Kuna habari kuwa aliyekuwa kocha msaidizi wa timu kongwe ya soka Tanzania Simba Sports Club, Jamhuri Kiwelo (Julio Alberto) ametimuliwa. Kwa mujibu wa taarifa zilizorushwa hewani na kipindi cha michezo cha kituo cha radio cha TBC Taifa, baadhi ya wanachama wa Simba wanamshutumu Julio kwa kuyumbisha benchi la ufundi la Simba hali iliyopelekea timu hiyo kongwe kufanya vibaya katika mechi zake kadhaa za ligi ya Vodacom inayoendelea. Akihojiwa na mtangazaji wa TBC Taifa Philip Cyprian, Julio alisema yeye hababaishwi na maamuzi ya kutimuliwa kwake kwani siku zote Simba inapofanya vibaya basi lazima atafutwe mchawi na safari hii hali hiyo imemuangukia yeye..... Hii ndio soka yetu wadau