Jaji ajitoa kesi ya Lema wa Arusha

mambo naona sasa yameiva , ninauhakika usahahidi utatolewa lakini watautia kapuni kama spika alivyo fanya kwa swala la Lema na Lisu

IMMA inasimamia majina ya wamiliki wa kampuni hiyo ya mawakili ambao ni Protase Ishengoma, Lawrence Masha, Aloysius Mujulizi na Sadock Magai.

Mmoja wa wamiliki wa kampuni hiyo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha aliithibitishia MwanaHALISI kwamba ni mwanzilishi na mmiliki wa IMMA.

Hata hivyo aliharakisha kusema kwamba kwa sasa amekabidhi majukumu yake kwa wakurugenzi wake wengine baada ya kuchukua wadhifa serikalini.

"Ni kweli kwamba mimi ni mmoja wa wakurugenzi waanzilishi wa IMMA, lakini kwa sasa siko huko. Nimeacha kujishughulisha na shughuli za kampuni hiyo tangu mwaka 2005 nilipoingia serikalini," alisema Masha.

Aidha, Masha alithibitisha pia kwamba kampuni ya IMMA ndiyo iliyosajili kampuni ya Deep Green Finance Limited na kwamba ni kweli kuwa inamwajiri Ridhwan.

Hata hivyo, Masha amesema mwenye nafasi nzuri zaidi ya kuzungumzia masuala ya IMMA hivi sasa ni mkurugenzi mwendeshaji, Protase Ishengoma.

Ridhwani alifanya kazi katika kampuni hiyo ya uwakili akiwa bado kwenye mafunzo mara baada ya kupata shahada yake ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.



 
Mkuu ritz,

Mheshimiwa Lema ana haki ya kumkataa Jaji lakini ni vyema taratibu na kanuni zikafuatwa.Notisi ya kumkataa Jaji Aloyce Mujulizi iliwasilishwa January 31,2012 kinyume cha sheria.Pamoja na notisi ya kumkataa Jaji Aloyce kutokidhi matakwa ya kisheria Jaji kaamua kujitoa.

Mheshimiwa Lema atatakiwa ndani ya siku tano kuwasilisha vielelezo vya tuhuma jinsi kampuni ya IMMA ilivyohusika na wizi wa fedha za EPA.Hii ni hatua nzuri sana kwasababu Rais atatakiwa kuunda tume kuchunguza sakata hilo na pengine kuangalia kama Jaji Aloyce anastahili kuendelea na wadhifa wake.Iwapo Mheshimiwa Lema atashindwa kuwasilisha ushahidi wake nadhani atakuwa amejiweka katika wakati mgumu na pengine sababu za kumkataa Jaji Aloyce zitachukuliwa ni mbinu a kuchelewesha kesi isimalizike ndani ya wakati.


Hakuna kosa kubwa alilofanya Lema, kama kumkataa Jaji wa Mahakama Kuu, Aloyce Mujulizi.

Lema, na wakili wake Method Kimomogoro, sijui watasemaje Jaji mpya akitoa hukumu kuwa Lema, kashindwa kesi nadhani itakuwa hakuna sababu yoyote ya kulalamika..

Kesi hiyo haina muda mrefu itakuwa imekwisha bado miezi minne tu tutajua yetu macho na masikio.
 
huyo jaji ni sehemu ya jamii za kitanzania zile zile zinazojiita zimesoma. Pumbafu yao.
 
Mkuu ritz,

Mheshimiwa Lema ana haki ya kumkataa Jaji lakini ni vyema taratibu na kanuni zikafuatwa.Notisi ya kumkataa Jaji Aloyce Mujulizi iliwasilishwa January 31,2012 kinyume cha sheria.Pamoja na notisi ya kumkataa Jaji Aloyce kutokidhi matakwa ya kisheria Jaji kaamua kujitoa.

