James Mbatia: Tulianzisha chama cha NCCR Mageuzi tukiwa wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam

GUSSIE

JF-Expert Member
Dec 2, 2014
3,866
11,100
James Mbatia: Haikuwa kazi rahisi tulipoamua kuanza kuandaa makongamano ya mabadiliko ya katiba tukiwa wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam mwishoni mwa miaka ya 1988 kuelekea 1989 na tuliita hayao mabadiliko kama National Construction and Constitutional Reform Tanganyika and Zanzibar.

James Mbatia: Tulikuwa watu 18 tulioanzisha hayo Mageuzi kabla hata serikali haijaunda Tume zake kuuliza watanzania wanataka mfumo gani chama kimoja au vyama vingi.

James Mbatia:
Mabadiliko hayo yalisimamiwa na watu wawili kama viongozi wetu tuliowachagua Chief Fundikira na Mabere Nyaucho Nyarandu.

James Mbatia: Hali hii ikapelekea mimi James Mbatia kufukuzwa Chuo kikuu cha Dar es Salaam mwaka wa mwisho wa masomo yangu.

James Mbatia: Tulianzisha vuguvugu la vyama vingi tukiamini nguvu ya vijana Vyuoni na mabadiliko ya siasa za vita baridi tungeweza kulazimisha serikali ikubali mfumo wa vyama vingi kutokana na msuguano uliokuwa unaendelea duniani juu ya ubepari na ujamaa.

James Mbatia: Enzi hizo chuo kikuu cha Dar es Salaam kilikuwa ni sehemu ya mawazo mbadala ambayo tulikaa Nkurumah Hall kuyajadili wanafunzi na walimu kama Prof Issa Shivji, Tenga na akina Dokta Sengondo Mvungi

Tuliamua kuanza kufanya choko choko hizo kabla hata serikali Haijafikia au kuwaza kuwa na mfumo wa vyama vingi

James Mbatia: Katika uasisi wa Mageuzi ya NCCR ( National construction and Constitutional reform) wakati huo nilipewa kadi namba 6.

James Mbatia: Baada ya Serikali kuunda Tume ya Francis Nyalali na kuridhia mfumo wa vyama vingi Tanzania miaka ya 1991, Sisi Tuliamua Kuongeza neno Mageuzi kwenye NCCR hivyo tukakisajili kama chama kamili mwaka 1992.

James Mbatia: Agustino Mrema tulimkaribisha NCCR -mageuzi mwaka 1995 mwezi march.

Hata baada ya kufukwa chuo nilienda kugombea ubunge kwenye uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi na nikashinda nikawa mbunge wa kwanza kijana mdogo Bungeni mwaka 1995

James Mbatia: Mwaka 1992 nilifukuzwa chuo moja kwa moja na wanafunzi Wengine tisa hivyo sikumaliza shahada yangu ya Civil Engineering na nilibakiza miezi miwili tu tulionekana watukutu na vinara wa mabadiliko chuo kikuu cha Dar es Salaam kwa kusababisha chuo kufungwa mwaka mzima
 
Kulingana na historia yake alianza vizuri akiwa na nia ya kuleta mabadiliko ya kweli, tatizo lake huku mbele ya safari amekuwa mtu asiyeeleweka, akiamka vizuri moto, akiamka vibaya baridi, siku nyingine vuguvugu.
 
Kulingana na historia yake alianza vizuri akiwa na nia ya kuleta mabadiliko ya kweli, tatizo lake huku mbele ya safari amekuwa mtu asiyeeleweka, akiamka vizuri moto, akiamka vibaya baridi, siku nyingine vuguvugu.
Mkuu hao Jamaa akina Mbatia waliamua kujilipua sana chuoni

Kumbuka hizo ni kesi za uhaini, Vijana wa sasa wanajua kula burger na Pizza huku wakiwaomba wabunge wawatetee bungeni

Akina Mbatia na wenzake walijilipua sio kidogo kwa kuamua kujitetea wenyewe kulazimisha mfumo ndani ya mfumo wa serikali na chama
 
Mkuu hao Jamaa akina Mbatia waliamua kujilipua sana chuoni

Kumbuka hizo ni kesi za uhaini, Vijana wa sasa wanajua kula burger na Pizza huku wakiwaomba wabunge wawatetee bungeni

Akina Mbatia na wenzake walijilipua sio kidogo kwa kuamua kujitetea wenyewe kulazimisha mfumo ndani ya mfumo wa serikali na chama
Ingependeza kama angeendelea na huo msimamo wake mpaka leo naamini angekuwa na support kubwa ya watu na chama chake kingekuwa na heshima.
 
James Mbatia: Enzi hizo chuo kikuu cha Dar es Salaam kilikuwa ni sehemu ya mawazo mbadala ambayo tulikaa Nkurumah Hall kuyajadili wanafunzi na walimu kama Prof Issa Shivji, Tenga na akina Dokta Sengondo Mvungi
hili nakubaliana na wewe kwa asilimia mia moja.
 
James Mbatia: Haikuwa kazi rahisi tulipoamua kuanza kuandaa makongamano ya mabadiliko ya katiba tukiwa wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam mwishoni mwa miaka ya 1988 kuelekea 1989 na tuliita hayao mabadiliko kama National Construction and Constitutional Reform Tanganyika and Zanzibar.

James Mbatia: Tulikuwa watu 18 tulioanzisha hayo Mageuzi kabla hata serikali haijaunda Tume zake kuuliza watanzania wanataka mfumo gani chama kimoja au vyama vingi.

James Mbatia:
Mabadiliko hayo yalisimamiwa na watu wawili kama viongozi wetu tuliowachagua Chief Fundikira na Mabere Nyaucho Nyarandu.

James Mbatia: Hali hii ikapelekea mimi James Mbatia kufukuzwa Chuo kikuu cha Dar es Salaam mwaka wa mwisho wa masomo yangu.

James Mbatia: Tulianzisha vuguvugu la vyama vingi tukiamini nguvu ya vijana Vyuoni na mabadiliko ya siasa za vita baridi tungeweza kulazimisha serikali ikubali mfumo wa vyama vingi kutokana na msuguano uliokuwa unaendelea duniani juu ya ubepari na ujamaa.

James Mbatia: Enzi hizo chuo kikuu cha Dar es Salaam kilikuwa ni sehemu ya mawazo mbadala ambayo tulikaa Nkurumah Hall kuyajadili wanafunzi na walimu kama Prof Issa Shivji, Tenga na akina Dokta Sengondo Mvungi

Tuliamua kuanza kufanya choko choko hizo kabla hata serikali Haijafikia au kuwaza kuwa na mfumo wa vyama vingi

James Mbatia: Katika uasisi wa Mageuzi ya NCCR ( National construction and Constitutional reform) wakati huo nilipewa kadi namba 6.

James Mbatia: Baada ya Serikali kuunda Tume ya Francis Nyalali na kuridhia mfumo wa vyama vingi Tanzania miaka ya 1991, Sisi Tuliamua Kuongeza neno Mageuzi kwenye NCCR hivyo tukakisajili kama chama kamili mwaka 1992.

James Mbatia: Agustino Mrema tulimkaribisha NCCR -mageuzi mwaka 1995 mwezi march.

Hata baada ya kufukwa chuo nilienda kugombea ubunge kwenye uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi na nikashinda nikawa mbunge wa kwanza kijana mdogo Bungeni mwaka 1995

James Mbatia: Mwaka 1992 nilifukuzwa chuo moja kwa moja na wanafunzi Wengine tisa hivyo sikumaliza shahada yangu ya Civil Engineering na nilibakiza miezi miwili tu tulionekana watukutu na vinara wa mabadiliko chuo kikuu cha Dar es Salaam kwa kusababisha chuo kufungwa mwaka mzima

Kitefu cha NCCR tafadhali
 
Back
Top Bottom