Nikupateje
JF-Expert Member
- Dec 22, 2009
- 1,334
- 988
Waheshimiwa,
Nadhani tunapomuenzi Julius Nyerere basi kisiasa hatuwezi kupishana na hilo. Lakini tupomuenzi kwa fikra ndipo hapo tunapofanya makosa. Kwa sababu kama ni fikra basi sifa ye kuenziwa fikra zako ni kuitwa wewe Philosopher.
Na kama ni hivyo basi, philosopher hakuwa yeye tu hapa Tanzania. Mitizamo yake zimo kwenye vitabu vyake kama zilivyo fikra za wenzake kwenye vitabu vyao.
Nimetumia neno mitizamo yake. Ningekuwa na uhakika ningejiunga na wale wengi walisema zidumu fikra zake. Kwangu hoja si kudumu au hata kuishi kwa fikra zake kwa muda gani. Kwangu hoja ni kwamba je zilikuwa au zake au za wengine.
Najiuliza hivi kwa sababu Nyerere angekuw hasomi hata kitabu kimoja basi hakika ningesema ni fikra zake. Lakini naambiwa kwamba ile maktaba yake pale Butiama ina vitabu zaidi ya 8,000. Yeye mwenyewe aliwahi kukiri kuwa utajiri wake ni vitabu. Kuwa na vitabu vingi maana yake una fikra za watu wengi, unasoma fikra zao.
Maadamu hatujui kuwa ni sehemu gani za hotuba au mandishi yake ilijazwa na hayo aliyosoma sasa tutasemaje tuzienzi fikra zake.
Hivyo ninaomba tujadili umuhimu wa kuwa na Tanzanian Philosophers Day. Kwamba siku hiyo au wiki hiyo tujadili michango ya mawazo ya philosphers wengi kama si wote waliojitokeza kuweka hadharani ideas zao.
Ninaona hatari ya kuendelea hivi tulivyo. Hatari moja ni kwamba jinsi tunavyo-publicize idea ya philosopher mmoja basi wajukuu zetu hawatasubiri tufe wafunue vichwa vyetu bali bado tukiwa hai watatuuliza "hivi babu, kwani mwenye mawazo nchi hii alikuwa mtu mmoja tu?".
Kingine, ni kwamba tunapiga kelele kila siku kuwa historia imepindishwa tutafiti historia ya kweli. Sasa tunachofanya ni kilekile. Kijana wa siku hizi kama mimi haoni kama sentensi yake itapata usikilizwaji bila kupachika maneno kama "kumuenzi Baba wa Taifa", "Kama alivyosema Nyerere", "Kama hotuba fulani ya Nyerere" na mengine mengi mradi tu litamkwe jina Nyerere na walau neno moja alilolisema wakati fulani.
Ukitamka neno "Kama alivyosema Shivji" wanaweza kukusikiliza kwa sababu yuko hai lakini akifa wanaweza kusahahu. Ni wangapi wanasema "Kama alivyosema Shaban Robert" na wanasikilizwa. Nyerere mwenyewe alikuwa anarejea na kuwataja maphilosopher kama Plato wala si kusema "Kama nilivyosema mimi".
Hivyo, nadhani tutaelewa vizuri nia yangu kuwa kuna maphilosopher wengi na wametoa mawazo yao mengi lakini hawajapata populality kama Nyerere na tusipokuwa makini tutapoteza mawazo yao au watakuja watu toka Ulaya na kutuambia kwamba mtanzania mwenzenu alisema haya na tukaishia kushangaa.
Hivyo, badala ya kutengeneza kongamano la kumuenzi philosopher mmoja na tukaliita "kongamano la kumuenzi Mwalimu Nyerere" basi ni bora tuwe na wiki nzima ya philosophers wa Tanzania. Huko vitabu vyao viuzwe ili tujue ukweli au udhaif wa mawazo yao. Watu kama Oscar Kambona tuna haki ya kusoma vitabu vyao ili tuwahukumu wenyewe kwa akili zetu binafsi kwa kusoma walichoandika kama tunavyowahukumu waandishi na philosopher wengine duniani. hatutaki kusimuliwa na aliyesoma au aliyekuwepo.
Narudia, msiponielewa basi tusiwalaumu baba na mama zetu ambao tunasema walipindisha historia wakati kumbe afadhali wakati wao maana usipotaja majina ya wanasisa hata kazi ilikuwa mbinde kupata, sasa leo hatubabaiki kwa kuwa na alternatives nyingi maishani bado tunaendeleza kutaja jina moja tu na matokeo yake dunia inatushangaa kama tulikuwa na thinker mmoja tu.
