DELETED ACCOUNT
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 9,805
- 15,470
Pamoja na mauzauza yooote yaliyotokea katika fainali hii ya CAFCC, kuna jambo moja ambalo kidogo limenifurahisha.
Kitendo cha Joshua Mutale kushinda tuzo ya mchezaji bora wa fainali ni mwisho mzuri wa story ya Simba katika mashindano haya.
Mutale alianza msimu vibaya na mimi ni mmoja wa watu tuliomkatia tamaa. Miezi miwili hivi ya hapa mwishoni katika mashindano ya CRDB Cup akaanza kuonyesha dalili za kuwa bora na jana akashinda tuzo ya mchezaji bora wa fainali mbele ya wachezaji tulioambiwa wana thamani ya mabilioni ya pesa na wanaogombaniwa huko Ulaya.
Ukiacha goli alilofunga, Mutale jana angeondoka pia na assist kama siyo famba aliyofanya Kapombe na angeweza kuipa Simba ubingwa wa CAF.
Ni mwisho bora sana wa story hii ya Simba katika fainali hizi.
NB. Pia ni uthibitisho kuwa ni timu ya Simba SC pekee iliyowahi kuleta fainali ya CAF hapa nchini, na tena imeleta fainali mbili. Hakuna timu nyingine ya Tanzania imewahi kuleta fainali ya CAF nchini Tanzania na kombe tukaliona.
Mechi ya kwanza ni utangulizi wa fainali, CAF wanahesabu fainali mechi ya pili tu na ndiyo inayotoa mchezaji bora.
Kitendo cha Joshua Mutale kushinda tuzo ya mchezaji bora wa fainali ni mwisho mzuri wa story ya Simba katika mashindano haya.
Mutale alianza msimu vibaya na mimi ni mmoja wa watu tuliomkatia tamaa. Miezi miwili hivi ya hapa mwishoni katika mashindano ya CRDB Cup akaanza kuonyesha dalili za kuwa bora na jana akashinda tuzo ya mchezaji bora wa fainali mbele ya wachezaji tulioambiwa wana thamani ya mabilioni ya pesa na wanaogombaniwa huko Ulaya.
Ukiacha goli alilofunga, Mutale jana angeondoka pia na assist kama siyo famba aliyofanya Kapombe na angeweza kuipa Simba ubingwa wa CAF.
Ni mwisho bora sana wa story hii ya Simba katika fainali hizi.
NB. Pia ni uthibitisho kuwa ni timu ya Simba SC pekee iliyowahi kuleta fainali ya CAF hapa nchini, na tena imeleta fainali mbili. Hakuna timu nyingine ya Tanzania imewahi kuleta fainali ya CAF nchini Tanzania na kombe tukaliona.
Mechi ya kwanza ni utangulizi wa fainali, CAF wanahesabu fainali mechi ya pili tu na ndiyo inayotoa mchezaji bora.