Alloyce PR
JF-Expert Member
- Nov 15, 2020
- 798
- 865
Nikwambie ukweli pasipo na haki na usawa hakuna amani bali ni kuvumiliana na ujinga wa waliochache kutumia neno amani kama kinga ya kulinda maslahi yao, na kuwanyonya wengine kwa kula dili na kufanya mikataba mibovu ya kuuza rasilimali za taifa kwa kisingizio cha uwekezaji! HUU UPUMBAVU WENU wa kuwafanya watanzania waishi maisha magumu huku ccm ikigawa rasilimali za nchi kwa wageni sio uzalendo ni USALITI!TOLEO MAALUM – APRILI 2025
JE, KUNA DALILI ZA MAKUSUDI ZA KUHUJUMU UTHABITI WA TAIFA LETU?
Katika kipindi ambacho Tanzania inapiga hatua kubwa za kimkakati katika ujenzi wa miundombinu, uendelezaji wa sekta binafsi, na kuimarisha mapato ya ndani kupitia mageuzi ya kiuchumi na utawala bora, kumeibuka hali ya wasiwasi kuhusu uwepo wa baadhi ya watu wanaotaka kuvuruga uthabiti huu. Ni wazi kuwa mafanikio haya hayawafurahishi wote hasa wale ambao maslahi yao binafsi hayajafanikishwa kupitia njia halali na za kizalendo.
Lakini je, Serikali inaweza kuendelea kukaa kimya wakati baadhi ya watu wanashabikia propaganda, uchochezi na upotoshaji, kwa kisingizio cha uhuru wa kidemokrasia?
KWANINI WENGINE HUDHANI TANZANIA INAWEZA KUCHEZEWA?
Tanzania ni nchi iliyojijengea heshima kimataifa kupitia sera thabiti, diplomasia ya uchumi, na utulivu wa kisiasa. Hata hivyo, kuna dalili kuwa baadhi ya watu, wakiwemo wanasiasa na wanaharakati wachache, wanadhani wanaweza kuitumia nchi hii kama uwanja wa majaribio ya ajenda zao binafsi. Wanajificha nyuma ya neno "uhuru wa kujieleza" na kuibua hoja zenye harufu ya uasi, ilimradi tu wapate umaarufu au uungwaji mkono wa kisiasa.
Hili ni kosa la kimkakati. Tanzania si nchi ya majaribio ni taifa lenye misingi imara, linalosimamia nidhamu, sheria, na uzalendo.
MSTARI MWEMBAMBA KATI YA DEMOKRASIA NA HUJUMA NI UPI?
Katika mfumo wowote wa kidemokrasia, uhuru huambatana na wajibu. Lakini kwa baadhi ya watu, uhuru huo unaelekea kugeuzwa kuwa silaha ya kisiasa inayolenga kuvuruga amani na mshikamano wa kitaifa. Wanafanya hivyo kwa kueneza taarifa potofu, mashambulizi dhidi ya taasisi za dola, na kushambulia uongozi wa juu wa nchi kwa maneno ya kejeli na dharau, na kutumia viongozi wa dini kama silaha ya shinikizo.
UTEKELEZAJI UNATAKIWA LEO, SIO KESHO
Wananchi tunalojukumu la kuhakikisha utulivu wa taifa kabla hata ya vyombo vya ulinzi na usalama, waathirika wakubwa wa machafuko ni sisi wananchi. Ukiambiwa jambo kaa lichuje kabla hujachukua hatua ya kufanya uovu.
Taifa tuwe wenye kubishana kwa hoja sio kupata mihemko ya kuleta machafuko. Wote inabidi tulindwe na sheria sio kauli za watu fulani ambao wakishapata umaarufu wao hujiona wanaweza kufanya lolote na wakapata watetezi kwa haraka.
Kijana mtanzania ukweli mchungu ni kwamba, maisha yako yapo mikononi mwako, Serikali kazi yake kubwa ni kuweka mazingira wezeshi kukuwezesha kufikia malengo yako na kuijenga Tanzania imara. Sivyo, kama wale wanavyo wahubirieni kwenye majukwaa. Kama unaona kuna jambo haliko sawa jenga hoja sio kutukana, na kutisha watu, kufanya hivyo haitabadilisha hatima yako.
Wale wanaotumia mwanya wa kufahamika kimataifa kuleta uchochezi hatua madhubuti zichukuliwe kwa mujibu wa sheria. Wanaopaswa kuwajibika waonywe na, ikibidi, wachukuliwe hatua bila kuogopa kelele za watu wachache wanaotaka kuvuruga amani kwa kisingizio cha demokrasia.
TAIFA HILI LINA HISTORIA. LINA DIRA. LINA DHAMIRA.
Tanzania haiko sokoni. Sidhani kama wenye dhamana (viongozi na wananchi) watakubali kuchokozwa na maneno ya kejeli na misukumo ya watu wenye ajenda za kisiasa zisizo na maslahi kwa Watanzania.
"YA KUAMBIWA CHANGANYA NA YA KWAKO". LINDA AMANI POPOTE ULIPO.
Nikwambie ukweli pasipo na haki na usawa hakuna amani bali ni kuvumiliana na ujinga wa waliochache kutumia neno amani kama kinga ya kulinda maslahi yao, na kuwanyonya wengine kwa kula dili na kufanya mikataba mibovu ya kuuza rasilimali za taifa kwa kisingizio cha uwekezaji! HUU UPUMBAVU WENU wa kuwafanya watanzania waishi maisha magumu huku ccm ikigawa rasilimali za nchi kwa wageni sio uzalendo ni USALITI!
Tangu mwaka juzi ukiangalia viongozi wa ccm wameshindwa hata kuleta kampeni zinazohamasisha watu kujitafutia maendeleo yao ila wako bize na kampeni za kuhamasisha starehe na anasa kwenye nchi ambayo inachangamoto nyingi! Yaani raisi anapenda kuonekana kwenye events za wasanii kuliko uzinduzi wa miradi ya maendeleo! Wasaidizi wake nao wamebobea kwenye burudani utasikia, goli la mama, mara uzinduzi wa album ya harmonize mara kuwapeleka waigizaji korea mara landlover festival, yaani ni ujinga wa hali juu yanayofanywa na serikali! Tulikua na magufuli hizi habari za sherehe za kipumbavu pumbavu hazikuwa na nafasi nchi ikawa iko serious na ajenda za maendeleo. ACHENI UJINGA WATANZANIA WANATAKA MAENDELEO YANAYOWAPA NAFUU KATIKA MAISHA YAO. BILA USAWA NA HAKI ZA RAIA KUHESHIMIWA CCM ITAJUTA KUBANA DEMOKRASIA NCHINI.
Asante! Mtukufu Raphael AlloyceHaya Pumbavu.
Usihofu mkuu, nimetoa mawazo yangu tu na wewe umetoa mawazo yako ila nimerudishia hivyo kutokana na wewe kusema mimi mpumbavu. Sisi sote inabidi tujifunze kujenga hoja pasipo kutumia maneno ya kuudhi, kudhalilisha. Tujikite kwenye misingi ya hoja.Asante! Mtukufu Raphael Alloyce
Nakiri naweza kuwa mpumbavu ila nitapenda kujua ni mpumbavu katika eneo gani? Maana me nimekuita wewe mpumbavu kwa kushindwa kuelewa kuwa hakuna uzalendo kutetea mwenyekiti wa ccm kuwa mteuaji wa wasimamizi wa uchaguzi ilihali yeye pia ni mgombea katika uchaguzi huo! Ni muhimu mawazo ya wanaodai uwepo wa usawa na haki katika chaguzi zetu yaheshimiwe maana hata wao ni watanzania kama wana ccm walivo watanzania. AsanteUsihofu mkuu, nimetoa mawazo yangu tu na wewe umetoa mawazo yako ila nimerudishia hivyo kutokana na wewe kusema mimi mpumbavu. Sisi sote inabidi tujifunze kujenga hoja pasipo kutumia maneno ya kuudhi, kudhalilisha. Tujikite kwenye misingi ya hoja.
NISAMEHE KWA KUTUMIA NENO UPUMBAVU KWENYE MAJIBU YANGU.
Sasa upumbavu uko hapo, nilichoandika na unacho tafsiri ni tofauti, walau ungeniuliza namaanisha nini kabla hujatumia neno mpumbavu.Nakiri naweza kuwa mpumbavu ila nitapenda kujua ni mpumbavu katika eneo gani? Maana me nimekuita wewe mpumbavu kwa kushindwa kuelewa kuwa hakuna uzalendo kutetea mwenyekiti wa ccm kuwa mteuaji wa wasimamizi wa uchaguzi ilihali yeye pia ni mgombea katika uchaguzi huo! Ni muhimu mawazo ya wanaodai uwepo wa usawa na haki katika chaguzi zetu yaheshimiwe maana hata wao ni watanzania kama wana ccm walivo watanzania. Asante
Umeongea vema, kiukweli uku mitaani kila mtu kaishachoka ni vile hawana pa kusemea ila ukiongea na watu na wana uhakika wako salama na maongezi yao wanatoa ya moyoni sana na wakati huo wamevaa na zile picha za kupigia mwingiNikwambie ukweli pasipo na haki na usawa hakuna amani bali ni kuvumiliana na ujinga wa waliochache kutumia neno amani kama kinga ya kulinda maslahi yao, na kuwanyonya wengine kwa kula dili na kufanya mikataba mibovu ya kuuza rasilimali za taifa kwa kisingizio cha uwekezaji! HUU UPUMBAVU WENU wa kuwafanya watanzania waishi maisha magumu huku ccm ikigawa rasilimali za nchi kwa wageni sio uzalendo ni USALITI!
Tangu mwaka juzi ukiangalia viongozi wa ccm wameshindwa hata kuleta kampeni zinazohamasisha watu kujitafutia maendeleo yao ila wako bize na kampeni za kuhamasisha starehe na anasa kwenye nchi ambayo inachangamoto nyingi! Yaani raisi anapenda kuonekana kwenye events za wasanii kuliko uzinduzi wa miradi ya maendeleo! Wasaidizi wake nao wamebobea kwenye burudani utasikia, goli la mama, mara uzinduzi wa album ya harmonize mara kuwapeleka waigizaji korea mara landlover festival, yaani ni ujinga wa hali juu yanayofanywa na serikali! Tulikua na magufuli hizi habari za sherehe za kipumbavu pumbavu hazikuwa na nafasi nchi ikawa iko serious na ajenda za maendeleo. ACHENI UJINGA WATANZANIA WANATAKA MAENDELEO YANAYOWAPA NAFUU KATIKA MAISHA YAO. BILA USAWA NA HAKI ZA RAIA KUHESHIMIWA CCM ITAJUTA KUBANA DEMOKRASIA NCHINI.