Mheshimiwa Lema atatakiwa ndani ya siku tano kuwasilisha vielelezo vya tuhuma jinsi kampuni ya IMMA ilivyohusika na wizi wa fedha za EPA.Hii ni hatua nzuri sana kwasababu Rais atatakiwa kuunda tume kuchunguza sakata hilo na pengine kuangalia kama Jaji Aloyce anastahili kuendelea na wadhifa wake.Iwapo Mheshimiwa Lema atashindwa kuwasilisha ushahidi wake nadhani atakuwa amejiweka katika wakati mgumu na pengine sababu za kumkataa Jaji Aloyce zitachukuliwa ni mbinu a kuchelewesha kesi isimalizike ndani ya wakati.

Mkuu Ngongo,
Kwa wanaojua sheria ,Hatua ya Lema ni Kutisha sana,ni kama amejipiga kisu mwenyewe.
Tatizo litakua kuthibitisha hayo madai yake pasi na shaka yoyote.

Kwa mujibu wa sheria,kampuni yoyote lazima ipite kwa mwansheria kabla ya kusajiliwa,na sheria za biashara ya kimataifa zinakwenda mbali zaidi kwa kuruhusu kampuni ya kisheria kusimamia michakato yote ya kibiashara katika nchi husika.

Kwamba deep green imesimamiwa na IMMA katika kuianzisha hakuna ubishi,je kuna ushahidi kua pesa ilikwapuliwa imekwenda mfukoni mwa wakurugenzi wa IMMA?

Kutokana na hadhi na heshima ya jaji(ikumbukwe kua jamaa kabobea katika sheria) ni dhahiri mh.Lema anapaswa kuleta ushahidi mzito usio na shaka,vinginevyo anaweza kujikuta analipa mabilioni kama fidia ya kuichafua kampuni na jaji
 
Mkuu Ngongo,
Kwa wanaojua sheria ,Hatua ya Lema ni Kutisha sana,ni kama amejipiga kisu mwenyewe.
Tatizo litakua kuthibitisha hayo madai yake pasi na shaka yoyote.

Kwa mujibu wa sheria,kampuni yoyote lazima ipite kwa mwansheria kabla ya kusajiliwa,na sheria za biashara ya kimataifa zinakwenda mbali zaidi kwa kuruhusu kampuni ya kisheria kusimamia michakato yote ya kibiashara katika nchi husika.

Kwamba deep green imesimamiwa na IMMA katika kuianzisha hakuna ubishi,je kuna ushahidi kua pesa ilikwapuliwa imekwenda mfukoni mwa wakurugenzi wa IMMA?

Kutokana na hadhi na heshima ya jaji(ikumbukwe kua jamaa kabobea katika sheria) ni dhahiri mh.Lema anapaswa kuleta ushahidi mzito usio na shaka,vinginevyo anaweza kujikuta analipa mabilioni kama fidia ya kuichafua kampuni na jaji

Jamani haya mambo mengine muwe mnapitia pitia kurasa za zamani kabla ya ku-conclude suala ambalo lilijadiliwa kwa kina na vielelezo humu humu JF. Inashangaza some 4 to 5 yrs later eti sasa inazungumzwa hadhi na heshima ya jaji!!!!!!!
 
Hakuna kosa kubwa alilofanya Lema, kama kumkataa Jaji wa Mahakama Kuu, Aloyce Mujulizi.

Lema, na wakili wake Method Kimomogoro, sijui watasemaje Jaji mpya akitoa hukumu kuwa Lema, kashindwa kesi nadhani itakuwa hakuna sababu yoyote ya kulalamika..

Kesi hiyo haina muda mrefu itakuwa imekwisha bado miezi minne tu tutajua yetu macho na masikio.

Suala la Lema kushinda ama kushindwa kesi ni kitu kimoja, na suala la Lema kumkataa jaji Mujuluzi ni kitu kingine.

Jaribu kushughulisha akili yako japo kidogo tu utaona tofauti, hata kama umesoma shule ya kata.

