Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Aliyekuwa Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia, ameibua mjadala mzito kuhusu historia ya mageuzi ya kisiasa nchini Tanzania, akisisitiza kuwa chama hicho ndicho kilichokuwa chimbuko la mfumo wa vyama vingi.
Akizungumza na mtangazaji Wilberforce Ngoto katika kipindi cha Maswali na Majibu kinachorushwa na Jambo TV, Mbatia amesema NCCR Mageuzi ndicho chama kilichoasisi mabadiliko hayo makubwa kati ya mwaka 1990 na 1991.
“NCCR Mageuzi ya mwaka 1995 ilikuwa NCCR Mageuzi kwelikweli, na ilitikisa nchi hii kweli kweli… Wabunge wengi wa kwanza waliopata nafasi kupitia mfumo wa vyama vingi walitoka NCCR Mageuzi,” amesema Mbatia.
Akizungumza na mtangazaji Wilberforce Ngoto katika kipindi cha Maswali na Majibu kinachorushwa na Jambo TV, Mbatia amesema NCCR Mageuzi ndicho chama kilichoasisi mabadiliko hayo makubwa kati ya mwaka 1990 na 1991.
“NCCR Mageuzi ya mwaka 1995 ilikuwa NCCR Mageuzi kwelikweli, na ilitikisa nchi hii kweli kweli… Wabunge wengi wa kwanza waliopata nafasi kupitia mfumo wa vyama vingi walitoka NCCR Mageuzi,” amesema Mbatia.