Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 141,449
- 283,758
yote yanaenda pamoja mjomba , hakuna lililosahaulika .Tumeshasahau kabisa kuhusu Uchaguzi wa Wazanzibar, Na ule uhuni wa Ras pamoja Na wanasheria wake kuhusu meya wa jiji, kweli sie wadanganyika
Umenena vema eh mwana wa Adam!WARAKA KWA RAIS MAGUFULI
Rais Magufuli usikubali watu wakutumie kumalizana
Na Paul Mwandemele
Rais wangu mpendwa, nakuandikia kwa heshima kubwa. Nakupongeza kwa kazi nzuri unayoifanyia nchi yetu, hasa safishasafisha ya viongozi wabovu. Kazi hii imepokelewa vizuri na wananchi.
Hata hivyo watu wengi tunaoishi huku mitaani na kufuatilia mwendeno wa Serikali yako tumebaini mwelekeo mmoja ambao napenda nikujulishe ili hili suala lisije kukuharibia na kuharibu kazi nzuri inayofanywa.
Majuzi nilikuwa kwenye mgawaha mmoja unaitwa Cruz-In Mikocheni. Wadau tuliokuwa nao walikuwa na mjadala mzito kuhusu Serikali yako. Upande mmoja wanasema Serikali yako inafukuza watu kwa ajili tu ya sifa kwa umma na kwamba kuna watu wengi wanaonewa. Wanasema kwamba ukitaka mtu afukuzwe na Rais wewe mchafue tu kwenye vyombo vya habari, tengeneza mazingira kama hatakiwi na jamii na utaona kama Rais hatamfukuza. Kwa upande mwingine, ambao nami nimo, tulikuwa tunapinga na tunasema Rais ni mtu wa haki, anafuata sheria na ukiona mtu katimuliwa ujue uchunguzi umefanyika na uchunguzi sio lazima utangazwe na kwamba mtu huyo kapewa haki ya kuelezea upande wake. Sisi tukasema Rais ni mtu wa haki. Lakini tulibishiwa sana.
Rais wangu jamii yetu imeharibika. Watu wanafurahia wengine wakidhalilika. Watu wanapenda kuona damu. Watu wanapenda visasi. Watu wanachukiana. Wengine wanafurahia safishasafisha sio kwasababu inasaidia nchi, bali kwasababu kuna watu wanaumbuka. Kwenye vyombo vya habari na mitandaoni kuna watu sasa wanatengeneza orodha ya nani anayefuatia kwenye kuumbuliwa. Dhana ya utumbuaji majipu wanaipotosha. Visasi vyao wanataka vikamilishwe na Serikali yako. Naomba usikubali kabisa. Moja ya sifa ya kiongozi ni kutenda haki. Rais ameshika upanga mkuu na upanga huo una makali na anaweza kuutumia atakavyo. Rais wangu usikubali watu wakushinikize kuzungusha upanga kwasababu tu ya raha ya kuona kichwa kinadondoka.
Mifano ya mashinikizo haya ipo mingi. Lakini mfano wa karibuni ni wa Waziri wako, January Makamba. Lipo kundi limejiapiza kwamba lazima aanguke na tunapowasoma mitandaoni wanasema wazi kabisa namna ya kumuangusha kijana wako huyu ni kumtengenezea uchafu wa kutunga ili Magufuli aone raha kuzungusha upanga. Pamoja na kujua kabisa kwa uhakika kwamba wanayozungusha ni ya kutunga, wanajihakikishia kwamba Magufuli anaamka na upanga na akisikia tu mabaya haulizi, anakata. Lakini mimi najua huyu siye Magufuli niliyempa kura yangu. Magufuli niliyempa kura yangu ni mtu wa haki.
