Najiuliza sana sana sana sipati majibu. Ni dhahiri mwanasiasa Zitho Z Kabwe alikuwa akipost chochote kinachohusiana na siasa wachangiaji walikuwa wengi tofauti na ilivyo sasa. Kuna post imewekwa hapa kuonesha mchango wake kwa bajeti inayojadiliwa sasa lakini siamini response iliyopo. Jamani ni kwa nini? Hata wale watetezi wake kutoka ccm hawaonekani kuchangia na kumpongeza kama ilivyo ada yao. Natoa rai tuendelee kuwa nae na tuendelee kumuunga mkono pale anapotoa hoja zenye maslahi kwa taifa. Au mnasemaje wadau?