MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,171
- 23,976
Kwa mtu anayefahamu vizuri historia ya siasa za Tanzania lazima atakuwa anafahamu vizuri historia ya UDP na sera yake ya Kujaza Mapesa.
UDP ilitikisa katika Mkoa wa Shinyanga na baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Mwanza ambapo katika Uchaguzi Mkuu wa 1995 na 2000 ilijikuta ikipata Wabunge watatu wa kuchaguliwa na mmoja wa viti maalum. Cheyo alipata kura zaidi ya 250,000 ambayo ni asilimia 6.4 ya kura zilizopigwa.
Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 ulikuwa ni mwanzo wa kuifuta UDP kama chama hai kwa sababu kilipoteza Madiwani wengi huku Mbunge akibakia mmoja.
Tatizo Kuu la UDP ilikuwa ni sera zake za kuwajaza Watanzania Mapesa ambazo zilijibiwa na Rais Kikwete baada ya kuanzisha na kusimamia sera ya kuwapa uwezo wa kifedha wajasiliamali kwenye vikundi mbali mbali. Huu ndio wakati ambapo wananchi walipokea pesa zilizoitwa "Mabilioni ya JK". Hili lilikuwa ni jeneza la kisiasa la UDP. Mwaka 2010 ikawa ndio maziko ya UDP.
Kama ilivyokuwa kwa UDP, Jeneza la kisiasa la ACT-Wazalendo naliona pia liko njiani kutokana na sera zao za Unyerere. Sera za Unyerere zimeanza kujibiwa na Rais Magufuli ndio maana viongozi wengi wa ACT-Wazalendo wanajiunga CCM.
ACT-Wazalendo ya sasa imekuwa ni chama cha mtu mmoja. Zitto Kabwe ndio Mkuu wa Chama, Katibu Mkuu, Katibu Mwenezi, Mweka Hazina, Ofisa wa mambo ya nchi za nje na Mbunge.
Kama ilivyokuwa kwa UDP iliyokuwa na Mbunge 1 na Madiwani wengi kutoka Mkoa wa Shinyanga, kwa sasa ACT-Wazalendo ina Mbunge 1 na Madiwani ambao wengi wao wako katika Mkoa wa Kigoma.
Hakuna asiyejua kuwa CCM ilikuwa inamsaidia Zitto ili ashinde chaguzi lakini kwa sasa imeanza kuachana naye!
Tumeona kwa sasa CCM wameanza kupeleka nguvu za kisiasa katika Mkoa wa Kigoma huku wakicheza michezo ya kisiasa ambayo ACT-Wazalendo hawana uzoefu nayo.
Mchezo mmoja wa kisiasa ni pale ambapo ACT-Wazalendo wamejikuta wakiingia kwenye mtego wa kisiasa kwa kupandisha malipo ya kodi za vibanda kwenye Manispaa ya Kigoma Ujiji bila kufanya makubaliano na wafanyabiashara halafu CCM wakamtuma Katibu Mwenezi, Polepole kwenda kuongea na "wanaCCM" wa mkoa wa Kigoma kwa kigezo cha ufuatiliaji wa Ilani ya Uchaguzi.
ACT-Wazalendo walichoshindwa kuelewa ni kuwa pamoja na kwamba wao ndio wanaongoza Manispaa lakini hawana nguvu za mwisho kisheria katika utungaji wa sheria ndogo ndogo na utekelezaji wake lakini kikubwa zaidi waliomba kuchaguliwa ili kuondoa kero na sio kuongeza kero.
Polepole atatoa tamko la kuiamuru serikali izifute sheria hizo mpya kwa sababu ni kero na zinaumiza wafanyabiashara na serikali itakubali huku lawama za kisiasa zitawaangukia ACT-Wazalendo. Huu ni mtaji wa CCM katika Uchaguzi 2019 na 2020 kwenye Udiwani na bunge. ACT-Wazalendo iliyokuwa inaonekana ni mkombozi wa wana Kigoma itajikuta inaonekana ni chama kisichosikiliza kilio cha wananchi na kinaongeza kero.
Hakuna asiyejua kuwa wana Kigoma huwa hawakopeshi kwenye siasa. Hawana tabia ya kumchagua Diwani au Mbunge zaidi ya vipindi viwili ndio maana Zitto alikimbia Jimbo la Kigoma Kaskazini na kwenda Kigoma Mjini.
Takwimu pia zinaonyesha Mkoa wa Kigoma ni moja ya Mikoa ambayo Rais Magufuli anapendwa sana na watu wengi.
