James St. Patrick
Senior Member
- Jun 23, 2011
- 162
- 62
Huyu ni kama dada yangu, ni mwalimu wa shule ya msingi katika shule moja mkoani Tabora na kiumri anaelekea 30 hivi, nilimfaham baada ya kupanga kwetu miezi kadhaa iliyopita, ana bwanake ambaye nae pia alikua mwalimu wa shule ya sekondari mkoani Tabora! Tatizo ni hili huyu dada anahitaji mtoto, aliwahi kujifungua mtoto akafariki miaka kadhaa nyuma, jamaa amekua na tatizo upande wa tendo la ndoa baada ya kukataa kumuoa dada mmoja aliyemzalisha mpaka leo tatizo hilo linazidi kuongezeka hata ujauzito wa kwanza kwa huyu dada ilikua ka bahati tu! Mwaka jana jamaa alienda chuo Dom, sasa kila akija hakuna kitu na habari mbaya zaidi ni likizo hii iliyopita jamaa alishindwa kabisa hata baada ya kutegeshewa siku za hatari! Mpaka wanaagana wamekubaliana kwamba kuna dawa jamaa ataanza kutumia ikishikana bora waachane kwa amani, amekua akiniomba ushauri kwa muda sasa mpaka imefikia hatua sijui nimwambie nini, tafadhali naombeni ushauri wenu ili nimsaidie dada huyu! It is a true story, take it seriously!