Bondpost
JF-Expert Member
- Oct 16, 2011
- 6,602
- 9,353
Imekuwa alfajiri, simu yangu inaita, naipokea na kusikia sauti ya kike, anajitambulisha kuwa ni mke wa rafiki yangu. Nahamaki kwa kudhani jamaa amepatwa na ajali au vipi kwani nae ni mlevi kwa muda sasa.
Shemeji ananiita nyumbani kwao, nafika nakuta mke analia na bwana amelala fofofo, nauliza kama rafiki yangu anaumwa au vipi shemeji ananiambia kalala ila nikae anisimulie ndipo tumuamshe mshkaji. Naamua kukaa nipate kuelewa kwa nini yule bwana kalala usingizi wa pono huku mkewe akilia alfajiri yote ile.
Mwanamke anasema jamaa amerudi kalewa, mke akamsaidia kushuka kwenye gari mpaka ndani, lakini alipofika sebuleni jamaa akawa mzito so mke akaamua amlaze kwenye kochi, sasa akamvua shati na akawa anamvua suruali ndipo akakutana na kituko cha mwaka.
Jamaa ameivaa ndomu na mchuzi upo ndani, mkewe kaishiwa nguvu, anataka kuondoka ila ndio ana mimba na hana kazi kwani ndo amemaliza masomo ya chuo kikuu anataka akijifungua ndo awe busy kusaka kazi, mjini ana ndugu mmoja ambaye hawaivi.
Nikaamua kumuamsha jamaa na kumuuliza kilichotokea, jamaa hana la kufanya kukataa hawezi ila kabaki kuomba msamaha. Naye tulipokuwa wawili nikamuuliza kwa nini kafanya hivyo? Naye anachokumbuka alikuwa kwa party ya ofisi, kuna mwanamke mzambia ni bosi wake walipiga ma-cocktail ya kumwaga wakaishia kuji-do kwenye gari. Kilichoendelea hakumbuki.
Mkewe kaomba kukaa kwangu japo apate muda wa kufikiria zaidi, nimeongea na wife wangu amekubali ili tuisevu ndoa yao. Mke wa jamaa anaingia jioni ya leo. Wandugu mnadhani kwa hili tulilofanya tupo sawa?
Shemeji ananiita nyumbani kwao, nafika nakuta mke analia na bwana amelala fofofo, nauliza kama rafiki yangu anaumwa au vipi shemeji ananiambia kalala ila nikae anisimulie ndipo tumuamshe mshkaji. Naamua kukaa nipate kuelewa kwa nini yule bwana kalala usingizi wa pono huku mkewe akilia alfajiri yote ile.
Mwanamke anasema jamaa amerudi kalewa, mke akamsaidia kushuka kwenye gari mpaka ndani, lakini alipofika sebuleni jamaa akawa mzito so mke akaamua amlaze kwenye kochi, sasa akamvua shati na akawa anamvua suruali ndipo akakutana na kituko cha mwaka.
Jamaa ameivaa ndomu na mchuzi upo ndani, mkewe kaishiwa nguvu, anataka kuondoka ila ndio ana mimba na hana kazi kwani ndo amemaliza masomo ya chuo kikuu anataka akijifungua ndo awe busy kusaka kazi, mjini ana ndugu mmoja ambaye hawaivi.
Nikaamua kumuamsha jamaa na kumuuliza kilichotokea, jamaa hana la kufanya kukataa hawezi ila kabaki kuomba msamaha. Naye tulipokuwa wawili nikamuuliza kwa nini kafanya hivyo? Naye anachokumbuka alikuwa kwa party ya ofisi, kuna mwanamke mzambia ni bosi wake walipiga ma-cocktail ya kumwaga wakaishia kuji-do kwenye gari. Kilichoendelea hakumbuki.
Mkewe kaomba kukaa kwangu japo apate muda wa kufikiria zaidi, nimeongea na wife wangu amekubali ili tuisevu ndoa yao. Mke wa jamaa anaingia jioni ya leo. Wandugu mnadhani kwa hili tulilofanya tupo sawa?