Jamani nimeamua kuokoka

Jamani nimeamua kuokoka

any way its long story.. natumia simu ndogo siwezi kuandika vitu vingi... lakini ni visasi vya muda mrefu vya watu niliotoa siri zao..
na kwa nini utoe siri za washirika wako? Huoni kama wewe ni mnafki na umeokoka kinafki kwa kuwa huenda mlizurumiana ndo ukaamua kutoa siri zao? Ebu tuambie ni siri zipi hizo? Nakudediketia wimbo ule wa wagosi wa kaya kibaka umeokoka
 
Mwaka 2014 nilipita katika misukosuko mingi ikiwemo kukoswa koswa kuuwawa mara kadhaa.. hata hivyo ni Mungu ndie aliyekuwa akinilinda kwa makusudi yake ili nimtumikie na kuwapeleka watu wengi kwa Yesu kupitia kazi yangu.. hivyo jana tar 1/1/2015 nimeamua kumpa Bwana Yesu kuwa mokozi wa maisha yanguj.. najisikia amani sana na hofu yote imekwisha..
Mungu awabariki wana JF wote,
happy new year.
Sisi mwaka 2014 ulikuwa poa sana. Tunahaja ya kuokoka?
 

JE, UNATAKA KUOKOKA SASA?

Tunasoma haya katika LUKA 1:77, “Uwajulishe watu wake wokovu, katika kusamehewa dhambi zao”. Hii ina maana kwamba ukiisha kutubu dhambi zako leo utasamehewa kwa hakika, na hivyo kupata wokovu mara moja. Je, kweli utasamehewa? Jibu ni Ndiyo! Yesu mwenyewe anasema katika YOHANA 6:37, “……….Wala yeyote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe”. Hivyo kwa dhahiri, leo hii, dakika hii hii, utasamehewa na kupata wokovu. Je, uko tayari kuokoka sasa na kuhesabiwa miongoni mwa wale watakaoingia mbinguni na kuishi na Mungu milele, hata wakiiaga dunia sasa hivi? Ukiwa tayari kuifuatisha sala ifuatayo ya toba, mara tu baada ya sala hii, nitakuombea na kwa ghafla utawezeshwa kushinda dhambi.

Je, uko tayari kuifuatisha sala hii sasa?
Najua uko tayari. Basi sema maneno haya,

“Mungu Baba, natubu dhambi zangu zote kwa kumaanisha kuziacha. Naomba unisamehe na kuniosha dhambi zangu kwa damu ya Yesu iliyomwagika msalabani. Niwezeshe kushinda dhambi kuanzia sasa. Liandike sasa jina langu katika kitabu cha uzima mbinguni. Asante kwa kuniokoa, katika Jina la Yesu, Amen”.

Sasa ninaomba kwa ajili yako, “Mungu Baba msamehe kiumbe wako huyu dhambi zake zote, na mpe uwezo wa kushinda dhambi kuanzia sasa na kumuokoa. Mbariki kwa baraka zote katika Jina la Yesu, Amen”. Tayari umeokoka. Ili uzidi kuukulia wokovu, hakikisha unahudhuria mafundisho katika Kanisa linalohubiri wokovu.

MUNGU AKUBARIKI!!!

naomba kuuliza swali fupi ndugu. mtu akifa sasa hiv anakwenda wapi?
 
siku moja niliwazuga masela wangu kilingeni kuwa nimeacha pombe na kuagiza coca-cola...aisee walimaindi na kuja mbogo hao...nalinganisha reaction yao na comments za watu humu...
 
Mwaka 2014 nilipita katika misukosuko mingi ikiwemo kukoswa koswa kuuwawa mara kadhaa.. hata hivyo ni Mungu ndie aliyekuwa akinilinda kwa makusudi yake ili nimtumikie na kuwapeleka watu wengi kwa Yesu kupitia kazi yangu.. hivyo jana tar 1/1/2015 nimeamua kumpa Bwana Yesu kuwa mokozi wa maisha yangu.. najisikia amani sana na hofu yote imekwisha..
Mungu awabariki wana JF wote,
happy new year.
Karibu sana kwa Yesu
 
naomba kuuliza swali fupi ndugu. mtu akifa sasa hiv anakwenda wapi?

Ndugu uliyeuliza swali hili unastahili kupongezwa kwa sababu watu wengi sana hawajui hatima yao baada ya kufa na kabla ya hukumu ya mwisho, na wengi wa watu hawa ni wakristo. Kimsingi watu wanaokufa wapo wa aina mbili tu yaani wale waliompokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yao na wale ambao ama ni wakristo lakini hawamwamini Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yao hivyo wanaishi katika maisha ya dhambi hadi vifo vyao au hawaamini kabisa kuwa Yesu ni njia, kweli na uzima. Kwa kifupi ni kwamba ulimwengu wa roho una maeneo halisi kabisa ambako roho za watu wanaokufa huenda, Luka16:19-31.

Kabla Yesu hajafa msalabani kuna sehemu ilikuwa inaitwa shiol hili neno ndio hilo limetafsiriwa na biblia linaitwa kuzimu, yaani ulimwengu wa wafu, ama eneo wanalokaa wafu. Waliokufa katika dhambi ama waliokufa katika haki. Shiol ilikuwa imegawanyika sehemu mbili shiol ya watu waliokufa katika haki na shiol ya watu waliokufa katika dhambi, na hii ilikuwa kabla Yesu hajafa msalabani.


