili asionekane yupo nyuma au choka mbaya au asionekane kua hakumthamini marehemu!

Napenda wanavyozikana waislamu,tajiri na masikini wote wanavalishwa sanda na wote wanabebwa kwenye jeneza lile lile kwenda kuzikwa!

Maiti zao hakuna cha kuvalishwa suti za gharama wala viatu vya gharama,wote ni sawa kwa tajiri na masikini,Gharama na mbwembwe zinazotumika kuwazika marehemu hazimsaidii lolote marehemu huko aendako bali matendo yake mema aliyoyafanya wakati wa uhai wake ndio yatakayo msaidia.
 
Zile dawa za kutunzia maiti zina chafua sana underground water,majeneza yanaharibu misitu.Cremation is the to go kwani hata kusafirisha maiti simple,.
 

Sababua zenye kupelekea kifo zipo nyingi sio hizo tu ambazo wewe umeeleza, lakini pia mtu anaposema kuwa lazima atakufa huwa hafikirii kwamba ni kwa sababu ya maradhi,uzee wala ajari bali huwa anajua tu lazima atakufa.

Uwepo wa kifo ndiyo kweli upo ni kama vile ambavyo ulemavyo nao upo lakini hakuna mwenye kufikiri kuwa lazima atakuwa mlemavu.

Ndiyo maana nasema huku kufikiri lazima tufe(na si vinginevyo) yaweza kuwa ni imani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…