Lissu kasema bila kupingwa kwamba kikosi kazi cha kumpiga risasi yeye, kutunga kesi, utekaji wote mpaka wa Dewji umefanywa chini ya maelekezo na usamamizi wa mtu mmoja ambaye ni Balozi Kipilimba. Hajawahi kutoka hata siku mmoja kukana chochote maana ni ukweli mtupu.
Kuna wanaofikiria alikuwa mazalendo na kufuata au kunusa hasira za Raisi bosi wake hivyo hana hatia. Wengine wanasema huwezi kufanya mauaji kwa niaba ya mtu yeyote unatakiwa kufuata katiba. Je leo hii ikigundulika kama wanavyodai anaweza kufunguliwa mashitaka? Na je huyu ni mzalendo au muuaji? Na Je aliapa kwa katiba au Raisi ?
Mimi kwa mawazo yangu na kumjua Magufuli kama kiongozi na kama familia siamini kama alimtuma huyu balozi kuuwa mtu yeyote lakini Magufuli anakuwa na hasira na anaweza kuongea vitu vya kutisha lakini siamini kama anaweza kumpigia simu na kutoa maelekezo kutoka kwenye kinywa chake kwamba fulani apigwe risasi hili ni gumu kuamini. Lakini Magufuli huyo huyo anaweza kuwasamahe na kusema tuko vitani na hawa ni kama wanajeshi wa taifa na hata ingilia kazi yao. Magufuli alikuwa na double personality.