kingwenje
Member
- Jun 19, 2020
- 79
- 108
Hipo hivi, nilikwenda kwa yule mtumishi wa mungu anaejiita kiboko ya wachawi. Ebwana niliyoyashudia, jamani watu wanajua kutafuta pesa, mimi nasema nitabaki kwa dini yangu, hii ya Romani Katoliki.
Mpaka mwisho wa maisha yangu hakuna mwamposa sijui, musa, wala nani. Sasa nimefika pale na sikua peke yangu, nilikua mimi na ndugu yangu pamoja na mgojwa. Sasa tumefika pale eneo la tukio, mimi nikamwambia ndugu yangu. Ngoja niangalie taratibu hapa nikatafuta wenyeji pale, kuna anko mmoja akaniambia onana na yule dada. Kweli nikamfuata, yule dada akaniambia nenda kakae pale na huyo mgojwa.
Nikaona hapana kwasababu pale nilikua na mgojwa, nikamtafutia kiti aweze kukaa. Mimi nikatoka mpaka kwa yule ndugu kumwambia. Na pia taratibu za yule dada hazikunilidhisha. Sasa wakati nipo kwa ndugu pale, sasa hapa naombeni munisikilize kwa makini, hapa, ndio kuna jambo.
Nipo pale nikamuona mkaka mmoja, yupo na kondoo wake pale, kama kunajambo anaongea nao, na palepale, alikuepo dada mmoja nae nafikiri alikua ni mhusika kwa maana alikua anapanga watu.
Ikabidi nimuendee nae nimuulize talatibu, majibu yake akaniambia niende kule mbele kama mwanzo, nikasema duh, hatari, nikachoka. Unajua lengo langu sikutaka nipoteze muda pale, najaligi sana muda.
Sasa wakati nimerudi kwa yule ndugu tukibadilishana mawazo, pembeni yangu alikua anko mmoja, nikaona sio vibaya kumuuliza, nikamwambia hivi hapa ukitaka kuonana na uyu mtumishi, yule anko akaniuliza umekuja na sh, ngap? Nikaona ngoja nimuite ndugu yangu, nae aje amsikie yule anko, akaendelea kutuambia akasema yeye, amefanya kumleta mke wake pale na kwamaongezi yake yule anko, ametoa pesa sh,40000 lakini bado wanasema haitoshi wanamtaka aongezee lakini wapi.
Akaendelea kutuambia kwamba kunawatu ,wanalalamika wametoa pesa lakini hakuna chochote. Zimeliwa akatudokezea anasema garama zakumuona uyo mchungaji ni Tsh. Laki 5 akatuambia kuna mama yeye walimwambia atoe kwanza Elfu 50000, ataweza kumuona lakini matokeo yake katoa iyo pesa akuna chochote, anatuambia mpaka muda ule anadai pesa yake, nasikia anataka kwenda police.
Yaani kwakweli nilichoka mimi na yule ndugu wakati anaendelea kufunguka yule anko, akaja yule dada akamwambia yule anko aondoke pale, duh yaani hatari yule ndugu akaniambia niende nikamchukue mgojwa tusepe. Jamani tuweni makini mambo ni mengi.
Mpaka mwisho wa maisha yangu hakuna mwamposa sijui, musa, wala nani. Sasa nimefika pale na sikua peke yangu, nilikua mimi na ndugu yangu pamoja na mgojwa. Sasa tumefika pale eneo la tukio, mimi nikamwambia ndugu yangu. Ngoja niangalie taratibu hapa nikatafuta wenyeji pale, kuna anko mmoja akaniambia onana na yule dada. Kweli nikamfuata, yule dada akaniambia nenda kakae pale na huyo mgojwa.
Nikaona hapana kwasababu pale nilikua na mgojwa, nikamtafutia kiti aweze kukaa. Mimi nikatoka mpaka kwa yule ndugu kumwambia. Na pia taratibu za yule dada hazikunilidhisha. Sasa wakati nipo kwa ndugu pale, sasa hapa naombeni munisikilize kwa makini, hapa, ndio kuna jambo.
Nipo pale nikamuona mkaka mmoja, yupo na kondoo wake pale, kama kunajambo anaongea nao, na palepale, alikuepo dada mmoja nae nafikiri alikua ni mhusika kwa maana alikua anapanga watu.
Ikabidi nimuendee nae nimuulize talatibu, majibu yake akaniambia niende kule mbele kama mwanzo, nikasema duh, hatari, nikachoka. Unajua lengo langu sikutaka nipoteze muda pale, najaligi sana muda.
Sasa wakati nimerudi kwa yule ndugu tukibadilishana mawazo, pembeni yangu alikua anko mmoja, nikaona sio vibaya kumuuliza, nikamwambia hivi hapa ukitaka kuonana na uyu mtumishi, yule anko akaniuliza umekuja na sh, ngap? Nikaona ngoja nimuite ndugu yangu, nae aje amsikie yule anko, akaendelea kutuambia akasema yeye, amefanya kumleta mke wake pale na kwamaongezi yake yule anko, ametoa pesa sh,40000 lakini bado wanasema haitoshi wanamtaka aongezee lakini wapi.
Akaendelea kutuambia kwamba kunawatu ,wanalalamika wametoa pesa lakini hakuna chochote. Zimeliwa akatudokezea anasema garama zakumuona uyo mchungaji ni Tsh. Laki 5 akatuambia kuna mama yeye walimwambia atoe kwanza Elfu 50000, ataweza kumuona lakini matokeo yake katoa iyo pesa akuna chochote, anatuambia mpaka muda ule anadai pesa yake, nasikia anataka kwenda police.
Yaani kwakweli nilichoka mimi na yule ndugu wakati anaendelea kufunguka yule anko, akaja yule dada akamwambia yule anko aondoke pale, duh yaani hatari yule ndugu akaniambia niende nikamchukue mgojwa tusepe. Jamani tuweni makini mambo ni mengi.