Jasusi Honda ndani ya mpango wa Congo

Riwaya : Mpango wa Congo

Na Bahati Mwamba

Simu: 0758573660


Hii ni sehemu ya tisa


Wakati akili ikitafakari maamuzi; macho yakanasa kitu ukutani juu kidogo ya mto na mto huo ulionekana ndio ulikuwa unatumiwa na marehemu Bulembo kwa kuwa ulikuwa unaonekana kuwa na mafuta ya nywele yaliotengeneza weusi kidogo kwa kulaliwa mara kwa mara.
Juu kidogo ya tendegu la kitanda aliona mikwaruzo, akasogea kwa hatua za aste aste na alipofikia karibu aliona maandishi ila yalikuwa ni maandishi yale yale alioyaona kwenye kikaratasi alichokitafuna wakati akiwa mikononi mwa Sajini Kebu.

Na yalikuwa yamepangiliwa vile vile kama yalivyokuwa kwenye karatasi alioitafuna.

“142BOULEVARD DU JUIN
B. P. 1612
KINSHASA CONGO (81)”

Aliyatazama tena maandishi yale, bado hakuwa amepata walau wazo la kujua Bulembo alitaka kumaanisha nini japo alijua hii ilikuwa ni anuani ya ubalozi wa Tanzania Lakini kilichomchangaya zaidi ni ile alama ya mabano kisha zikafuatia namba (81) ilimaanisha nini hii namba! Hakujua wala kufikiria mbali zaidi ya kuzidi kuchanganyikiwa na asijue afuate lipi katika anuani ile.

Honda alitoka pale kitandani, kisha akataka kutoka nje ya chumba kile lakini akasita.

Kuna sehemu alikuwa hajafikia mle ndani.

Godoro!!!

Hakuwa ameligusa kabisa lile godoro juu ya kitanda, akarudi na kulitoa shuka yake.
Macho yake yakaambulia patupu, akaamua kulitoa lote.

Aliona!

Macho yake yalikutana na karatasi nyeupe ikiwa imepachikwa kwenye kingo ya chaga,wala haikuonekana kuwekwa siku nyingi mana ilikuwa bado inamwonekano wa kuridhisha machoni.

“Ina maana alijua atakufa?” Alijiuliza Honda kisha akakichukua kikaratasi kile ambacho kilikuwa kimekatwa upande hivyo kupunguza ukubwa wake.

Akakifunua!

Kilikuwa kimeandikwa kwa mafumbo au kwa lugha ya kijasusi ‘code' lakini fumbo lilikuwa katika lugha rahisi ila ngumu kutafsirika.

Iliandikwa katika muundo wa mduara ila katika kila neno kulikuwa kuna mduara mwingine mdogo kumaanisha kila neno lilikuwa linajitegemea ila katika muunganiko mmoja.

Honda alirudia maneno yale.

“MTANZANIA X” kisha yakazungushiwa duara na ukafuata msitari ambapo ulikutana na mduara uliokuwa na neno lingine lililosomeka

“MAKANISA MATATU”

Kisha ukafuatia msitari mwingine ambapo nao ulienda kukutana na kiduara kilichokuwa na maneno

‘CLUB X'

Kisha ukafuatia mstari mwingine ulienda kuungana ni kiduara cha maneno ya kwanza.

Lakini kulikuwa na duara kubwa lililozunguka kiduara chenye muunganiko wa viduara vitatu na juu ya mduara ule kulikuwa na maneno makubwa yaliokuwa yameandikwa kwa kukolezwa.

“MPANGO WA CONGO”

Yote hayo aliyasoma kwa umakini wa hali ya juu huku akili yake ikijaribu kupambanua nini kilimanishwa kwenye mchoro ule.

hakika alipagawa!

Lakini alikumbuka pale ndani anamateka, haraka akatoka kule chumbani na kwenda chumba kingine alikokuwa amemfunga mateka wake.

Alipoingia akakuta mateka akiwa amesharejewa na fahamu.

Akamtazama kwanza!

Kisha akavuta kiti na kukaa mbele ya mateka wake.

“Mlifuata nini pale Tunde” aliuliza Honda.

“Tulikufuata wewe” alijibu mateka.

“Nani aliwatuma” Honda aliendelea kusaili.

“Mr X” alijibu mateka

Jibu la mateka lilimuinua kwenye kiti Honda,na hii ni kwa kuwa dakika chache tu katoka kuliona hilo jina X kwenye karatasi ilioachwa na Bulembo tena likiwa limesomeka mara mbili.

Mwanzo ilitanguliwa na Mtanzania kisha Club na sasa Mr.

Je X inatumika kote huko na X ndie mhusika mkuu? Sasa kama X ni mtu na ndie kiongozi, kwa nini awe mtanzania ikiwa mpango upo chini ya mtu aliewahi kusemekana kufa ila hakuwa mtanzania!?” alijiuliza Honda huku akimtizama mateka wake bila kusema lolote.

Pagumu!!!.

*****

.MWANZA TANZANIA.

Remi alibaki akiwa mgongoni mwa Mtega nyoka, mtu waliekutana ndani ya ofisi za Kasuku contractors.

Hakutaka kuamini kuwa mtu mgeni yule alieingilia ugonvi wake na mtekaji angeliweza kumdhibiti mtekaji ambae yeye alijua uwezo na ukatili wake kuliko mtu yoyote aliekuwa eneo lile.

Remi aliona ni kama mtetezi wake ameingilia jambo gumu asilojua uzito wake.

Akajisogeza nyuma zaidi huku akiomba watu wazidi kuongezeka eneo lile apate wepesi wa kuchomoka pale.

Mtekaji ni kama alikuwa anazihesabu karata za Remi kichwani pake.
Hivyo wakati Remi anapiga hatua moja nyuma, tayari mtekaji alikuwa anatarajia hilo na kwa kuwa mbele yake kulikuwa na mtu tata alietokea kutibua mpango wake, hakutaka akwamishwe nae na hatimae kumkosa Remi kwa mara nyingine.

Alimchukulia poa Mtega nyoka.

Kwa kasi ya aina yake, mtu yule mrefu na mwembamba akatisha kama anataka kushambulia,ila akagairi gafla na tayari hila zake zilikuwa zimezaa matunda kwa kumtikisa kidogo Mtega nyoka.

Mtu yule akampita kwa kasi ile ile Mtega nyoka; lengo likiwa ni kumfikia Remi kabla hajatokomea tena.

Ila hakufika mbali akajikuta akipaa na kudondokea tumbo na hii ni bada ya kupigwa mtama safi na Mtega nyoka.

Mtega nyoka hakutaka kumfuata pale chini akamngoja asimame.

Mtekaji akasimama kwa mbwembwe kisha akamgeukia Mtega nyoka kwa gadhabu na kwa kuokoa muda akaenda mzimamzima
Kwa kushambulia kwa mtindo wa haraka haraka, lakini mapigo yote; Honda aliyaona vyema na kuyapangua kisha akaachia konde safi lilitua kifuani mwa mtekaji na kumyumbisha kidogo lakini halikutoa madhara makubwa.

Watu walizidi kushangilia na wengine kupiga picha za video bila kujua kitu gani hasa kinaendelea zaidi ya kuona mapigano kama muvi za Jet Lee.

Makelele na simu za watu zilizidi kumchanganya mtekaji mana hakutaka kabisa hilo litokee ila kukua kwa techonolijia na eneo walipokuwa lilirahisisha asichokitaka kitokee.

Akanesa kidogo kisha akawa kama anapeleka teke la kulia na alipoona Mtega nyoka ameingia kwenye mtego wake akaachia konde zito lililotua sawia kwenye paji la uso la Mtega nyoka.

Mtega nyoka alijikuta akiona nyota nyota na alipojaribu kufumba macho alijikuta anaambulia kuona mashilingi mengi na alipofumbua macho akaona ni kama umati wa watu unaiba shilingi alizoona.

Akagwaya!

Mtekaji alitaka kutumia nafasi ile kummaliza Mtega nyoka, lakini kabla hajatimiza lengo lake mara ukasikika mlipuko wa risasi na kuzua taharuki kwa watu waliokua pale huku kila mmoja akijaribu kuokoa uhai wake.
Mtekaji alibabaika kidogo lakini punde akasikia mvumo wa pikipiki anayoijua haraka akapiga tambo kubwa huku akikwepa konde lililotupwa na Mtega nyoka na tambo la pili lilimfikisha juu ya pikipiki huku nyuma zikisikika tena risasi kadhaa.

Mtega nyoka alishuhudia pikipiki isio kuwa na namba za usajili ikitokomea kuelekea katikati ya mji.

Jicho la Mtega nyoka likabaki likiangaza alipo binti asie jua kusoma wala asimuone.

Akah!!

“yuko wapi tena?” alijiuliza huku akianza kupiga hatua huku macho yake yakiwa yanaangaza huku na huko miongoni mwa watu waliokuwa wanakimbia milio ya risasi.

“Tulia na nyoosha mikono juu!” ilisikika sauti ya kimamlaka ikamuamuru Mtega nyoka.

Mtega nyoka aligeuka taratibu huku aking’ata meno kwa gadhabu.

