Jamani mwenzenu DSTV imenishinda

Jamani mwenzenu DSTV imenishinda

Hata mie nimeamua kuachana nao yaani kila baada ya miezi 3 wanapandisha bei zao.
 
Hahahhaha, JF rahaa sana aisee..Karibun Bein sport HD. Channel 20 HD zote sports tu, malipo ni 45,000 tu kwa mwezi

tupe hiyo bean sport unapataje maana mie naipata kupitia KODI, sasa kwenye king'amuzi inakuaje
 
Kile cha pass wamekifikisha sh ngapi maana tulizoea tsh 22,000/= ila itabidi tusepe maana hawasikii

Mpaka jana tarehe 30/09/2015 kilikuwa shs 23,500/=, sasa kuanzia leo tarehe 01/10/2015 sijui kitakuwa shs ngapi maana wamesema kitapanda. Inasikitisha sana!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!BONGO.
 
Hiki ni 23000 mkuu wameongeza buku, hiki ndo nimekuwa member wa kukilipia kila mwezi, cha premium nimeachana nacho life inakaba unless kama nipo mapumziko ndo nalipia
Nitaendelea nao buku halinishindi japo kubwa.....Kwa soka nimehamia Azam
 
Nunua Qsat 28G weka na dish ya nile sat peleka muelekeo wa south Africa mpango mzima!

Hii ukitumia dish la dstv halifai maana kujaza madish ndani nayenyewe ni shiida. ukinunua receiver na decoder yake bila dish itafaa na kwa dar ni wapi wanapatikana maana kiukweli dstv ni majanga
 
Watanzania wengi wanapenda vitu vizuri ila wakisikia bei tu wanaanza lia lia
 
Mbona mnalialia, kwani mmejipangaje?

Acheni ubinafsi, nenda bar jumuika na wenzako jipatie kinywaji upendacho na kwa raha zako unacheck game!

Faida ni nyingi kuliko kujifungia ndani. Kwanza utatumia gharama kidogo, pili unaweza pata hata dili la kuongeza kipato, tatu unachangia maendeleo ya mwekezaji wa ndani, nne unawahakikishia hata wahudumu upatikanaji wa mishahara yao mwisho wa mwezi n.k n.k
 
Nilishawapiga chini tangu last May, kwass nawatch match via screaming site online
 
Nliacha baada ya kugundua nalipa ela nyingi naangalia siku nane au saba za premier league kwa mwezi nkaamia azam
 
mafisadi wa fisiem wanashare kwenye mu.lti choice hivyo wananufaika na upandaji holela wa subscription fee!
 
Aisee poleni sana. walisema....Kama sio DSTV zima...Ila mi niligoma kwa kweli.
 
Dstv nimeshawamwaga! Mimi ni mpenzi wa EPL na nilikuwa mwanachama wa kudumu wa compact plus iliyokuwa inaonyedha EPL kupitia SS3. Tangu channel hii ya SS3 ilipohamishiwa kwenye kifurushi cha premium linachodai kilo 2 kwa mwezi, nimeamua kuanzisha mapenzi na la liga ambayo inapatikana azam TV ! Dstv bye bye!
 
Mimi pia imenishinda kifurushi 56,000 kimepanda hadi 84,000. Ila naskia south Africa bei vifurushi IPO chini
 
ngoja tukaangwe mpaka tutakagozinduka kutoka usingizini. haya ndio madhara ya kuishobokea CCM ambao mkada wao ndiyo wamiliki wakubwa wa haya makampuni ya kinyonyaji.

Duh hii kali yaani hadi wewe kushindwa kilipa DSTV ni CCM inailaumu..., au CCM ndio wamiliku wa DSTV mwisho ukikosa choo wiki moja utalaumu CCM pia
 
Hamia ZNZ, huku zstv ni 20000 tu kwa mwezi na EPL unaangalia.
 
Back
Top Bottom