Kambi ya Lowassa inaanza kubabaika na kuhangaika na Januari Makamba. Wote tunajua kwamba kwenye vikao vyao huyu pekee ndiye wanayemtaja kwamba ni tishio na sasa wameanza kuja na hii ya kitoto ya kumhusisha na ulaji wa IPTL. Hii nayo itabuma. Tatizo la watu wa Lowasa hawafikirii kwa kina. Katika wote waliotajwa, Ngeleja alikuwa na nafasi ya kuisaidia IPTL kama Waziri wa Nishati, Pinda ana nafasi ya kuisaida IPTL kama PM, Membe naye sina hakika. Sasa Januari anawasaidia vipi IPTL hadi wampe pesa? Halafu nyie watu wa Lowasa si kila siku mnasema huyu bwana mdogo hana nafasi ya ushindi, sasa kama hana nafasi pesa anapewa za nini?
Nimesikia tetesi kutoka ndani ya familia ya Makamba kuhusu uchafuzi huu wa kambi ya Lowasa sasa nao nasikia wanakuja na vitu vizito.
Anna Tibaijuka ana nafasi gan ya kuisaidia IPTL?