Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
Wasalamu Wanajamvi...
Kweli kaa kwenye nyumba za kupanga uone mengi. Leo kuna jambo nimeliona nikashindwa kuelewa kama limetokea kwa sababu ya heshima au kwasababu ya mapenzi yaliyopo kwa Wapenzi hawa
Majira ya saa moja jioni nikiwa nimerejea kwenye mizunguko yangu ikabidi nikae nje ya nyumba yetu nipunge upepo kidogo kabla ya kuingia ndani. Nyumba yetu tunakaa wapangaji wengi kidogo na tunatumia mabafu ya nje. Katika nyumba hii kuna Wapangaji wapya ambapo ni Mwanaume na Mwanamke (Kwa mujibu wao wameona)
Basi nimekaa nje hapa nikaona Mwanamke ametoka na ndoo ya kisha akachota maji kutoka kwenye bomba la nje na kuyapeleka katika bafuni (bafu hilo la nje) na kisha akarudi ndani. Baada ya kama dakika 10 hiyo Mwanaume akatoka akiwa kavaa taulo na kwenda kuoga. Alipo maliza akatoka na ndoo akaacha nje ya mlango wa bafu, baada ya muda Mwanamke akaja na kuichukua ile ndoo
Sasa hadi muda huu najiuliza Mwanamke alifanya vile kutokana na mapenzi mazito aliyonyo ana ni nini kingine au ni heshima tu ya mila za kwao. Maana ukiangalia bomba alipochota maji lipo njiani ukitoka kwenye chumba chao kwenda bafuni? Lakini cha zaidi Mwanaume aliacha ndoo bafuni na yeye akaja kuifuata
Wakuu nisaidie siku hizi bado wapo Wanawake wa namna hii?
Kweli kaa kwenye nyumba za kupanga uone mengi. Leo kuna jambo nimeliona nikashindwa kuelewa kama limetokea kwa sababu ya heshima au kwasababu ya mapenzi yaliyopo kwa Wapenzi hawa
Majira ya saa moja jioni nikiwa nimerejea kwenye mizunguko yangu ikabidi nikae nje ya nyumba yetu nipunge upepo kidogo kabla ya kuingia ndani. Nyumba yetu tunakaa wapangaji wengi kidogo na tunatumia mabafu ya nje. Katika nyumba hii kuna Wapangaji wapya ambapo ni Mwanaume na Mwanamke (Kwa mujibu wao wameona)
Basi nimekaa nje hapa nikaona Mwanamke ametoka na ndoo ya kisha akachota maji kutoka kwenye bomba la nje na kuyapeleka katika bafuni (bafu hilo la nje) na kisha akarudi ndani. Baada ya kama dakika 10 hiyo Mwanaume akatoka akiwa kavaa taulo na kwenda kuoga. Alipo maliza akatoka na ndoo akaacha nje ya mlango wa bafu, baada ya muda Mwanamke akaja na kuichukua ile ndoo
Sasa hadi muda huu najiuliza Mwanamke alifanya vile kutokana na mapenzi mazito aliyonyo ana ni nini kingine au ni heshima tu ya mila za kwao. Maana ukiangalia bomba alipochota maji lipo njiani ukitoka kwenye chumba chao kwenda bafuni? Lakini cha zaidi Mwanaume aliacha ndoo bafuni na yeye akaja kuifuata
Wakuu nisaidie siku hizi bado wapo Wanawake wa namna hii?