Tuendelee na safishasafisha Rais wangu. Ila ni muhimu watu wanaopenda kufitiniana wajue Rais wangu ni mtu wa haki. Sio ukimsema tu kiongozi kwenye Serikali yake basi upanga unampitia. Wakijua hivyo Rais hayumbi, fitina zitapungua kwenye Serikali na kwenye siasa. Umechagua timu imara kwenye Serikali yako. Nimefurahi kwamba pamoja na mashinikizo na fitina kuhusu Prof Muhongo na Prof Maghembe bado umewapa nafasi wakusaidie. Umetengeneza sifa nzuri kwamba maneno ya magazeti na mitandaoni hayasukumi uamuzi wako. Kuna ambao hawapendi kwamba baadhi ya watu wamo kwenye Serikali yako. Simama imara na timu yako, anayeharibu atolewe, anayesakamwa kwa fitina simama naye, utaijengea timu yako kujiamini katika kazi zao na watakufanyia kazi nzuri. Tusikubali kurudi kule kwenye miaka 10 iliyopita ambapo nchi ilipitia Mawaziri 121 kwasababu fitina ziliruhusiwa, na Mawaziri wakawa wanapukutishwa kila miezi sita. Unayo nafasi kubwa ya kuisaidia nchi kumaliza fitina kwenye siasa nchini kwa kuonyesha kwamba huchukui hatua kwa kufuata upepo, ambao zama hizi unatengenezwa mezani.
Nisamehe kama nimekukwaza kwa kutoa ushauri lakini mimi nimekupa kura yangu na ni mdau mkubwa wa kutaka Serikali yako ifanikiwe.
Ningekuwa mimi ili nikubali kumtetea ningeomba ka-Vitz na hiyo nanilii uliyoiandika hapo ya dada ake kwa angalau mwezi...Usiku wa jana watu wamelipwa wakakesha kuandaa nyaraka za kumtetea yule dogo anayeuza rasimali sambamaba na papuchi ya dafaye.
Hivi kumbe JPM anafanya maamuzi kutegemea maoni ya mitandao ya jamii? Basi UWT hawana kazi.WARAKA KWA RAIS MAGUFULI
Rais Magufuli usikubali watu wakutumie kumalizana
Na Paul Mwandemele
Rais wangu mpendwa, nakuandikia kwa heshima kubwa. Nakupongeza kwa kazi nzuri unayoifanyia nchi yetu, hasa safishasafisha ya viongozi wabovu. Kazi hii imepokelewa vizuri na wananchi.
Hata hivyo watu wengi tunaoishi huku mitaani na kufuatilia mwendeno wa Serikali yako tumebaini mwelekeo mmoja ambao napenda nikujulishe ili hili suala lisije kukuharibia na kuharibu kazi nzuri inayofanywa.
Majuzi nilikuwa kwenye mgawaha mmoja unaitwa Cruz-In Mikocheni. Wadau tuliokuwa nao walikuwa na mjadala mzito kuhusu Serikali yako. Upande mmoja wanasema Serikali yako inafukuza watu kwa ajili tu ya sifa kwa umma na kwamba kuna watu wengi wanaonewa. Wanasema kwamba ukitaka mtu afukuzwe na Rais wewe mchafue tu kwenye vyombo vya habari, tengeneza mazingira kama hatakiwi na jamii na utaona kama Rais hatamfukuza. Kwa upande mwingine, ambao nami nimo, tulikuwa tunapinga na tunasema Rais ni mtu wa haki, anafuata sheria na ukiona mtu katimuliwa ujue uchunguzi umefanyika na uchunguzi sio lazima utangazwe na kwamba mtu huyo kapewa haki ya kuelezea upande wake. Sisi tukasema Rais ni mtu wa haki. Lakini tulibishiwa sana.
Rais wangu jamii yetu imeharibika. Watu wanafurahia wengine wakidhalilika. Watu wanapenda kuona damu. Watu wanapenda visasi. Watu wanachukiana. Wengine wanafurahia safishasafisha sio kwasababu inasaidia nchi, bali kwasababu kuna watu wanaumbuka. Kwenye vyombo vya habari na mitandaoni kuna watu sasa wanatengeneza orodha ya nani anayefuatia kwenye kuumbuliwa. Dhana ya utumbuaji majipu wanaipotosha. Visasi vyao wanataka vikamilishwe na Serikali yako. Naomba usikubali kabisa. Moja ya sifa ya kiongozi ni kutenda haki. Rais ameshika upanga mkuu na upanga huo una makali na anaweza kuutumia atakavyo. Rais wangu usikubali watu wakushinikize kuzungusha upanga kwasababu tu ya raha ya kuona kichwa kinadondoka.
