missnyakanazi
Ha ha haaa. Unadhani mama wa kambo alinifanya mazuri basi? Yaani maskini ya mungu mi sijui hata kosa nililomfanyia (I was only 5 years old), nashinda na njaa wakati ndani kuna chakula cha kutosha. Wanapewa majirani vingine vinamwagwa, mi nashinda na njaa mdomo umekaukaaaaa! Siku mshua akirudi ndio napewa kipande cha nyama cha kuzuga.
Akiondoka kesho yake napikiwa maharage ya kula hata siku nne (sikumbuki kama hata chumvi yalikuwa yanawekwa yale), na nakula jioni tu, mchana napigishwa pasi ndefu wakati mdingi ana mahela kibao, kila akirudi vyakula vya kutosha vinaletwa home, hasa nyama za porini. Nimepiga hizo since 5 years old mpaka std 7. Acheni utani nyie watu.
Siku njaa ikanizidia nikadokoa nyama motoni ambayo alikuwa anamuandalia mwanawe, weeeee! Alinitandika mpaka nika-faint nilipozinduka
(hapa sasa ndio patasababisha nikill mwanamke), akanishika mdomo wangu akauachanisha akanitemea mate ya kutosha humo, sijui yalikuwa makohozi yale (ghrrrrrrr!). Siwezi sahau.
Ningekuwa mkubwa labda ningechukulia ni denda tu nikapotezea, sasa nilikuwa std 3 tu jamani.