Kijakazi
JF-Expert Member
- Jun 26, 2007
- 6,409
- 8,909
Nimekuwa nikifuatilia mwenendo wa kisiasa wa CHADEMA nchini na kujiuliza kwamba Je Viongozi wa CHADEMA ni Wabinafsi?
Ni kwa nini wamejikita sana kwenye kuchukua Dola (Uraisi) kwenye Uchaguzi ujao 2015 wakati ni ukweli ulio wazi kwa mtu yoyote anayeelewa mambo yalivyo nchini Tanzania kwamba 2015 ni mapema mno kwa CHADEMA au chama chochote cha Upinzani kushinda Uraisi?
Ni kwa nini wasianzie kujijenga polepole kutoka chini kwenda juu? wana haraka gani? kwani ni ukweli ulio wazi kwamba wanahitaji kama Chaguzi mbili zijazo ili waweze kushinda Uraisi (kama wakibakia na kasi walio nayo sasa hivi) sasa ni kwa nini wasiwekeze zaidi kwa sasa kwenye kushinda kwa mfano Chaguzi za Serikali za Vijiji/Mitaa, Udiwani na mpaka Ubunge na mwishowe kwa mfano kufanikiwa kwanza kuongoza Halmashauri na Miji na kuhakikisha kwamba hizo Halmashauri au Miji wanayoiongoza inakuwa mfano ili wapate kithibitisho/kigezo cha kuwashawishi wananchi kwamba Halmashauri wanazoziongoza zinafanya vizuri kulinganisha na Halmashauri zinazooongozwa na vyama vingine.
Kigezo cha kusema 2015 ni mapema mno kwa mfano ukiangalia tu Chaguzi 2 zilizopita Arumeru na Igunga ingawaje ni kweli kwamba watu wengi wameanza kuchoshwa na baadhi ya Viongozi wa CCM lakini bado chaguzi hizo kwa kiasi fulani zimethibitisha kwamba bado watu wengi sana aidha bado wanaamini kwamba CCM ikipewa nafasi bado inaweza kujirekebisha na kufanya vizuri au bado hawajawaamini Wapinzani kiasi hicho cha kuweza kuwapa ushindi mkubwa sana kwani Arumeru ambako ndio mtu angetegemea labda CCM isiambulie kitu lakini bado waliweza kuchuana na CHADEMA sembuse sehemu nyingine za nchi?
Kwa hali ilivyo sasa hata kama CCM wakimsimamisha Bibi Kidude na wakaungana wote na kuanza kumkampenia hakuna Chama kitakachoishinda huo ni ukweli ulio wazi sasa Ni kwa nini Viongozi wa CHADEMA wamejikita sana kwenye kitu ambacho ni wazi hawawezi kushinda wana haraka gani? kwa nini wasiende pole pole?
Ni kwa nini wamejikita sana kwenye kuchukua Dola (Uraisi) kwenye Uchaguzi ujao 2015 wakati ni ukweli ulio wazi kwa mtu yoyote anayeelewa mambo yalivyo nchini Tanzania kwamba 2015 ni mapema mno kwa CHADEMA au chama chochote cha Upinzani kushinda Uraisi?
Ni kwa nini wasianzie kujijenga polepole kutoka chini kwenda juu? wana haraka gani? kwani ni ukweli ulio wazi kwamba wanahitaji kama Chaguzi mbili zijazo ili waweze kushinda Uraisi (kama wakibakia na kasi walio nayo sasa hivi) sasa ni kwa nini wasiwekeze zaidi kwa sasa kwenye kushinda kwa mfano Chaguzi za Serikali za Vijiji/Mitaa, Udiwani na mpaka Ubunge na mwishowe kwa mfano kufanikiwa kwanza kuongoza Halmashauri na Miji na kuhakikisha kwamba hizo Halmashauri au Miji wanayoiongoza inakuwa mfano ili wapate kithibitisho/kigezo cha kuwashawishi wananchi kwamba Halmashauri wanazoziongoza zinafanya vizuri kulinganisha na Halmashauri zinazooongozwa na vyama vingine.
Kigezo cha kusema 2015 ni mapema mno kwa mfano ukiangalia tu Chaguzi 2 zilizopita Arumeru na Igunga ingawaje ni kweli kwamba watu wengi wameanza kuchoshwa na baadhi ya Viongozi wa CCM lakini bado chaguzi hizo kwa kiasi fulani zimethibitisha kwamba bado watu wengi sana aidha bado wanaamini kwamba CCM ikipewa nafasi bado inaweza kujirekebisha na kufanya vizuri au bado hawajawaamini Wapinzani kiasi hicho cha kuweza kuwapa ushindi mkubwa sana kwani Arumeru ambako ndio mtu angetegemea labda CCM isiambulie kitu lakini bado waliweza kuchuana na CHADEMA sembuse sehemu nyingine za nchi?
Kwa hali ilivyo sasa hata kama CCM wakimsimamisha Bibi Kidude na wakaungana wote na kuanza kumkampenia hakuna Chama kitakachoishinda huo ni ukweli ulio wazi sasa Ni kwa nini Viongozi wa CHADEMA wamejikita sana kwenye kitu ambacho ni wazi hawawezi kushinda wana haraka gani? kwa nini wasiende pole pole?