ITV wanadhoofisha bomoabomoa ya Magufuli?

ITV wanadhoofisha bomoabomoa ya Magufuli?

Tanzania bwana sasa kuwavunjia watu majumba ndiyo kuinyoosha nchi?watanzania wengi akili zao zina walakini
 
Mtu anaishi mkwajuni anafanya kazi ya kuuza vitu vidogo vidogo Posta...mtoto wake anasoma magomeni we unampeleka Mabwepande alafu unamuwekea nauli ya magari 1400.
 
mobile.mwananchi.co.tz/Habari/Watu-1-500-wakumbwa-na-mafuriko-Morogoro/-/1597580/3022802/-/format/xhtml/-/apiqit/-/index.html
 
Endelea kufurahi wenzio kubomolewa..lakini ninavyowajua madictator hata wewe yatakukuta kwa namna nyingine..
 
ITV wanajihangaisha tu. Boss wao naye ni mhanga wa bomoa bomoa inayoendelea. Lakini hata hivyo waziri alishasema. hataonewa mtu, na wala hataachwa yeyote aliyevunja sheria
 
Katika taarifa ya habari iliyosomwa jana usiku saa mbili na kurudiwa leo asubuhi ITV imeripoti kuwa hata nyumba ambazo zilikuwa maeneo ya juu ambazo hazijawahi kukumbwa na mafuriko nazo zimebomolewa. Taarifa hii wameipata kwa kuwahoji waathirika pekee bila kuwahoji wasimamizi wa ubomoaji kama zina ukweli wowote au ni malalamishi yasiyo na msingi.

Kwa mtazamo wangu nadhani walipaswa kuwahoji na wasimamizi wa bomoabomoa ili kupata habari iliyokamilika vizuri. ITV kurusha taarifa kama hii kwa upande wangu naona kama ni kudhoofisha bomoa bomoa inayoendelea kwa kuwa itaonekana kama ni zoezi ambalo halikufanyiwa utafiti wa kina kujua ni nyumba zipi zinapaswa kubomolewa hivyo kuonekana kama serikali ilikurupuka na inachofanya ni uonevu kwa baadhi ya watu.

Naomba kuwasilisha ila matusi hapana.
Nyumba zinazo bomolewa si tu zilizo bondeni bali hata zile zilizo jengwa ambapo ni sehemu za wazi au sehemu zenye matumizi mengine....! Hivyo wako sahihi...kwa hiyo sababu za kubomoa ziko nyingi si kuwa bondeni pekee...
 
Katika taarifa ya habari iliyosomwa jana usiku saa mbili na kurudiwa leo asubuhi ITV imeripoti kuwa hata nyumba ambazo zilikuwa maeneo ya juu ambazo hazijawahi kukumbwa na mafuriko nazo zimebomolewa. Taarifa hii wameipata kwa kuwahoji waathirika pekee bila kuwahoji wasimamizi wa ubomoaji kama zina ukweli wowote au ni malalamishi yasiyo na msingi.

Kwa mtazamo wangu nadhani walipaswa kuwahoji na wasimamizi wa bomoabomoa ili kupata habari iliyokamilika vizuri. ITV kurusha taarifa kama hii kwa upande wangu naona kama ni kudhoofisha bomoa bomoa inayoendelea kwa kuwa itaonekana kama ni zoezi ambalo halikufanyiwa utafiti wa kina kujua ni nyumba zipi zinapaswa kubomolewa hivyo kuonekana kama serikali ilikurupuka na inachofanya ni uonevu kwa baadhi ya watu.

Naomba kuwasilisha ila matusi hapana.

Na pia ni rahisi kuleta uchochezi, hasira na vurugu kwa wananchi. Hiyo ni hatari sana
 
ITV wanajihangaisha tu. Boss wao naye ni mhanga wa bomoa bomoa inayoendelea. Lakini hata hivyo waziri alishasema. hataonewa mtu, na wala hataachwa yeyote aliyevunja sheria
Soma habari usiingie mkenge wa watu hakuna sehemu ITV wanapinga bomoa bomoa..hili jambo si la kisiasa...! Bahati mbaya huwa watu mkikuta mada mnaivaa tuu bila hata kufatilia...! Mtoa mada anachochea tuu hajui kama walio hojiwa wako sahihi maana unaweza kuwa hauko bondeni lakini ukabomolewa kwa sababu si sehemu ya makazi! Ni vyema mkafatilia kuliko kuandika tuu! Tafadhali msimchonganishe watu....
 
Unachotakiwa kuelewa ni kuwa hata mmiliki wa ITV ni mhanga wa bomoabomoa. Bila shaka anajihami na dhahama inayomsubiri muda wowote kuanzia sasa.
 
ITV lazima wawe negative na zoezi,si unajua nyumba ya bosi wao ipo baharini na imewekwa X
 
Hivi kwa akili yako unadhani ITV wataonesha mema ya Serikali ya Magufuli? Unamjua mmiliki wa ITV? Ni nani na anatoka wapi?

Umejibu vema tena stesheni hii inashabikia sehemu zenye vurugu tu shane on them!!!🙁
 
Soma habari usiingie mkenge wa watu hakuna sehemu ITV wanapinga bomoa bomoa..hili jambo si la kisiasa...! Bahati mbaya huwa watu mkikuta mada mnaivaa tuu bila hata kufatilia...! Mtoa mada anachochea tuu hajui kama walio hojiwa wako sahihi maana unaweza kuwa hauko bondeni lakini ukabomolewa kwa sababu si sehemu ya makazi! Ni vyema mkafatilia kuliko kuandika tuu! Tafadhali msimchonganishe watu....

Ukiona mwenzio ananyolewa, na wewe tia maji sasa ITV badala ya kutia maji wanaendelea kumchana afro boss wao. Boss wao ile nyumba ya baharini imewekewa X, badala ya kumuandaa kisaikolojia boss wao, wanazungumzia bondeni tu. Ubomoaji unaoendelea haupo kwenye siasa tena kama walivyozoea, narudia, waziri alishasema ubomoaji unaoendelea hautamwonea mtu na wala hautawaacha waliovunja sheria. Sasa kuchonganisha kuko wapi hapa kama wanachokionyesha kiko upande mmoja!
 
Back
Top Bottom