Alipotulia macho yake yakakutana na mitutu miwili ya bunduki kutoka kwa askari wawili ambao aliwatambua ni waliokuwa wanalinda benki ya NMB.

“Amani afande” alisema Mtega nyoka huku akiingiza mkono mfukoni na alipotoa alikuwa na kitambulisho rasimi cha kazi yake.

Kilichofuata ni saluti kutoka kwa askari wale. Mtega nyoka hakujali saluti zao aligeuka na kujichanganya kwenye umati wa watu ulioanza kujikusanya tena huku kwa mbali akisikia king’ora cha gari la polisi kilisikika kikija eneo lile hivyo akajua askari wale watakuwa waliomba usaidizi makao makuu kwa kudhani wao ni wezi wakiwa wanapanga kuiba benki.




Itaendelea..



Nb: Nashukuru sana kwa sapoti mliooonesha leo na jana lakini pia kwa maoni yenu nami nawaahidi sitawaangusha nitafanya kadri ya uwezo wangu ili nanyi mridhike, vipande viwili kuanzia kesho vitakuwa vikiwekwa hapa...

Ambao bado mnapita kimya, tafadhalini toeni sapoti nami nipate moyo wa kuwaburudisheni..

Karibuni
 
Riwaya : Mpango wa Congo

Na Bahati Mwamba

Simu: 0758573660


Hii ni sehemu ya tisa


Wakati akili ikitafakari maamuzi; macho yakanasa kitu ukutani juu kidogo ya mto na mto huo ulionekana ndio ulikuwa unatumiwa na marehemu Bulembo kwa kuwa ulikuwa unaonekana kuwa na mafuta ya nywele yaliotengeneza weusi kidogo kwa kulaliwa mara kwa mara.
Juu kidogo ya tendegu la kitanda aliona mikwaruzo, akasogea kwa hatua za aste aste na alipofikia karibu aliona maandishi ila yalikuwa ni maandishi yale yale alioyaona kwenye kikaratasi alichokitafuna wakati akiwa mikononi mwa Sajini Kebu.

Na yalikuwa yamepangiliwa vile vile kama yalivyokuwa kwenye karatasi alioitafuna.

“142BOULEVARD DU JUIN
B. P. 1612
KINSHASA CONGO (81)”

Aliyatazama tena maandishi yale, bado hakuwa amepata walau wazo la kujua Bulembo alitaka kumaanisha nini japo alijua hii ilikuwa ni anuani ya ubalozi wa Tanzania Lakini kilichomchangaya zaidi ni ile alama ya mabano kisha zikafuatia namba (81) ilimaanisha nini hii namba! Hakujua wala kufikiria mbali zaidi ya kuzidi kuchanganyikiwa na asijue afuate lipi katika anuani ile.

Honda alitoka pale kitandani, kisha akataka kutoka nje ya chumba kile lakini akasita.

Kuna sehemu alikuwa hajafikia mle ndani.

Godoro!!!

Hakuwa ameligusa kabisa lile godoro juu ya kitanda, akarudi na kulitoa shuka yake.
Macho yake yakaambulia patupu, akaamua kulitoa lote.

Aliona!

Macho yake yalikutana na karatasi nyeupe ikiwa imepachikwa kwenye kingo ya chaga,wala haikuonekana kuwekwa siku nyingi mana ilikuwa bado inamwonekano wa kuridhisha machoni.

“Ina maana alijua atakufa?” Alijiuliza Honda kisha akakichukua kikaratasi kile ambacho kilikuwa kimekatwa upande hivyo kupunguza ukubwa wake.

Akakifunua!

Kilikuwa kimeandikwa kwa mafumbo au kwa lugha ya kijasusi ‘code' lakini fumbo lilikuwa katika lugha rahisi ila ngumu kutafsirika.

Iliandikwa katika muundo wa mduara ila katika kila neno kulikuwa kuna mduara mwingine mdogo kumaanisha kila neno lilikuwa linajitegemea ila katika muunganiko mmoja.

Honda alirudia maneno yale.

“MTANZANIA X” kisha yakazungushiwa duara na ukafuata msitari ambapo ulikutana na mduara uliokuwa na neno lingine lililosomeka

“MAKANISA MATATU”

Kisha ukafuatia msitari mwingine ambapo nao ulienda kukutana na kiduara kilichokuwa na maneno

‘CLUB X'

Kisha ukafuatia mstari mwingine ulienda kuungana ni kiduara cha maneno ya kwanza.

Lakini kulikuwa na duara kubwa lililozunguka kiduara chenye muunganiko wa viduara vitatu na juu ya mduara ule kulikuwa na maneno makubwa yaliokuwa yameandikwa kwa kukolezwa.

