OLESAIDIMU wewe ni moja ya wanajamii wa JF wenye mawazo na michango ninayoikubali kwa kiasi kikubwa. Lakini hili la kusema eti Mwingulu anaponzwa na misimamo yake sikubaliani nalo. Mwingulu hana msimamo wa aina yoyote ambao ni positive kwa nchi yetu. Ni msanii asiyetumia maarifa na aliyeona uchaguzi unakaribia akajifanya kubadilika na kuwa upande wa wananchi. Na kama huyu Jairo amechukua fomu na akiweza kumwangusha Mwingulu basi nitafurahi sana (sio kwa sababu ni mtu mzuri) bali nataka Mwingulu aone makosa ya kutumika kuzima ukweli kuhusu uchafu uliokuwa unafanywa na utawala.