Kisheria mlalamikaji ama mlalamikiwa ana haki ya kumkataa jaji ama hakimu, na ndiyo sababu jaji mujuluzi amekubali kujitoa ili hata kama mlalamikiwa akishindwa isionekane amefanya uonevu kwa sababu ya tuhuma zilizotolewa dhidi yake.
 
Jamani haya mambo mengine muwe mnapitia pitia kurasa za zamani kabla ya ku-conclude suala ambalo lilijadiliwa kwa kina na vielelezo humu humu JF. Inashangaza some 4 to 5 yrs later eti sasa inazungumzwa hadhi na heshima ya jaji!!!!!!!

Sidhani kama kuna mtu anayeweza kuwa na uwezo wa ku access mtandao na mfuatiliaji wa siasa za Tanzania asiyefahamu sakata la IMMMA advocates na kampuni ya Deep Green Finance, jinsi walivyoshirikiana kukwapua fedha toka BOT.

Hawa wanaojaribu kujitoa akili wanajaribu kupiga rangi upepo, kwakuwa ukweli wa hili suala ni bayana.
 
Je ushahidi ukitolewa Mujulizi atakuwa tayari kuuweka hadharani na kukiri kuwa kweli alihusika kuiba jasho la watanzania?

Ndugu yangu Mungi hawa majaji waliochaguliwa na JK fastafasta kwa kisingizio cha mrundikano wa kesi umesababishwa na uchache wa majaji ni lazima tuwe waangalifu kuliko kwa majaji wazamani, ukiwachunguza mmojammmoja kwa undani wao basi utakuta loopholes zinazotia shaka sana, kuna mmoja katika group hilo si msafi kabisa na siku akiyaboronga tu tutamjadili kwa evidence.
 
Mkuu Ngongo,
Kwa wanaojua sheria ,Hatua ya Lema ni Kutisha sana,ni kama amejipiga kisu mwenyewe.
Tatizo litakua kuthibitisha hayo madai yake pasi na shaka yoyote.

Kwa mujibu wa sheria,kampuni yoyote lazima ipite kwa mwansheria kabla ya kusajiliwa,na sheria za biashara ya kimataifa zinakwenda mbali zaidi kwa kuruhusu kampuni ya kisheria kusimamia michakato yote ya kibiashara katika nchi husika.

Kwamba deep green imesimamiwa na IMMA katika kuianzisha hakuna ubishi,je kuna ushahidi kua pesa ilikwapuliwa imekwenda mfukoni mwa wakurugenzi wa IMMA?

Kutokana na hadhi na heshima ya jaji(ikumbukwe kua jamaa kabobea katika sheria) ni dhahiri mh.Lema anapaswa kuleta ushahidi mzito usio na shaka,vinginevyo anaweza kujikuta analipa mabilioni kama fidia ya kuichafua kampuni na jaji
ushahidi gani wewe ?? vyeo walivyopewa wahusika wote wa IMMA na seikali ni ushahidi tosha wa kufunika maovu wkishapewa ushaidi them what's next?
 
Kwanza mimi nilikuwa nashangaa kwa nini Mjulizi alichelewa ku declare interest na kujidisqualify kusikiliza kesi hiyo kampuni yao ndiyo iliyomwajiri Ridhiwani na binti wa Karume na hiyo ndiyo contributing factor kuteuliwa kuwa Jaji na mwenzake kuwa waziri na ndugu zao wengine kuteuliwa kwenye nafasi mbalimbali na kubwa serikalini, Inawezekana mjulizi angeweza kutenda haki lakini principles of natural justice haziruhusu yeye kuwa trial judge kutokana na interest hizo kwani haki siyo tu inatakiwa itendeke bali pia ionekane kutendeka. Hongera sana kamanda Lema na wakili Kimomogoro
 
kweli,mkuu I know exactly what is IMMA!!mtoto,wa,karume,unayemsema ni FATMA!!
 
Back
Top Bottom