Wadau, hili swala la kampuni ya Tanzanite 1 kunyanyasa wafanyakazi wao kule migodini Arusha lilishawahi kurushwa na ITV na serikali ikaahidi kulishughulikia. Cha ajabu leo asubuhi wakati nasikiliza BBC Swahili inaonekana unyanyasaji umeongezeka maradufu. Wafanyakazi wanapekuliwa na ajabu zaidi unyanyasaji huo unafanywa hadi kwa wanawake na bado wanataka kuleta machine ya X-ray itakayotumika kuwakagua wanapotoka mgodini. Mashine hizo zinaaminika zina madhara makubwa kwa binadamu. Cha kushangaza, mkuu wa polisi mkoani Arusha alipohojiwa na BBC akadai swala hilo ni la wakubwa, halimuhusu....
JE, TUTAFIKA...????
Wa Tanzania tutanyanyaswa hivyi mpaka lini na Wazungu ili hali wakubwa wanafumbia macho swala kama hili?