Mwanzo 37:35 "…Nitamshukia mwanangu hata kuzimu nikiwa nasikitika…" Yaani hapa Yakobo anamaanisha akifa atamshukia mwanae Yusufu huko kuzimu, hii ilikuwa ni kuzimu ya waliokufa katika haki.
Torati 32:22 "…Moto umewashwa kwa hasira yangu unateketea hata chini ya kuzimu…" Hii ni kuzimbu ya waliokufa katika dhambi.

"Kusimu upande wa wenye haki, na kuzimu upande wa waliokufa dhambini Kabla ya Yesu Kristohajafa msalabani"

1 Samweli 2:6 "…Hushusha hata kuzimu, tena huleta juu…" Zaburi 6:5 "…Maana mautini hapana kumbukumbu lako; katika kuzimu ni nani atakayekushukuru?..." Zaburi 16:10 "…Maana hutakuachia kuzimu nafsi yangu…" Yuda 1:6 "...Amewaweka vifungo vya milele chini ya giza…" kuzimu kwa lugha ingine ni chini ya giza kwenye vifungo vya milele.

Yesu alipokufa akashuka kuzimu ya waliokufa katika dhambi akamnyang'anya yule joka ufunguo wa kuzimu na mauti, halafu akaeleke upande wakuzimu ya Ibrahimu (kuzimu ya walikufa katika haki) akawaambia yule uzao wa mwanamke ndio mimi, akawahubiria manabii wote huko kuzimu, na kuwaambia nimekuja kuwahamisha twende juu mbinguni, huku sio mahala penu. Yale makaburi kufunguka ilikuwa ni ishara ya uhamisho wa watu wote waliokufa katika haki kutoka kuzimu ya chini na kwenda mbinguni (paradiso) kule Yesu anakaa. Yesu akawaambia sasa tunahama huku tunaenda paradiso. Kwa hiyo baada ya hapo kuzimu ikawa ni mahali pa wafu waliokufa kwatika dhambi na paradiso (mbinguni) ikawa ni makao ya waliokufa katika haki huko wakimuimbia Mungu,na kufurahi.

Unapokata roho huwa kuna malaika maalumu wanaochukua roho yako, kama ulikuwa unatenda dhambi malaika wa giza wanabeba roho yako wanashusha mpaka kuzimu(gereza la milele), na kama ulikuwa unatenda haki, malaika kutoka mbinguni wanabeba roho yako na kuipeleka mbinguni (pradiso), Ufunuo 20:13. "…Kuzimu ikawatoa watu waliokuwa ndani yake…" Kuzimu ni makao makuu ya shetani, na ziwa la moto ni sehemu ya hukumu ya wale waliokufa katika dhambi, ukishafika hapo unakuwa mfungwa, na unaanza kumtumikia shetani. Babu yako yule aliekufa katika dhambi yupo kuzimu hajakaa tu kule, yupo anapiga mzigo huko, ndio maana utasikia watu tunaowarudisha msukule hapa, ama watu waliokuwa wamekufa wakifufuka hapa kwetu utasikia kazi yangu ilikuwa ni kwenda kwenda kuua watoto wadogo mahosipitali wengine utasikia nilikuwa nasababisha ajali barabarani, hizo ndizo kazi za wafu huko kuzimu.
 
Mwaka 2014 nilipita katika misukosuko mingi ikiwemo kukoswa koswa kuuwawa mara kadhaa.. hata hivyo ni Mungu ndie aliyekuwa akinilinda kwa makusudi yake ili nimtumikie na kuwapeleka watu wengi kwa Yesu kupitia kazi yangu.. hivyo jana tar 1/1/2015 nimeamua kumpa Bwana Yesu kuwa mokozi wa maisha yangu.. najisikia amani sana na hofu yote imekwisha..
Mungu awabariki wana JF wote,
happy new year.

asante kwa baraka amein
 
Mungu akuatamie ,usirudi nyuma kamwe,umepata ushindi wa maisha haya ya dunia ,uzima wa milele hongera mshike sana mungu ,na neno lake .
 
Kwa Yesu kuna raha! Mimi niliokoka toka mwaka1979, tangu hapo mpaka leo nimeshuhudia wema wa Mungu nyakati zote. Mwisho wa siku atanifikisha mbinguni.
 
You have made a very wise decision.

Kuchagua njia ya kwenda mbinguni kwenye uzima wa milele, na kuepuka kwenda jehanum kwenye lile ziwa la moto.

Congratulations to you.

ubarikiwe sana. na jambo la muhimu kujikabidhi mikononi kwa mungu kwani ndio muweza wa kila jambo
 
siku moja niliwazuga masela wangu kilingeni kuwa nimeacha pombe na kuagiza coca-cola...aisee walimaindi na kuja mbogo hao...nalinganisha reaction yao na comments za watu humu...

Walishasema kila mtu atabeba mzigo wake. vijana acheni kuvuta majani gizani
 
Mwaka 2014 nilipita katika misukosuko mingi ikiwemo kukoswa koswa kuuwawa mara kadhaa.. hata hivyo ni Mungu ndie aliyekuwa akinilinda kwa makusudi yake ili nimtumikie na kuwapeleka watu wengi kwa Yesu kupitia kazi yangu.. hivyo jana tar 1/1/2015 nimeamua kumpa Bwana Yesu kuwa mokozi wa maisha yangu.. najisikia amani sana na hofu yote imekwisha..
Mungu awabariki wana JF wote,
happy new year.

Picha tafazari
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom