Je chumvi huzuia mvua ?

Bob Dylan

JF-Expert Member
Dec 28, 2011
206
216
Wanajamvi habarini, nimekutana na kisanga kutoka kwa dada wa kazi, yeye ni mzaliwa wa Dodoma na alikuja kufanya kazi nyumbani kwangu hapa Chugastan.

Siku moja tumeanika maharage baada ya kuvuna na tukaona kuna dalili za mvua mvua vimanyunyu kwa mbali tukaanza kutapa hofu kwamba mvua inaweza anguka na tukapata hasara.

Dada kuona tunahofu akasema hainashida akaingia jikoni akachukua chumvi akaweka kwenye kisosi akaenda kuweka nje.

Chakushangaza mvua haikunyesha tena pakawa kawaida tu na maharage yetu yakaendelea kukauka.

Sasa swali langu ni hii sayansi aliyoitumia kwakweli sijawahi kuiona na nilibaki nashangaa kweli kweli.

Je hii issue ya chumvi ni kweli inazuia mvua au ni kiini macho tu alitupiga ?
 
Wanajamvi habarini, nimekutana na kisanga kutoka kwa dada wa kazi, yeye ni mzaliwa wa Dodoma na alikuja kufanya kazi nyumbani kwangu hapa Chugastan. Siku moja tumeanika maharage baada ya kuvuna na tukaona kuna dalili za mvua mvua vimanyunyu kwa mbali tukaanza kutapa hofu kwamba mvua inaweza anguka na tukapata hasara. Dada kuona tunahofu akasema hainashida akaingia jikoni akachukua chumvi akaweka kwenye kisosi akaenda kuweka nje. Chakushangaza mvua haikunyesha tena pakawa kawaida tu na maharage yetu yakaendelea kukauka. Sasa swali langu ni hii sayansi aliyoitumia kwakweli sijawahi kuiona na nilibaki nashangaa kweli kweli. Je hii issue ya chumvi ni kweli inazuia mvua au ni kiini macho tu alitupiga ?
Hamna kitu kama hicho
 
Huenda ni kweli maana hata mtoto wa mwisho akielekeza makalio mvua inakotokea hua inakata
Watoto wa kateksta watapinga na kudai uchawi ila Afrika Kuna mambo. Hii ya mtoto wa mwisho ipo kabisa na inafanya kazi.

Wagogo pia Wana namna nyingi za kuzuia mvua ikiwemo hiyo chumvi.

Wafanyabiashara moinadani, wazee wa ccm Wana uwezo wa kuzuia mvua pia wanapokuwa na shughuli
 
Kuna njia nyingi za kuzuia mvua, kila kabila au Koo flani Wana ujuzi wao. Msidharau mambo ya asili sio uchawi jamani,Kuna miungu , lakini pia Kuna Mungu mkuu!
 
Wanajamvi habarini, nimekutana na kisanga kutoka kwa dada wa kazi, yeye ni mzaliwa wa Dodoma na alikuja kufanya kazi nyumbani kwangu hapa Chugastan. Siku moja tumeanika maharage baada ya kuvuna na tukaona kuna dalili za mvua mvua vimanyunyu kwa mbali tukaanza kutapa hofu kwamba mvua inaweza anguka na tukapata hasara. Dada kuona tunahofu akasema hainashida akaingia jikoni akachukua chumvi akaweka kwenye kisosi akaenda kuweka nje. Chakushangaza mvua haikunyesha tena pakawa kawaida tu na maharage yetu yakaendelea kukauka. Sasa swali langu ni hii sayansi aliyoitumia kwakweli sijawahi kuiona na nilibaki nashangaa kweli kweli. Je hii issue ya chumvi ni kweli inazuia mvua au ni kiini macho tu alitupiga ?
Sasa si ushaona kabisa na si kusimuliwa halafu bado unatuuliza, mkulungwa unafeli
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom