Jamaa atengewa hotpot lenye mkaa dinning

Jamaa atengewa hotpot lenye mkaa dinning

BUSH BIN LADEN

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2019
Posts
8,628
Reaction score
19,810
Kwema wana jukwaa?

Kuna jamaa yangu kakumbwa na mkasa amenisumulia nimebaki kinywa wazi.

Ni hivi jamaa anaishi na mke wake na ndoa haina muda mrefu akiwa anajishughulisha na kazi za miradi ambayo huwa inamfanya awe mtu wa kusafiri sana.

Sasa jamaa huwa ana utaratibu wa kuja na gunia la mkaa anaporejea nyumbani kama kawaida ya wanaume tulio wengi tunapotoka safarini kuja tumebeba chochote kwa ajili ya familia zetu.

So siku hiyo amefika toka safari akaja na mkaa kama kawaida akapokelewa, mkewe kamtengea maji bafuni. Jamaa kaoga amemaliza kakaribishwa mezani kwa ajili ya chakula. Mkewe kaongoza sara na mwisho jamaa kafungua hotpot ili apakuwe. La haula si kafungua hotpot kakutana na mkaa.

Jamaa akiwa kapigwa na mshangao si akauliza hiki ni kitu gani, mke akamjibu ni mkaa. Jamaa anauliza ndo nini sasa kunitengea mkaa, mke anajibu nimekutengea mkaa liwe funzo maana unaona mahitaji ya humu ndani ni mkaa tu kwamba kila ukirudi kutoka safari unachoona cha muhimu sana ni gunia la mkaa.

Jamaa kauliza sasa kwani shida iko wapi, mke anajibu shida ipo kwa sababu mkaa hua unahitaji vitu vipikwe ili kupata chakula kwahiyo nilitegemea wakati unakuja mara zingine uwe unabeba mchele, ndizi, maharagwe, kuku nk.

Jamaa akabaki mdomo wazi si ndo kunisimulia nikamuuliza kwani hivyo vitu kama mchele, maharagwe nk havipo nyumbani jamaa kadai vipo na hata kama havipo hua anaacha hela ya mahemezi anaposafiri.

Kiukweli mpaka hapa hapa sijaona kwanini jamaa katengewa msosi wa mkaa kwenye hotpot.
 
Vijana mnapotaka kuoa kuweni makini wakati wakuchagua wake wa kuoa

Sasa waweza kuniambia huyo mwanamke anatofauti Gani na Chizi Kibedui

Kuna watu wengine ni vichaa badala ya kuwaacha na vichaa vyao mnawachukua mna waoa/wana waoa na hatimae mnakuwa mmewapa majukumu mazito ambayo hayaendani na uwezo wao wakufikiri

Msipo kuwa makini kila siku mtakuwa mnalia lia na Mikasa ya kutisha katika ndoa itakuwa haiishi

BTW -- Nimecheka sana ...mkaa !!!!
 
Anaposafiri kuna anayemletea gesi ili apikie sasa ndugu yako wanamwambia kuwa huyo mwanamke asimchukulie poa yeye si wa kupikia mkaa.
 
Vijana mnapotaka kuoa kuweni makini wakati wakuchagua wake wa kuoa

Sasa waweza kuniambia huyo mwanamke anatofauti Gani na Chizi Kibedui

Kuna watu wengine ni vichaa badala ya kuwaacha na vichaa vyao mnawachukua mna waoa/wana waoa na hatimae mnakuwa mmewapa majukumu mazito ambayo hayaendani na uwezo wao wakufikiri

Msipo kuwa makini kila siku mtakuwa mnalia lia na Mikasa ya kutisha katika ndoa itakuwa haiishi

BTW -- Nimecheka sana ...mkaa !!!!
😀😀 Wengi siku hizi tunaangukia mapepo sio wanawake
 
Hapendi muvi za karate yeye anapenda muvi za mume bwege, za mume kulishwa limbwata na muvi za shilole kumchapa Nuhu Mziwanda
Huyu itabidi tumkalishe kikao anatuaibisha kwakeli kwanza ilitakiwa ile amefunua tu hotpot na kukuta mkaa angemuuliza mbona hivi sasa ile anaanza tu kujibu hapohapo anamrukia na kichwa kile cha ulipo tupo.. hicho kichwa kwa tunaojua kukipiga mtu lazima atoke na nundu..😂
 
Huyu itabidi tumkalishe kikao anatuaibisha kwakeli kwanza ilitakiwa ile amefunua tu hotpot na kukuta mkaa angemuuliza mbona hivi sasa ile anaanza tu kujibu hapohapo anamrukia na kichwa kile cha ulipo tupo.. hicho kichwa kwa tunaojua kukipiga mtu lazima atoke na nundu..😂
Mke hapigwi vichwa, utasababisha kichaaa chake kuongezeka Mara elfu tano.
Tayari huyo mke ana sifa za yule mfungwa mpiga kelele wa JF
 
Mke hapigwi vichwa, utasababisha kichaaa chake kuongezeka Mara elfu tano.
Tayari huyo mke ana sifa za yule mfungwa mpiga kelele wa JF
😂😂
Wengine adabu hawana Sasa utampiga kwenzi.. akionewa huruma Basi anapigwa mitama miwili then unambembeleza..😅
 
😂😂😂
Mkaa? Waoaji mnaangalia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom