Hassani
JF-Expert Member
- Jun 5, 2009
- 710
- 1,147
Nimepita kwenye account za Januari Makamba,Matusi na kejeli za wananchi wenye hasira za mgao wa umeme zimekua nyingi.Na nyingi zikijielekeza na kukumbushia miaka 5 ya Magufuli kuwa umeme haukukatika na hata kama ulikatika sio kwa kiasi hiki.
Mimi sio mtaalam wa umeme ila ntatoa hoja yangu kisiasa zaidi, inajulikana wazi Makamba ni mwanasiasa kijana ambaye yuko very ambitious, sihitaji kukumbushia nafasi yake katika mbio za urais za 2015,na wengi tunaamini mbio zake za urais hazijakoma ingawa kwa miaka 5 iliyopita mambo hayakuwa marais kwake.
Amekuja mama Samia na kumrudisha uwanjani baada ya kukaa benchi mda mrefu.hii ni fursa hadhim kwake kufufua ndoto na matarajio yake. Kwa kawaida mchezaji anayetoka benchi anakuwa na nguvu mpya bila kuacha makeke mengi.
Sio rahisi mchezaji anayetoka benchi na kuona makosa mengi ya wachezaji wenzake aanze kwa kujifunga goli la makusudi kabisa ukichukulia mtu kama Makamba ni mwanasiasa aliyetoka kwenye familia ya wanasiasa wakongwe.
Naamini kabisa kinachoendelea kuhusu umeme ni kama jumba bovu lililomwangukia Makamba mara tu baada ya kuingia kama mpangaji mpya.
Nikirejea kauli yake ya kuwapa TANESCO wiki mbili na ile ya mitambo kutofanyiwa matengenezo kwa uoga wa watu,naamini kabisa kuna sababu iko nje ya uwezo wake inayosababisha umeme kukatika.
Nawasilisha
Mimi sio mtaalam wa umeme ila ntatoa hoja yangu kisiasa zaidi, inajulikana wazi Makamba ni mwanasiasa kijana ambaye yuko very ambitious, sihitaji kukumbushia nafasi yake katika mbio za urais za 2015,na wengi tunaamini mbio zake za urais hazijakoma ingawa kwa miaka 5 iliyopita mambo hayakuwa marais kwake.
Amekuja mama Samia na kumrudisha uwanjani baada ya kukaa benchi mda mrefu.hii ni fursa hadhim kwake kufufua ndoto na matarajio yake. Kwa kawaida mchezaji anayetoka benchi anakuwa na nguvu mpya bila kuacha makeke mengi.
Sio rahisi mchezaji anayetoka benchi na kuona makosa mengi ya wachezaji wenzake aanze kwa kujifunga goli la makusudi kabisa ukichukulia mtu kama Makamba ni mwanasiasa aliyetoka kwenye familia ya wanasiasa wakongwe.
Naamini kabisa kinachoendelea kuhusu umeme ni kama jumba bovu lililomwangukia Makamba mara tu baada ya kuingia kama mpangaji mpya.
Nikirejea kauli yake ya kuwapa TANESCO wiki mbili na ile ya mitambo kutofanyiwa matengenezo kwa uoga wa watu,naamini kabisa kuna sababu iko nje ya uwezo wake inayosababisha umeme kukatika.
Nawasilisha