“MPANGO WA CONGO”

Yote hayo aliyasoma kwa umakini wa hali ya juu huku akili yake ikijaribu kupambanua nini kilimanishwa kwenye mchoro ule.

hakika alipagawa!

Lakini alikumbuka pale ndani anamateka, haraka akatoka kule chumbani na kwenda chumba kingine alikokuwa amemfunga mateka wake.

Alipoingia akakuta mateka akiwa amesharejewa na fahamu.

Akamtazama kwanza!

Kisha akavuta kiti na kukaa mbele ya mateka wake.

“Mlifuata nini pale Tunde” aliuliza Honda.

“Tulikufuata wewe” alijibu mateka.

“Nani aliwatuma” Honda aliendelea kusaili.

“Mr X” alijibu mateka

Jibu la mateka lilimuinua kwenye kiti Honda,na hii ni kwa kuwa dakika chache tu katoka kuliona hilo jina X kwenye karatasi ilioachwa na Bulembo tena likiwa limesomeka mara mbili.

Mwanzo ilitanguliwa na Mtanzania kisha Club na sasa Mr.

Je X inatumika kote huko na X ndie mhusika mkuu? Sasa kama X ni mtu na ndie kiongozi, kwa nini awe mtanzania ikiwa mpango upo chini ya mtu aliewahi kusemekana kufa ila hakuwa mtanzania!?” alijiuliza Honda huku akimtizama mateka wake bila kusema lolote.

Pagumu!!!.

*****

.MWANZA TANZANIA.

Remi alibaki akiwa mgongoni mwa Mtega nyoka, mtu waliekutana ndani ya ofisi za Kasuku contractors.

Hakutaka kuamini kuwa mtu mgeni yule alieingilia ugonvi wake na mtekaji angeliweza kumdhibiti mtekaji ambae yeye alijua uwezo na ukatili wake kuliko mtu yoyote aliekuwa eneo lile.

Remi aliona ni kama mtetezi wake ameingilia jambo gumu asilojua uzito wake.

Akajisogeza nyuma zaidi huku akiomba watu wazidi kuongezeka eneo lile apate wepesi wa kuchomoka pale.

Mtekaji ni kama alikuwa anazihesabu karata za Remi kichwani pake.
Hivyo wakati Remi anapiga hatua moja nyuma, tayari mtekaji alikuwa anatarajia hilo na kwa kuwa mbele yake kulikuwa na mtu tata alietokea kutibua mpango wake, hakutaka akwamishwe nae na hatimae kumkosa Remi kwa mara nyingine.

Alimchukulia poa Mtega nyoka.

Kwa kasi ya aina yake, mtu yule mrefu na mwembamba akatisha kama anataka kushambulia,ila akagairi gafla na tayari hila zake zilikuwa zimezaa matunda kwa kumtikisa kidogo Mtega nyoka.

Mtu yule akampita kwa kasi ile ile Mtega nyoka; lengo likiwa ni kumfikia Remi kabla hajatokomea tena.

Ila hakufika mbali akajikuta akipaa na kudondokea tumbo na hii ni bada ya kupigwa mtama safi na Mtega nyoka.

Mtega nyoka hakutaka kumfuata pale chini akamngoja asimame.

Mtekaji akasimama kwa mbwembwe kisha akamgeukia Mtega nyoka kwa gadhabu na kwa kuokoa muda akaenda mzimamzima
Kwa kushambulia kwa mtindo wa haraka haraka, lakini mapigo yote; Honda aliyaona vyema na kuyapangua kisha akaachia konde safi lilitua kifuani mwa mtekaji na kumyumbisha kidogo lakini halikutoa madhara makubwa.

Watu walizidi kushangilia na wengine kupiga picha za video bila kujua kitu gani hasa kinaendelea zaidi ya kuona mapigano kama muvi za Jet Lee.

Makelele na simu za watu zilizidi kumchanganya mtekaji mana hakutaka kabisa hilo litokee ila kukua kwa techonolijia na eneo walipokuwa lilirahisisha asichokitaka kitokee.

Akanesa kidogo kisha akawa kama anapeleka teke la kulia na alipoona Mtega nyoka ameingia kwenye mtego wake akaachia konde zito lililotua sawia kwenye paji la uso la Mtega nyoka.

Mtega nyoka alijikuta akiona nyota nyota na alipojaribu kufumba macho alijikuta anaambulia kuona mashilingi mengi na alipofumbua macho akaona ni kama umati wa watu unaiba shilingi alizoona.

Akagwaya!

