TANZIA Jackson Makwetta (Mbunge na Waziri wa zamani) afariki dunia

mkuuu wa nchi sijui kama atakwenda kutowa salamu za rambi rambi atadai amechoka na safari ya dodoma anaitaji kupumzika

MUNGU akurehemu upumzike kwa amani
 
Mzee huyu alikuwa ni miongoni mwa viongozi wachache wa CCM waliotumikia taifa lao kwa uadilifu na kwa uzalendo wa hali ya juu, akiwa waziri wa serikali kwa miaka 25 mfululizo (1975 - 2000), lakini hakuna mahali alitumia vibaya madaraka yake kwani inasemekana kwamba hata nyumba ya kuishi nje kidogo ya jiji la Dar-es-salaam alijengewa na wanae kabla ya kustaafu na hata hivyo haikukamilika ipasavyo; na katika kipindi karibia chote cha ustaafu wake alikuwa anaishi kwao kijijini;

Lakini kwa vile serikali yetu ya CCM haijali watu kama hawa, msiba wake utaendeshwa kinafiki tu; Misiba yenye kupewa uzito ni ile ya viongozi wasiokuwa wazalendo ambao utashi wao unapimwa kwa utajiri wao; Lakini ipo siku yote haya yatabadilika;

Poleni wafiwa; Mwenyezi mungu amlaze mahali pema peponi Mzee wetu Makweta, Amen;

Mkuu hapo kwenye Red sidhani kama unaongea sawa! Jee, mazishi ya Mwalimu Nyerere hayakupewa uzito unaostahili? jee, vipi mazishi ya Sokoine, Kawawa, Mzee Rupia, Bibi Titi, nk? jee, hawa viongozi hawakuwa Wazalendo? kama jibu lako ni ndio basi utakuwa Mtanzania wa kwanza kuwatuhumu viongozi hawa kwa utovu wa uzalendo!

Vinginevyo nakuomba ukanushe kauli yako na kuwaomba msamaha familia ya wazalendo hawa!
 
rip
Haya wanasiasa wakaoshe sura na kurusha mapicha kwenye blogi ya michuzi
 
Ninamkumbuka sana makweta, tulikuwa tukimuimba katika nyimbo madarasani mwetu wakati nilipokuwa shule ya msingi miaka ya 1983 na 1984 enzi hizo akiwa ni waziri wa Elimu. Kwa kweli tulikuwa na viongozi wazalendo enzi zile, watu kama akina Rashid Mfaume Kawawa, Edward Moringe Sokoine n.K. Leo viongozi waliosalia ni balaa tupu, tumbo mbele uzalendo nyuma.
 
Mwadilifu namba moja ktk serikali alizozitumikia!

Maisha yake hafifu baada ya kustaafu yametufundisha kuwa labda inabidi uwe fisadi angalau kidogo ili usiadhirike ukistaafu kwani pensheni kiduchu wanayolipwa wastaafu ya kila mwezi haikusaidii lolote kwa hii inflation kubwa tuliyo nayo!

RIP Mzee Makweta na serikali iwaangalie sasa watumishi wake kwa kubadili pensheni zao!
 
Namkumbuka haswa enzi nikiwa shule ya msingi enzi ile Mwalimu naye alikuwa na wasifu serikalini na hata awamu ya pili ya Mwinyi alikuweko tu madarakani.

Rest In Peace Jackson Makwetta! Bwana atakufufua siku ya ufufuo! Aaamen!
 
Utashangaa msiba wa Kanumba serikali ya CCM very budy, lakini wazalendo kama Makweta hamna kitu. RIP Makweta
 
mwenyezi MUNGU amlaze pema mzee makweta na pia awajalie moyo wa uvumilivu ndugu na jamaa wote hasa katika kipindi hiki kigumu cha kumpoteza mtu mashuhuri
 
Mkuu hapo kwenye Red sidhani kama unaongea sawa! Jee, mazishi ya Mwalimu Nyerere hayakupewa uzito unaostahili? jee, vipi mazishi ya Sokoine, Kawawa, Mzee Rupia, Bibi Titi, nk? jee, hawa viongozi hawakuwa Wazalendo? kama jibu lako ni ndio basi utakuwa Mtanzania wa kwanza kuwatuhumu viongozi hawa kwa utovu wa uzalendo!

Vinginevyo nakuomba ukanushe kauli yako na kuwaomba msamaha familia ya wazalendo hawa!

Kwa wanaonielewa wamenielewa; unafiki wa viongozi wetu kwenye misiba kama hii upo pale pale ndugu yangu; Na sitabadilisha kauli yangu;
 
Pamoja na kuwa na mawaziri kibao wa elimu kama akina Mayagila, Mgonja, Kapuya, Mungai n.k, marehemu Makweta ni bora kuliko wote. Namkumbuka sana kwa kuanzisha mtihani wa kidato cha pili.

Poleni sana wafiwa, RIP Makweta, J.
 
ni miongoni mwa wazee wakongwe kabisa ndani ya 'chama changu'!.....ambao kiukweli hichi 'chama changu'(mimi,fmes na pasco) kitakumbuka mchango wake mkubwa katika kukijengea sifa kubwa 'chama changu'

pumzika babu yangu!.......

you are in a better place now
 
Pole sana dada Tumwa! Baba katutoka! Mungu kampenda zaidi, mungu atawafariji wakati huu mgumu wa majonzi, bwana ametoa bwana ametwaa! RIP Makweta
 
Back
Top Bottom