Je, CHADEMA hawaelewi maana ya Lockdown?

Watz wengi wanajitoa ufahamu kwa kujifanya wanaiweza lockdown
 
Yohana hiki chama kinatatizo kubwa la kuwa na watu wasio uelewa. Wengi wao ni wahuni wahuni tu na walichobakiza sasa hivi ni matusi tu.
Hili janga ni baya sana linahitaji umakini na mikakati madhubuti kulidhibiti.
Wao wamekalili tu funga mipaka, weka lockdown, hawajui kuwa social distancing ni mojawapo ya njia ambayo mkiitumia vizuri mnaweza kufanikiwa. Waulize Mama lishe ambaye anapika vitumbua na mtaji wa elfu tano,ukimfungia ndani siku 30 ataishi vipi?
Sasa badala ya kuonyesha umoja na mshikamano wao wanaleta political conspiracy wakati ni janga la dunia.
Kuna mbunge alitoa hoja labda ikibidi hili li chama lifungiwe kabisa. Any way bora waliache life kwa kupigwa na wananchi mwezi October.
 
..suala hili msilifanye la CCM vs CDM.

..tuchukue ushauri kulingana na uzito na mantiki ya ushauri husika.

..huu siyo wakati wa kuchunguza ushauri unatoka ktk chama gani.
 
Unaongelea Sweden ipi mkuu? Ebu kaangalie takwimu uone, maambukizi zaidi ya watu 10,000 na vifo zaidi ya 800 halafu hao unawaona wako salama?

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu responsibility sio ya mtu moja. Wao hawajafunga kitu chochote na wanaamini njia yao ndio mbadala. Tusubiri tuone, kila nchi ni lazima ifanye vile ambavyo ni sahihi kwa raia wake. Hatuwezi kuiga nchi flani flani kwa sababu kuna tofauti kubwa sana ya maisha kati ya USA na TZ au nchi yoyote ya ulaya. Usiige tembo k*ny*
 
Ccm na wajinga wenzao wanaelewa nin.
 
serikali inayojenga miradi kwa pesa za ndani inashindwa vipi ku enject pesa kwa ajili ya raia wake waka survive kipindi cha lockdown?
 
Kwanza ukiangalia hata wanaolilia hiyo lock down ni kakikundi ka watu wachache sana ambao ni kula kulala hawaelewi maisha yanaendaje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Taarifa ya habari leo usiku inasema wamiliki wa mabasi Tanga ya kwenda mikoani wamesimamisha safari za mabasi yao baada ya kukosa abiria, sijui Chadema inahusika nini na kujifungia huku.
 
Hata serikali ingetangaza total lockdown hao hao Chadema wangepinga na kusema wananchi watapata tabu. Hao jamaa ni wa kuwasikiliza na kuwapuuza tu.
Yaani hawa jamaa hawaeleweki kipi wanakitaka. Kwao kila kitu wanataka kukifanya kiwe mtaji wa kisiasa. Yaani shida tupu
 
Hao ni kula kulala mkuu, achana nalo hilo hata hilo bando analotumia kucoment hapa amelipata baada ya kubana jero alipokuwa ametumwa gengeni kununua nyanya na dadake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sera ya Chadema hapa iwe Social Distansing kwa sababu kirusi kimeshaingia Nchini na sasa kinaambukiza
Tukifanya hivyo tutapunguza maambukizi kwa kiasi kikubwa

Huu utawala wa Wachunga Ng'ombe hauna plan yoyote na fedha walishazitumia kiholela
 
Una Akili za kiccm

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaani mtu kusema ukweli wa mambo tu kosa? By the way CCM hii awamu imebadilika sana, watu hawasikii wapigaji kama Harbinder Seth. Kinachosikika ni miradi kama Sgr,JNHHP,barabara kujengwa, Madaraja kama busisi na wami,Zahanati,vituo vya afya na hospital kwa maelfu. Shule zimekarabatiwa. Kwa ujumla mambo yamebadilika sana.
 
Mkuu please usifanyie Siasa hili Janga. Usisubiri ndugu zako waondoke ndio ujuwe ili ni janga la dunia.
Kwenye hili janga la corona achana na siasa bwashee. Acha kuingiza CCM, CUF wala CHADEMA!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…