Mtekaji alitaka kutumia nafasi ile kummaliza Mtega nyoka, lakini kabla hajatimiza lengo lake mara ukasikika mlipuko wa risasi na kuzua taharuki kwa watu waliokua pale huku kila mmoja akijaribu kuokoa uhai wake.
Mtekaji alibabaika kidogo lakini punde akasikia mvumo wa pikipiki anayoijua haraka akapiga tambo kubwa huku akikwepa konde lililotupwa na Mtega nyoka na tambo la pili lilimfikisha juu ya pikipiki huku nyuma zikisikika tena risasi kadhaa.

Mtega nyoka alishuhudia pikipiki isio kuwa na namba za usajili ikitokomea kuelekea katikati ya mji.

Jicho la Mtega nyoka likabaki likiangaza alipo binti asie jua kusoma wala asimuone.

Akah!!

“yuko wapi tena?” alijiuliza huku akianza kupiga hatua huku macho yake yakiwa yanaangaza huku na huko miongoni mwa watu waliokuwa wanakimbia milio ya risasi.

“Tulia na nyoosha mikono juu!” ilisikika sauti ya kimamlaka ikamuamuru Mtega nyoka.

Mtega nyoka aligeuka taratibu huku aking’ata meno kwa gadhabu.

Alipotulia macho yake yakakutana na mitutu miwili ya bunduki kutoka kwa askari wawili ambao aliwatambua ni waliokuwa wanalinda benki ya NMB.

“Amani afande” alisema Mtega nyoka huku akiingiza mkono mfukoni na alipotoa alikuwa na kitambulisho rasimi cha kazi yake.

Kilichofuata ni saluti kutoka kwa askari wale. Mtega nyoka hakujali saluti zao aligeuka na kujichanganya kwenye umati wa watu ulioanza kujikusanya tena huku kwa mbali akisikia king’ora cha gari la polisi kilisikika kikija eneo lile hivyo akajua askari wale watakuwa waliomba usaidizi makao makuu kwa kudhani wao ni wezi wakiwa wanapanga kuiba benki.




Itaendelea..



Nb: Nashukuru sana kwa sapoti mliooonesha leo na jana lakini pia kwa maoni yenu nami nawaahidi sitawaangusha nitafanya kadri ya uwezo wangu ili nanyi mridhike, vipande viwili kuanzia kesho vitakuwa vikiwekwa hapa...

Ambao bado mnapita kimya, tafadhalini toeni sapoti nami nipate moyo wa kuwaburudisheni..

Karibuni

Mzigo umesisisma sema tu unatoka kidogo kidogo sana haikati KIU Kabisa
 
Riwaya : mpango Congo

Sehemu ya kumi



Kilichofuata ni saluti kutoka kwa askari wale. Mtega nyoka hakujali saluti zao aligeuka na kujichanganya kwenye umati wa watu ulioanza kujikusanya tena huku kwa mbali akisikia king’ora cha gari la polisi kilisikika kikija eneo lile hivyo akajua askari wale watakuwa waliomba usaidizi makao makuu kwa kudhani wao ni wezi wakiwa wanapanga kuiba benki.

***
Dakika kumi badae Mtega nyoka alikuwa ndani ya nyumba ya kulala wageni ya D8,pembezoni kidogo mwa stendi ya mabasi ya Buzuruga.

Akilini mwake aliona mapicha ambayo hakujua yana mana gani.

Kwanza ni operesheni yake maalumu ya kuwatafuta wahandisi watatu waliohusika katika ujenzi wa jengo fulani, na kabla hajawafikia akakutana na maiti zao.

Nani alieua;? Hakumjua.

Pili ni wakati akijaribu kutafuta fununu za wahusika wa mauaji yale na kujua sababu za mauaji, mara anakutana na binti wa ajabu anaeandamwa na watu wa ajabu.

Lakini kilichomumiza zaidi ni kuwa wote wawili walijikuta ndani ya ofisi za Kasuku contractors huku wote wakimuulizia Malima.

“Kuna nini Kati ya Malima na yule dada?” alijiuliza huku akiwa anatizama uso wake kwenye kioo kikubwa kilichokuwa ndani ya chumba alichokuwamo.
Akavuta pumzi nyingi na kuzishusha kwa nguvu, hapo ndipo alipohisi maumivu katikati ya paji la uso alipopigwa ngumi na mtekaji.

Akatabasamu!!.

Jamaa anangumi kavu” akajisemea huku akitoka kujitazama na kwenda kukaa kitandani.

Mara wazo likamjia.

Haraka akanyanyuka na kuvaa nguo na kisha akavaa raba safi nyeusi ilioendana na rangi ya fulana nyeusi aliokuwa amevaa, kisha akavaa kofia Kaki iloendana na suruali aliokuwa amevaa kisha akajitazama kwenye kioo.

