Jamani shemeji mchepuko ananiwazisha

Jamani shemeji mchepuko ananiwazisha

MLALUKO JR

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2015
Posts
962
Reaction score
309
Mimi ni kijana nina umri wa miaka 22, pia nipo chuo kikuu mwaka wa kwanza. Kuna dada ya shemeji yangu ambaye ameolewa ila katika kukua kwetu yaani utotoni wakati tulipokuwa shule ya msingi tulikuwa na uhusiano but sikuwahi kuzini.

Lakini wakati nilipomaliza kidato cha sita kwa hali isiyokuwa ya kawaida tulipoweza kuzini kwa siku ya kwanza na siku iliyofuata alikuja tena na tukazini tena, kwangu ilikuwa mara ya kwanza kumjua mwanamke na kufanya mapenzi.

Kitu kinachoniumiza mpaka leo, binti huyo ni mke wa mtu pia ameshazaa mara mbili, nataka nimtafute mme wake nimuombe msamaha ili niwe huru kifikra na moyo unaniuma sana nifanyaje But yeye huyo mwanamke nilimwacha siku nyingi.


Tushauriane vizuri ndugu zangu
 
sasa huo ni ukorofi mana mi sioni la msingi hapo...! kama ulishaachana na huyo mwanamke! labda hujui wapi pa kukufanya uwe huru kifikra...! huoni kwamba utaenda kuamsha mambo mengine na huenda ukawatenganisha kabisa...!? mi nadhan kuwa huru kifikra kwakuwa ni mdhambi, rudi kwa imani ya dini yako ufanye maombi maalum ukiwa peke yako na si vinginevyo
 
Mh!Karne hii watu wenye mioyo ya hivyo hawapo acha kutuzuga.
 
Alikuwa bnt wa kwnz kumjua bt now ninae mwingine ambaye nina malengo ya kuoa km atakuwa mvumilivu.Ila nikimwona jamaa nasikitka kupta kiasi.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom