Wadau habari za mchana huu jana nilisafiri na kaka mmoja kwenye ndege alikuwa ni mtu mwenye mawazo mengi sana badae akaamua kuzungumza namnukuu kama ifuatavyo. (Dada mm naitwa .......................... akataja jina lake naishi Arusha nafanya kazi katika mgodi wa Tanzanite nimeoa na nina mtoto mmoja sijui wewe unaitwa nani nami nikataja jina langu nakumweleza naishi Dar es salaam nimetoka Arusha kwa matembezi tu akaendelea samahani dada mm nina matatizo makubwa na mke wangu nikastuka kdg na kwa haraka moyoni nikajiambia sasa matatizo yako na mkeo mm yananihusu nn? kama vile alinisoma akilini mwangu akanambia najua hili nalokuelezea hapa halikuhusu lakini nakuomba tu univumilie na unisikilize tafadhari nikamwambia usijali endelea akasema dadahuu ni mwaka wa 3 nalala kitanda kimoja na mke wangu lakini hatushirikiani chochote katika tendo la ndoa jaman mwenzenu nilistuka mno yani naomba niweke wazi nilistuka na kutomwamini huyu kaka nilijiuliza maswali mengi sna haraka haraka wanawezaje kulala kitanda kimoja miaka 3 na awashirikiani kwa chochote lakini huyu kaka alivyoendelea kunielezea nikaanza kupata picha kamili kwamba akisemacho ni kweli nilimuuliza kitu kimoja unadhani kuna wakati utafika mtashilikiana tena na mke wako akajibu hata wakati ukifika yy binafsi hayuko tayari tena wataishi hivyo hivyo hd kifo kiwatenganishe kwani hayuko tayari kumtaliki mkewe sasa wadau mm nko njia panda na ndoa hii ivi tunaiitaje ndoa hii? na je kwa umri niliomwona nao huyu mkaka ni age ya miaka 30 na kitu tena azidi 35 it means na mkewe hatakuwa 30 ivi sasa mbona bado vijana je haja zao wanatimizia wapi? nikamuuliza umewahi kwenda Kanisani au hata kwa wasimamizi wenu mkakaa chini kuongea akasema yote wamefanya tena wakiyaongea wanakubaliana yameisha ila wakifika kitandani hakuna kinachoendelea kiukweli nilikosa cha kumshauri nimebaki naona kama mchezo wakuigiza labda ww mdau kama unaushauri wwte utoe.