Akajicheka mwenyewe!.

Hakuwa amevaa mpangilio sahihi wa rangi za mavazi yake.

“Nianzie wapi sasa!” alijiuliza mara bada ya kuongezeka wazo la pili tofauti na la awali..

Hatimae akanyakua simu yake na kutaka kupiga hatua ili atoke nje.

Simu ikaita.

Alipotizama mpigaji, sura yake ikajikunja kwa fadhaa huku akilini akijishauri namna ya kumjibu mpigaji.

Hatimae akapokea.

“Kimya sana mtegaji!’” iliunguruma sauti ya Mzee Kinyonga.

“Hali tete Mzee, ila nipo njia moja” alisema Mtega nyoka.

Ukapita ukimya wa sekunde kadhaa.

“Hali imeshavuka Def Cond 0002” alisema Kinyonga.

Mtega nyoka akatumbua macho na asione alichokitumbulia.

Hii ilikuwa mpya kwake.

“ina maana ilishaanza Def Cond 0001 na sasa inavuka 0002?” aliuliza Mtega nyoka

“Lakini sio ile unayoijua wewe” alisema Mtega nyoka.

Hapo tena Mtega nyoka akakwama sauti kisha akamsikia Kinyonga akiendelea kuelezea…

“ Hii Def inaandaa Def cond 0008,na sio kama ni ya ndani; la hasha, hii ni ya kutokea nje ikihusisha watu wa ndani, hivyo basi kipimo changu kinasoma 0002 bado ni kimya kimya” alifafanua Mzee Kinyonga.


“ooh Sawa nimeelewa, kwa hiyo, kwa huo mkia umeonekana au kichwa ndo kimeonekana” aliuliza Mtega nyoka.

“aaah Mtega nyoka!!; kwani lini umeanza kuniuliza habari za kina nyoka mimi Kinyonga?” alilalama Mzee kinyonga.

Mtega nyoka, aliamua kukaa kimya mana alijua jukumu bado ni lake yeye kapewa tu fununu.

Na kikubwa aliwaza uzito wa kipimo alichodokezewa yani Def cond.
Def cond(defence control) ni kipimo cha migogoro ndani ya serikali huku kikianza na 1-8,sasa Mtega nyoka alikuwa ameambiwa hii Def cond sio anayoijua, hivyo basi katika uelewa wake alijua ya kuwa kuna mipango ya usaliti inafanyika kuiangusha serikali, mana def ilikadiriwa kuelekea def cond 0008 kumaanisha huko kunafukuta Vita kamili.
Lakini pia aliambiwa yakuwa kuna watu ndani na nje katika mipango hiyo na yeye ndo anapaswa kuwatafuta.

Akatabasamu hasa alipokumbuka vifo vya wahandisi, siku moja iliopita.

Fumbo!!

Hiyo ilimaanisha kuna fumbo lipo ndani ya kampuni ya Kasuku contractors lakini swali likabaki kwake.

Kwa nini Kasuku?

Na lilikuwa swali la msingi yeye kujiuliza kwa sababu Kasuku wanahusika na uchoraji na ujenzi wa majengo, lakini hata jengo lililojengwa nao lililomhusisha Mtega nyoka wao wajengaji hawakujua ni la nini lakini pia ramani ya jengo hawakuwa nayo yote.

Sasa ni vipi Kasuku wahusike na sakata gumu vile?

Mtego!!

Akajiwazia huku akipiga hatua kutoka ndani ya chumba alichokuwamo.

***

Safari yake ilimfikisha hadi soko dogo la machinjioni Mandu, kisha huko akaungana na wasafiri wengine kupanda daladala za kwenda kisasa kulikokuwa na mazishi ya mmoja wahandisi wa kampuni ya Kasuku.

Alichagua kwenda hapa, sababu wengine walisafirishwa mikoani kwao kwa ajili ya maziko.

Alifika mazishini na kushuhudia umati wa watu wengi sana ukiwa umejuimuika pamoja huku baadhi ya watu wakiwa wamejitenga huku na huko.

Msiba ulikuwa umepokea watu wa kila aina huku magari ya kifahari yakiwa yametapakaa kila sehemu hii ilimaanisha aliefariki alikuwa ni mtu wa watu lakini pia alikuwa ni mwenye kujiweza kifedha..

Roho ilimuuma mtega nyoka hasa aliposikia sauti za akina mama wakiomboleza.

“kwanini waluwawa watu hawa?” alijiuliza mtega nyoka bila kupata majibu.