Nawasilisha
Nadhani tunapomuenzi Julius Nyerere basi kisiasa hatuwezi kupishana na hilo. Lakini tupomuenzi kwa fikra ndipo hapo tunapofanya makosa. Kwa sababu kama ni fikra basi sifa ye kuenziwa fikra zako ni kuitwa wewe Philosopher.
Na kama ni hivyo basi, philosopher hakuwa yeye tu hapa Tanzania. Mitizamo yake zimo kwenye vitabu vyake kama zilivyo fikra za wenzake kwenye vitabu vyao.
Nimetumia neno mitizamo yake. Ningekuwa na uhakika ningejiunga na wale wengi walisema zidumu fikra zake. Kwangu hoja si kudumu au hata kuishi kwa fikra zake kwa muda gani. Kwangu hoja ni kwamba je zilikuwa au zake au za wengine.
Najiuliza hivi kwa sababu Nyerere angekuw hasomi hata kitabu kimoja basi hakika ningesema ni fikra zake. Lakini naambiwa kwamba ile maktaba yake pale Butiama ina vitabu zaidi ya 8,000. Yeye mwenyewe aliwahi kukiri kuwa utajiri wake ni vitabu. Kuwa na vitabu vingi maana yake una fikra za watu wengi, unasoma fikra zao.
Maadamu hatujui kuwa ni sehemu gani za hotuba au mandishi yake ilijazwa na hayo aliyosoma sasa tutasemaje tuzienzi fikra zake.
Hivyo ninaomba tujadili umuhimu wa kuwa na Tanzanian Philosophers Day. Kwamba siku hiyo au wiki hiyo tujadili michango ya mawazo ya philosphers wengi kama si wote waliojitokeza kuweka hadharani ideas zao.
Ninaona hatari ya kuendelea hivi tulivyo. Hatari moja ni kwamba jinsi tunavyo-publicize idea ya philosopher mmoja basi wajukuu zetu hawatasubiri tufe wafunue vichwa vyetu bali bado tukiwa hai watatuuliza "hivi babu, kwani mwenye mawazo nchi hii alikuwa mtu mmoja tu?".
Kingine, ni kwamba tunapiga kelele kila siku kuwa historia imepindishwa tutafiti historia ya kweli. Sasa tunachofanya ni kilekile. Kijana wa siku hizi kama mimi haoni kama sentensi yake itapata usikilizwaji bila kupachika maneno kama "kumuenzi Baba wa Taifa", "Kama alivyosema Nyerere", "Kama hotuba fulani ya Nyerere" na mengine mengi mradi tu litamkwe jina Nyerere na walau neno moja alilolisema wakati fulani.
Ukitamka neno "Kama alivyosema Shivji" wanaweza kukusikiliza kwa sababu yuko hai lakini akifa wanaweza kusahahu. Ni wangapi wanasema "Kama alivyosema Shaban Robert" na wanasikilizwa. Nyerere mwenyewe alikuwa anarejea na kuwataja maphilosopher kama Plato wala si kusema "Kama nilivyosema mimi".
Hivyo, nadhani tutaelewa vizuri nia yangu kuwa kuna maphilosopher wengi na wametoa mawazo yao mengi lakini hawajapata populality kama Nyerere na tusipokuwa makini tutapoteza mawazo yao au watakuja watu toka Ulaya na kutuambia kwamba mtanzania mwenzenu alisema haya na tukaishia kushangaa.
Hivyo, badala ya kutengeneza kongamano la kumuenzi philosopher mmoja na tukaliita "kongamano la kumuenzi Mwalimu Nyerere" basi ni bora tuwe na wiki nzima ya philosophers wa Tanzania. Huko vitabu vyao viuzwe ili tujue ukweli au udhaif wa mawazo yao. Watu kama Oscar Kambona tuna haki ya kusoma vitabu vyao ili tuwahukumu wenyewe kwa akili zetu binafsi kwa kusoma walichoandika kama tunavyowahukumu waandishi na philosopher wengine duniani. hatutaki kusimuliwa na aliyesoma au aliyekuwepo.
Narudia, msiponielewa basi tusiwalaumu baba na mama zetu ambao tunasema walipindisha historia wakati kumbe afadhali wakati wao maana usipotaja majina ya wanasisa hata kazi ilikuwa mbinde kupata, sasa leo hatubabaiki kwa kuwa na alternatives nyingi maishani bado tunaendeleza kutaja jina moja tu na matokeo yake dunia inatushangaa kama tulikuwa na thinker mmoja tu.
Nawasilisha