ngudengude
JF-Expert Member
- Jul 2, 2015
- 1,175
- 466
CCM imemdhalilisha sana huyu Jaji, yaani Makamba na Membe waliofungiwa kufanya siasa kwa mwaka mmoja ndio wenye maadili kumshinda huyu Jaji? Kweli CCM kiboko!
Ni sawa na kununua sanda baada ya mazishi...
Heri ya huyu Jaji kuliko kapi lenu Lowassa ambalo saa hizi ndiyo linajifanya lina uchungu na watanzania kisa lilikatwa na ccm.Ni mbinafsi,mnafiki na hana uzalendo kwa nchi yake.Taifa lilipofanyiwa ufisadi kisha yeye kuamua kujiuzulu na kukaa kimya ni usaliti mkubwa kwa watanzania.Malipo ya kufanya hivyo alitaka apewe Urais.What he cares ni madaraka na si watanzania.Tungemuelewa sana kama baada ya kashfa ile angejiuzulu na kuhama chama kwenda kupigania ukombozi mahali pengine.Badala yake akaanza harakati za usaliti ndani ya chama ili kutimiza malengo yake binafsi.Pigeni kelele tu humu sababu thamani yenu ni bilioni 10 but wananchi wametulia tulii sababu wanajua ni mtu ambaye hafai na tayari Rais wao wanaye mioyoni mwao.M4C,maandamano mpaka damu za watu kumwagika,migomo na vurugu bungeni kumbe thamani yake ni bilioni 10 tu
Lowasa hasafishiki hata kwa fagio la chuma, kachafuka mnoo, ni mtu wa propaganda tu hana lolote, Magufuli oyeee
Hili lingefanyika kwa kufuata katiba yao ya CCM kila mtu angeridhika. Kamati ya maadili ni kitengo katika secreterieti ya chama itakuwaje na nguvu na maamuzi kuliko hata kamati kuu?!!Kama mgombea wa ukuu wa mtaa ,udiwani n.k. wanapewa nafasi ya kujinadi na kuomba kura katika vikao husika , je wagombea Urais kupitia CCM hilo lilifanyika? Nina hakika wote waliokatwa urais CCM a.k.a makapi na familia zao hawataipa kula CCM ingawaje wako CCM kimwili.Wasingeweza kupitishwa kugombea urais wote 40. Ilikuwa lazima apatikane mmoja wao katika wale wote. Hili lazima alijue na kila Mtanzania alijue
Pinda naye anatoa ya moyoni lini?
naona umekomenti na kutupa kasimu kako hutaki hata kuona uchafu ilioandika na Udogi wako
Ni kweli ni kapi tu. Angelikuwa na lolote la maana ansingesema eti anaogopa kusema ili asibadilishe upepo w auraisi. Huyu ni kapi tena halifai. Hajitambui na hana uchungu na nataifa. Asingekuwa kapi, asinge sita kusema kweli yoyote anayoijua ambayo ingewafanya Watanzania waamue kuchagua kiongozi kwa busara kwa kutumia taarifa sahihi ili kujenga nchi.
Huyu ni kapi tu linaloenda na upepo, hana uchungu na nchi, hana ujasiri wa kufanya maamuzi na hana uwezo hata mdogo wa kuikomboa nchi. Kajaa unafisi na ubendera fuata upepo.
Kweli ni kapi tena lisilokomaa, na ambalo halifai. kusema baada a uchaguzi ni kuwazomea Watanzania na hila za kusababisha machafuko
M.baffu kabisa na kama nasemi sasa na anyamaze hata milele. Hatutegemei lolote jema kutoka ccm. Yote ni majambazi tu yamezoea rushwa na ku black mail.