lord atkin
Senior Member
- Sep 30, 2018
- 197
- 683
Ndugu zangu kama ilivyokawaida ile redio station pendwa super brand namba moja nchini clouds FM na clouds media, wameanza msimu mpya wa tamasha lao la fiesta.
Katika hali ya tofauti kabisa na miaka mingine tamasha hilo limeonekana kuwatoka wanajamii hivyo kupoteza mvuto kwa kiwango kikubwa.
Tamasha la fiesta mwaka huu limekosa mvuto kutokana na wasanii wanaofanya vizuri zaidi nchini kuwa wanatokea kwenye lebo ya WCB ambayo haipatani na Clouds.
Ni ukweli usiopingika kuwa ukitaja Nyimbo kumi zilizofanya vizuri nchini kwa mwaka huu basi Nyimbo zaidi ya 7 zitakuwa kutoka WCB. Ni kwa sababu hii hofu ya tamasha hilo kudoda imetanda wingu la clouds media wasione pa kushika.
Wakati hali hiyo ikiendelea msanii mashuhuri Alikiba ametangaza kuachia wimbo mpya unaoitwa Hela. Ikumbukwe kuwa mwaka jana msanii Ali Kiba alikuwa kivutio na nyota wa show ya fiesta kupitia wimbo wake wa seduce me.
Je mwaka huu pia anataka kuachia wimbo huo ili kuwasaidi fiesta na clouds media?
Atatumika mpaka lini?
Katika hali ya tofauti kabisa na miaka mingine tamasha hilo limeonekana kuwatoka wanajamii hivyo kupoteza mvuto kwa kiwango kikubwa.
Tamasha la fiesta mwaka huu limekosa mvuto kutokana na wasanii wanaofanya vizuri zaidi nchini kuwa wanatokea kwenye lebo ya WCB ambayo haipatani na Clouds.
Ni ukweli usiopingika kuwa ukitaja Nyimbo kumi zilizofanya vizuri nchini kwa mwaka huu basi Nyimbo zaidi ya 7 zitakuwa kutoka WCB. Ni kwa sababu hii hofu ya tamasha hilo kudoda imetanda wingu la clouds media wasione pa kushika.
Wakati hali hiyo ikiendelea msanii mashuhuri Alikiba ametangaza kuachia wimbo mpya unaoitwa Hela. Ikumbukwe kuwa mwaka jana msanii Ali Kiba alikuwa kivutio na nyota wa show ya fiesta kupitia wimbo wake wa seduce me.
Je mwaka huu pia anataka kuachia wimbo huo ili kuwasaidi fiesta na clouds media?
Atatumika mpaka lini?