Zitto na ACT-Wazalendo wanapambana na msemo wa Waingereza usemao, " If your adversaries are stronger than you, it is better to join their side".
UDP ilitikisa katika Mkoa wa Shinyanga na baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Mwanza ambapo katika Uchaguzi Mkuu wa 1995 na 2000 ilijikuta ikipata Wabunge watatu wa kuchaguliwa na mmoja wa viti maalum. Cheyo alipata kura zaidi ya 250,000 ambayo ni asilimia 6.4 ya kura zilizopigwa.
Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 ulikuwa ni mwanzo wa kuifuta UDP kama chama hai kwa sababu kilipoteza Madiwani wengi huku Mbunge akibakia mmoja.
Tatizo Kuu la UDP ilikuwa ni sera zake za kuwajaza Watanzania Mapesa ambazo zilijibiwa na Rais Kikwete baada ya kuanzisha na kusimamia sera ya kuwapa uwezo wa kifedha wajasiliamali kwenye vikundi mbali mbali. Huu ndio wakati ambapo wananchi walipokea pesa zilizoitwa "Mabilioni ya JK". Hili lilikuwa ni jeneza la kisiasa la UDP. Mwaka 2010 ikawa ndio maziko ya UDP.
Kama ilivyokuwa kwa UDP, Jeneza la kisiasa la ACT-Wazalendo naliona pia liko njiani kutokana na sera zao za Unyerere. Sera za Unyerere zimeanza kujibiwa na Rais Magufuli ndio maana viongozi wengi wa ACT-Wazalendo wanajiunga CCM.
ACT-Wazalendo ya sasa imekuwa ni chama cha mtu mmoja. Zitto Kabwe ndio Mkuu wa Chama, Katibu Mkuu, Katibu Mwenezi, Mweka Hazina, Ofisa wa mambo ya nchi za nje na Mbunge.
Kama ilivyokuwa kwa UDP iliyokuwa na Mbunge 1 na Madiwani wengi kutoka Mkoa wa Shinyanga, kwa sasa ACT-Wazalendo ina Mbunge 1 na Madiwani ambao wengi wao wako katika Mkoa wa Kigoma.
Hakuna asiyejua kuwa CCM ilikuwa inamsaidia Zitto ili ashinde chaguzi lakini kwa sasa imeanza kuachana naye!
Tumeona kwa sasa CCM wameanza kupeleka nguvu za kisiasa katika Mkoa wa Kigoma huku wakicheza michezo ya kisiasa ambayo ACT-Wazalendo hawana uzoefu nayo.
Mchezo mmoja wa kisiasa ni pale ambapo ACT-Wazalendo wamejikuta wakiingia kwenye mtego wa kisiasa kwa kupandisha malipo ya kodi za vibanda kwenye Manispaa ya Kigoma Ujiji bila kufanya makubaliano na wafanyabiashara halafu CCM wakamtuma Katibu Mwenezi, Polepole kwenda kuongea na "wanaCCM" wa mkoa wa Kigoma kwa kigezo cha ufuatiliaji wa Ilani ya Uchaguzi.
ACT-Wazalendo walichoshindwa kuelewa ni kuwa pamoja na kwamba wao ndio wanaongoza Manispaa lakini hawana nguvu za mwisho kisheria katika utungaji wa sheria ndogo ndogo na utekelezaji wake lakini kikubwa zaidi waliomba kuchaguliwa ili kuondoa kero na sio kuongeza kero.
Polepole atatoa tamko la kuiamuru serikali izifute sheria hizo mpya kwa sababu ni kero na zinaumiza wafanyabiashara na serikali itakubali huku lawama za kisiasa zitawaangukia ACT-Wazalendo. Huu ni mtaji wa CCM katika Uchaguzi 2019 na 2020 kwenye Udiwani na bunge. ACT-Wazalendo iliyokuwa inaonekana ni mkombozi wa wana Kigoma itajikuta inaonekana ni chama kisichosikiliza kilio cha wananchi na kinaongeza kero.
Hakuna asiyejua kuwa wana Kigoma huwa hawakopeshi kwenye siasa. Hawana tabia ya kumchagua Diwani au Mbunge zaidi ya vipindi viwili ndio maana Zitto alikimbia Jimbo la Kigoma Kaskazini na kwenda Kigoma Mjini.
Takwimu pia zinaonyesha Mkoa wa Kigoma ni moja ya Mikoa ambayo Rais Magufuli anapendwa sana na watu wengi.
Zitto na ACT-Wazalendo wanapambana na msemo wa Waingereza usemao, " If your adversaries are stronger than you, it is better to join their side".