Mifano ya mashinikizo haya ipo mingi. Lakini mfano wa karibuni ni wa Waziri wako, January Makamba. Lipo kundi limejiapiza kwamba lazima aanguke na tunapowasoma mitandaoni wanasema wazi kabisa namna ya kumuangusha kijana wako huyu ni kumtengenezea uchafu wa kutunga ili Magufuli aone raha kuzungusha upanga. Pamoja na kujua kabisa kwa uhakika kwamba wanayozungusha ni ya kutunga, wanajihakikishia kwamba Magufuli anaamka na upanga na akisikia tu mabaya haulizi, anakata. Lakini mimi najua huyu siye Magufuli niliyempa kura yangu. Magufuli niliyempa kura yangu ni mtu wa haki.
Tuendelee na safishasafisha Rais wangu. Ila ni muhimu watu wanaopenda kufitiniana wajue Rais wangu ni mtu wa haki. Sio ukimsema tu kiongozi kwenye Serikali yake basi upanga unampitia. Wakijua hivyo Rais hayumbi, fitina zitapungua kwenye Serikali na kwenye siasa. Umechagua timu imara kwenye Serikali yako. Nimefurahi kwamba pamoja na mashinikizo na fitina kuhusu Prof Muhongo na Prof Maghembe bado umewapa nafasi wakusaidie. Umetengeneza sifa nzuri kwamba maneno ya magazeti na mitandaoni hayasukumi uamuzi wako. Kuna ambao hawapendi kwamba baadhi ya watu wamo kwenye Serikali yako. Simama imara na timu yako, anayeharibu atolewe, anayesakamwa kwa fitina simama naye, utaijengea timu yako kujiamini katika kazi zao na watakufanyia kazi nzuri. Tusikubali kurudi kule kwenye miaka 10 iliyopita ambapo nchi ilipitia Mawaziri 121 kwasababu fitina ziliruhusiwa, na Mawaziri wakawa wanapukutishwa kila miezi sita. Unayo nafasi kubwa ya kuisaidia nchi kumaliza fitina kwenye siasa nchini kwa kuonyesha kwamba huchukui hatua kwa kufuata upepo, ambao zama hizi unatengenezwa mezani.
Nisamehe kama nimekukwaza kwa kutoa ushauri lakini mimi nimekupa kura yangu na ni mdau mkubwa wa kutaka Serikali yako ifanikiwe.
Erythrocyte ule Uzi siuuoni nini kimetokeayote yanaenda pamoja mjomba , hakuna lililosahaulika .
Wewe nae! Pesa za mchongo uende mahakamani. Msijitie hamuelewiHuyu Muitaliano kana anamdai JM kwa nini asiende Mahakamani?
sina taarifa kamili mkuu , ngoja tuwaulize viongozi wa jf .Erythrocyte ule Uzi siuuoni nini kimetokea
nani kakuambia Magumashi yana ushahidi ?Huyu Muitaliano kana anamdai JM kwa nini asiende Mahakamani?
acha ujinga wapi january kasema amepokea fedha kutoka kwa mzungu usiongee vitu usivyojua utafungwa tuUmohojoka kweli kweli kwa sababu ya kumtetea Makamba na Uchafu wa dada yake, Mzungu mwenyewe ashapewa chake, makamba kakiri kumjua, kakiri kupokea hela kupitia dada yake aliyepewa na mzungu, mzungu mwenyewe inadaiwa makamba anamjua kuwa anabwia unga, alimwona wapi anabwia? au Dubai, hata hivyo Mange ni kama unamuandaa kutoa ushahidi wa kiti hiki maana ana kila aina ya ushahidi, amejitolea kutoa ushirikiano na takukuru, haya sasa takukuru waanze kazi kama makamba hatanyea kambi? bora unyamaze tu watu wanajua mengi juu ya utapeli wa mwanadada huyu na kaka mtu. Haya sasa watetezi mshakuwa wengi mtuharibie serikali yetu tukufu, serikali ile ya kishikaji, ya kubebana ishaoondoka, wewe umeungana na Yule wa ACT kutetea ujinga, acha ujinga bwana acha watu wamwage ukweli.
kwahiyo hiyo blog ndio umeiamini sana sindio ufinyu wa mawazo huo
Daaah!! Hii familia ni noma mazee.Usiku wa jana watu wamelipwa wakakesha kuandaa nyaraka za kumtetea yule dogo anayeuza rasimali sambamaba na papuchi ya dafaye.