Hebu wana jf tuliongelee hili, kwa ushuhuda nilionao naona watoto wana mapenzi sana na mama zao kuliko baba. Hebu tuangalie mifano michache, nyimbo nyingi zinazoimbwa dedication ni kwa mama, watu wakipewa nafasi ya kutoa shukrani mara nyingi mama anatajwa tena bila kumuhusisha baba, juzi tuzo za kili wasanii wengi walidedicate tuzo kwa mama, tukiulizana hapa kati ya baba na mama nani unampenda wengi tutajibu ni mama. Mimi najiuliza kwa nini baba mara nyingi hana nafasi mioyoni mwetu? Jamani tatizo liko wapi?