G11
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 225
- 64
Yuko busy na mambo ya kitaifa. Atarudi muda si mrefu.
Kwani CHADEMA baraza kuu mnaliitisha lini?
Hapo kwenye red isomeke Kigoma
Yuko busy na mambo ya kitaifa. Atarudi muda si mrefu.
Kwani CHADEMA baraza kuu mnaliitisha lini?
Moja ya sifa kuu za wabunge wa CDM ni umaarufu, na umaarufu wao huupata kwakuwa huongea sana bungeni na kwa kiasi kikubwa hoja zao huwakosha sana wananchi wa nchi hii.
Mmoja wa watu niliozoea kuwaona wakipambana ili kuweka mambo sawa ni huyu jamaa wa Kigoma akiitwa kwa jina la Zitto. Ninachoshangaa ni kuwa simsikii tena tangu bunge la katiba lianze. Simsikii akiongea wala simuoni akimulikwa na makamera ili hata tumuone tu kama yupo.
Hivi huyu mtu yupo hayupo? Kama hayupo yuko wapi? Na kama yupo mbona kalowa hivyo? Anakuwa kama Augustino Mrema?
Kuna watu wasipolitaja taja jina la ZZT, hujisikia kuwashwa hadi wamtaje tuu roho zao zitulie!.
Kuna wajinga wajinga fulani wasiojua wanadhani haya mabishano yanayoendelea kwenye bunge maalum ni vikao vya bunge maalum vimeanza!. No way!, vikao vya bunge maalum kujadili katiba havijaanza!, hiki kinachoendelea ni "semina tuu!"
"men of integrity!" wamejituliza kimya tuu, hawana sababu ya kupigishana kelele kwenye semina, warsha na makongamano!, wao wataibuka kwenye real thing na hoja zenye mashiko!. Jee mmeishamsikia Prof. Abdalah Safari?. Kila siku yupo namuona ni mwanasheria aliyebobea na yet amejinyamazia tuu!.
Kuna watu wana kimbembelembele tuu kuongea sana, ila wanamwaga pumba tuu!, na kuna watu kwa kutoongea huko ndiko busara zao zilikolalia!.
Pasco.
gogo Zito
jiwe Zito
etc.
Zitto ni kijana shupavu sana, na ni mhimili wa siasa za Tanzania, hatutegemei kumuona akiropoka ropoka hovyo kwenye bunge la katiba. Katika CHADEMA yote hakuna mwenye akili nyingi kama Zitto.
tupo watanzania almost mil 45..tungekuwa na watanzania japo milion 2. Wenye akili kama ya pasco sasaivi tusingekuwa tunaandaa katiba, tungekuwa tunawaza kwenda sayari nyingine..ila aina ya watz tulio wengi ni kama Sugu, josephine mshumbusi, ole sendeka, poul makonda na le mutuz. Pasco nafurahia sana uwezo wako wa kujenga hoja hata pale unapokuwa unajadili nisivyovipenda, huwa najikuta napenda uwasilishaji wako. Mungu awajalie vijana wako nao wawe majiniaz.
Zitto si mtu wa kuropoka hovyo siyo kama lisu ambao huongea hata ubwabwa ngoja kazi ya kutunga katiba ianze utamuona motto wake.