“mtuhumiwa wa kwanza yupo kwetu au yupo ndani ya Kasuku” alizidi kuwaza mtega nyoka huku akipepesa macho huku na huko na hapo akaona vijana wa usalama kadhaa wakiwa katika majukumu yao ya kufuatilia kesi ile.

Akaachana nao na macho yake yakagota kwa kijana mmoja mtanashati akiwa amekaa na vijana wengine wawili wakijadili jambo huku mara kadhaa wakionekana kufurahia walichokuwa wanakijadili.

Lakini wakiwa katikati ya majadiliano mara akaja binti mmoja na kumuita yule kijana mtanashati alietizamwa na Mtega nyoka.

Yule kijana akaenda kumsikiliza yule binti, huku maongezi yao yakionekana kuwa ya utata upande mmoja kwani binti aliongea kwa kubabaika ama kuchanganywa na jambo huku kijana wa kiume akiwa makini kusikiliza.

Mtega nyoka akavuta hatua kujipitisha karibu yao, lakini kabla hajawafikia tayari walikuwa wamekwisha kuongozana kutoka eneo lile.

“una nini Malima!!” alijisemea Mtega nyoka huku akiangaza huku na huko ili aone kama kulikuwa kuna mtu mwingine aliekuwa anafuatilia nyendo za kijana yule.

Alimuona!!
 
Riwaya : mpango Congo

Sehemu ya kumi



Kilichofuata ni saluti kutoka kwa askari wale. Mtega nyoka hakujali saluti zao aligeuka na kujichanganya kwenye umati wa watu ulioanza kujikusanya tena huku kwa mbali akisikia king’ora cha gari la polisi kilisikika kikija eneo lile hivyo akajua askari wale watakuwa waliomba usaidizi makao makuu kwa kudhani wao ni wezi wakiwa wanapanga kuiba benki.

***
Dakika kumi badae Mtega nyoka alikuwa ndani ya nyumba ya kulala wageni ya D8,pembezoni kidogo mwa stendi ya mabasi ya Buzuruga.

Akilini mwake aliona mapicha ambayo hakujua yana mana gani.

Kwanza ni operesheni yake maalumu ya kuwatafuta wahandisi watatu waliohusika katika ujenzi wa jengo fulani, na kabla hajawafikia akakutana na maiti zao.

Nani alieua;? Hakumjua.

Pili ni wakati akijaribu kutafuta fununu za wahusika wa mauaji yale na kujua sababu za mauaji, mara anakutana na binti wa ajabu anaeandamwa na watu wa ajabu.

Lakini kilichomumiza zaidi ni kuwa wote wawili walijikuta ndani ya ofisi za Kasuku contractors huku wote wakimuulizia Malima.

“Kuna nini Kati ya Malima na yule dada?” alijiuliza huku akiwa anatizama uso wake kwenye kioo kikubwa kilichokuwa ndani ya chumba alichokuwamo.
Akavuta pumzi nyingi na kuzishusha kwa nguvu, hapo ndipo alipohisi maumivu katikati ya paji la uso alipopigwa ngumi na mtekaji.

Akatabasamu!!.

Jamaa anangumi kavu” akajisemea huku akitoka kujitazama na kwenda kukaa kitandani.

Mara wazo likamjia.

Haraka akanyanyuka na kuvaa nguo na kisha akavaa raba safi nyeusi ilioendana na rangi ya fulana nyeusi aliokuwa amevaa, kisha akavaa kofia Kaki iloendana na suruali aliokuwa amevaa kisha akajitazama kwenye kioo.

Akajicheka mwenyewe!.

Hakuwa amevaa mpangilio sahihi wa rangi za mavazi yake.

“Nianzie wapi sasa!” alijiuliza mara bada ya kuongezeka wazo la pili tofauti na la awali..

Hatimae akanyakua simu yake na kutaka kupiga hatua ili atoke nje.

Simu ikaita.

Alipotizama mpigaji, sura yake ikajikunja kwa fadhaa huku akilini akijishauri namna ya kumjibu mpigaji.

Hatimae akapokea.

“Kimya sana mtegaji!’” iliunguruma sauti ya Mzee Kinyonga.

“Hali tete Mzee, ila nipo njia moja” alisema Mtega nyoka.

Ukapita ukimya wa sekunde kadhaa.

“Hali imeshavuka Def Cond 0002” alisema Kinyonga.

Mtega nyoka akatumbua macho na asione alichokitumbulia.

Hii ilikuwa mpya kwake.

“ina maana ilishaanza Def Cond 0001 na sasa inavuka 0002?” aliuliza Mtega nyoka

“Lakini sio ile unayoijua wewe” alisema Mtega nyoka.

Hapo tena Mtega nyoka akakwama sauti kisha akamsikia Kinyonga akiendelea kuelezea…

“ Hii Def inaandaa Def cond 0008,na sio kama ni ya ndani; la hasha, hii ni ya kutokea nje ikihusisha watu wa ndani, hivyo basi kipimo changu kinasoma 0002 bado ni kimya kimya” alifafanua Mzee Kinyonga.


“ooh Sawa nimeelewa, kwa hiyo, kwa huo mkia umeonekana au kichwa ndo kimeonekana” aliuliza Mtega nyoka.

“aaah Mtega nyoka!!; kwani lini umeanza kuniuliza habari za kina nyoka mimi Kinyonga?” alilalama Mzee kinyonga.

Mtega nyoka, aliamua kukaa kimya mana alijua jukumu bado ni lake yeye kapewa tu fununu.

Na kikubwa aliwaza uzito wa kipimo alichodokezewa yani Def cond.
Def cond(defence control) ni kipimo cha migogoro ndani ya serikali huku kikianza na 1-8,sasa Mtega nyoka alikuwa ameambiwa hii Def cond sio anayoijua, hivyo basi katika uelewa wake alijua ya kuwa kuna mipango ya usaliti inafanyika kuiangusha serikali, mana def ilikadiriwa kuelekea def cond 0008 kumaanisha huko kunafukuta Vita kamili.
Lakini pia aliambiwa yakuwa kuna watu ndani na nje katika mipango hiyo na yeye ndo anapaswa kuwatafuta.

Akatabasamu hasa alipokumbuka vifo vya wahandisi, siku moja iliopita.

Fumbo!!

Hiyo ilimaanisha kuna fumbo lipo ndani ya kampuni ya Kasuku contractors lakini swali likabaki kwake.

Kwa nini Kasuku?

Na lilikuwa swali la msingi yeye kujiuliza kwa sababu Kasuku wanahusika na uchoraji na ujenzi wa majengo, lakini hata jengo lililojengwa nao lililomhusisha Mtega nyoka wao wajengaji hawakujua ni la nini lakini pia ramani ya jengo hawakuwa nayo yote.

Sasa ni vipi Kasuku wahusike na sakata gumu vile?

Mtego!!

Akajiwazia huku akipiga hatua kutoka ndani ya chumba alichokuwamo.

***

Safari yake ilimfikisha hadi soko dogo la machinjioni Mandu, kisha huko akaungana na wasafiri wengine kupanda daladala za kwenda kisasa kulikokuwa na mazishi ya mmoja wahandisi wa kampuni ya Kasuku.

Alichagua kwenda hapa, sababu wengine walisafirishwa mikoani kwao kwa ajili ya maziko.

Alifika mazishini na kushuhudia umati wa watu wengi sana ukiwa umejuimuika pamoja huku baadhi ya watu wakiwa wamejitenga huku na huko.

Msiba ulikuwa umepokea watu wa kila aina huku magari ya kifahari yakiwa yametapakaa kila sehemu hii ilimaanisha aliefariki alikuwa ni mtu wa watu lakini pia alikuwa ni mwenye kujiweza kifedha..

Roho ilimuuma mtega nyoka hasa aliposikia sauti za akina mama wakiomboleza.

“kwanini waluwawa watu hawa?” alijiuliza mtega nyoka bila kupata majibu.

“mtuhumiwa wa kwanza yupo kwetu au yupo ndani ya Kasuku” alizidi kuwaza mtega nyoka huku akipepesa macho huku na huko na hapo akaona vijana wa usalama kadhaa wakiwa katika majukumu yao ya kufuatilia kesi ile.

Akaachana nao na macho yake yakagota kwa kijana mmoja mtanashati akiwa amekaa na vijana wengine wawili wakijadili jambo huku mara kadhaa wakionekana kufurahia walichokuwa wanakijadili.

Lakini wakiwa katikati ya majadiliano mara akaja binti mmoja na kumuita yule kijana mtanashati alietizamwa na Mtega nyoka.

Yule kijana akaenda kumsikiliza yule binti, huku maongezi yao yakionekana kuwa ya utata upande mmoja kwani binti aliongea kwa kubabaika ama kuchanganywa na jambo huku kijana wa kiume akiwa makini kusikiliza.

Mtega nyoka akavuta hatua kujipitisha karibu yao, lakini kabla hajawafikia tayari walikuwa wamekwisha kuongozana kutoka eneo lile.

“una nini Malima!!” alijisemea Mtega nyoka huku akiangaza huku na huko ili aone kama kulikuwa kuna mtu mwingine aliekuwa anafuatilia nyendo za kijana yule.

Alimuona!!
shukrani mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom