James Mbatia: Ni aibu kubwa sana kusitisha uokoaji kisa giza karne hii

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
mbatia.jpg

Mbunge wa Vunjo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi, Jamse Mbatia, ametoa pole kwa familia zilizopoteza ndugu zao kwenye ajali ya kuzama kwa kivuko cha Mv. Nyerere, kilichozama siku ya jana ambayo hadi sasa inaripotiwa kuwa zaidi ya watu 50, wamepoteza maisha.

Ajali iliyotokea jana, ile tunaweza kusema ni ajali ya kujitakia, na waliohusika wameua kwa kukusudia, kwa sababu hii dhana ya kutothamini uhai wa mwanadamu hapa nchini imezidi kukithiri - Jamse Mbatia Mbunge wa Vunjo ( NCCR Mageuzi).

Zaidi ya 96% ya majanga yanasababishwa na wanadamu na 4% ni nguvu asilia - Mbunge wa Vunjo, Jamse Mbatia.

Mbunge wa Ukerewe alilitahadharisha hili ndani ya Bunge, na alitoa mapendekezo lakini bado kivuko hakitoshelezi japo kilinunuliwa injini mpya, sasa nani alijali - Jamse Mbatia.

"Mbunge wa Vunjo James Mbatia ameitaja ajali ya jana ya MV. Nyerere kuwa ni janga la kujitakia, amesema kwa mujibu wa elimu aliyoipata ya namna ya kukabiliana na majanga kuwa hilo ni janga la kujitakia na waliohusika wameua kwa kukusudia" 1/2.

Katika ufafanuzi wake James Mbatia amebainisha kuwa asilimia 96 ya majanga yanayotokea yanasababishwa na binadamu na ni asilimia 4% huwa ni yale yanayosababishwa na nguvu asilia. 2/2.

"Ukirejea ajali ya MV. Bukoba miaka 20 liyopita ile Ilikuwa ni elimu tosha kwetu sisi ya kutufanya ajali hii isitokee." James Mbatia - Mbunge wa Vunjo

"Mbunge wa Ukerewe, Serikali ilimpa majibu na haikumpa majawabu sahihi na endapo ingempa majawabu sahihi hili lililotokea leo lisingetokea" - James Mbatia.

Hasara inayotokana na kuzama, kwa Mv. Nyerere huwezi kufananisha na kitu chochote, hata uuze Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, huwezi kurudisha uhai wa watu - Jamse Mbatia, Mbunge wa Vunjo.

Cha kushangaza, eti wanasitisha zoezi la uokoaji kwa sababu ya giza, karne hii, haingii akilini, hapa tulipofikia mungu atusamehe - Jamse Mbatia.

NUKUU: Kujibu kabla ya kutafakari ni upumbavu na aibu kwako - Jamse Mbatia.

Habari zaidi, soma=>Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 125 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa! - JamiiForums
 
Mtoa post rekebisha hapo jina ni James Mbatia na sio Jamse...............


Hakuna kilichoniliza kama yule mbunge anaesema sio kuja bungeni nakuanza kuomba rambi rambi kweli alisema na yametokea Mungu tuokoe wenyewe hatutakaa tuweze
 
IMG_8695.JPG


Mbunge wa Vunjo na Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia ameinyooshea kidole Serikali kwa uzembe wa kushindwa kufanyia ukarabati kivuko cha MV Nyerere hadi kupelekea Mbunge wa Ukerewe, Joseph Mkundi kutahadharisha bungeni kuwa, kuna janga litakuja kutokea kwenye kivuko hicho cha MV Nyerere.

IMG_8693.jpg

Yaliyotabiriwa na mbunge kuzama Mv Nyerere yatimia

Hata hivyo, ukweli ni kwamba, Mbunge huyo alikuwa akiiomba Serikali mwaka Jana 2017 kukikarabati kivuko hicho kutokana na kuchakaa kwa mashine zake na kushindwa kutoa huduma kwa muda mrefu.



Hivyo kwa muda mrefu wa mwaka 2018, Seriikali ilikuwa ikikarabati Kivuko hicho ambacho kilifunguliwa Mwezi Julai 2018 baada ya kufungwa injini mbili mpya kwa gharama ya Tsh. milioni 191.
IMG_8694.jpg



Kwa hali hiyo, Kivuko hicho kimepata ajali si kwa sababu ya ubovu bali sababu nyingine tu japokuwa wengi wanadai Kivuko kilijaza watu wengi na mizigo mingi.
Ni vyema Viongozi waache kauli za uchochezi na badala yake waseme ukweli ili kuepuka chuki za wananchi dhidi ya Serikali yao bila sababu.
 
Eti giza limekuwa kikwazo cha uokozi hii nchi imeishiwa mipango,mwisho wa picha tutawaona wazee wa kimila wakienda kutambika yaani badala ya kuwapelekea meli ya kisasa
 
Hahahaha
Lijamaa limeibuka nalo!
Mijitu isiyo na agenda wana matatizo sana walahi
 
Wewe acha kutetea vitu vya ajabu
Yule mbunge alitaadharisha ajali mpaka akasema mambo ya rambi rambi
 
Back
Top Bottom