ng'adi lawi
JF-Expert Member
- Sep 27, 2014
- 2,956
- 1,115
Wakuu kuna tetesi kuwa James ole Milya anataka kugombea ubunge Arusha mjini mwaka ujao. Mimi naona anafaa zaidi ya mbunge wetu wa sasa Godbless Lema. Godbless Lema amefanya kazi kubwa kuimarisha chama chetu CHADEMA na amewaimarisha vijana na kuwafanya jasiri wa kujua na kudai haki zao. Ni vema sasa akapandishwa cheo na apewe nafasi iliyoachwa na John Mnyika ya Ukatibu Mwenezi na uhamasishaji ili apewe wigo mpana wa kuongeza wanachama na wapenzi nchi nzima. Kwa wasiomfahamu James ole Milya yeye ni mwanasheria, ni kijana wa Kimasai na anaweza kutuletea mawazo mapya ya maendeleo katika jiji letu hasa pale halmashauri ambapo mikataba ya hovyo na ya kifisadi inatengenezwa na hatuoni maendeleo.
Wakuu mwaonaje ?
Wakuu mwaonaje ?