ITV na Wosia wa Baba wa Taifa

ZIDUMU FIKRA SAHIHI
 

Kila kitu kwa kiasi, hata uhuru unatakiwa kuwa Na kiasi.
Nchini ufaransa, uhuru ulizidi kiasi,Charlie Hebdo wakachora katuni za kumkashifu mtume Muhammad, kilichofuatia sote tunakijua, mauaji ya kutisha!
Mwalimu alipinga udikteta, lakini hata yeye alitambua kuwa uhuru unapaswa kuwa Na kiasi Na kuna wakati inahitajika kiongozi "kukaza kamba" kidogo ili Nchi iende.
Kama Nyerere angelegeza Na kuruhusu uhuru kupita kiasi, ishu ya Kambona ingeishia wapi?
Kipindi cha utawala wake wanafunzi wa UDSM waliandamana, alikaa kimya akaruhusu?
Je, walichokua wakidai hakikua haki?
Ifike mahali, siasa zisizo Na msingi tuweke pembeni Na tuangalie mambo kwa Upana wake,
Gaddafi aliitwa dikteta Libya, akauawa, Leo Libya ina hali gani baada ya kumuondoa "dikteta" Gaddafi?
Marekani ambako historia inatuambia ndiko demokrasia imezaliwa, ndio huko watu wanamiliki bunduki hovyo Na kila kukicha kuna matukio ya watu wasio Na hatia, wakiwemo watoto mashuleni kuuawa kwa kupigwa risasi,
Kwa nini matukio Kama Haya hayatokei Korea kaskazini au Urusi, nchi zinazotuhumiwa watawala wake kutawala kibabe?
Tuangalie mambo kwa upana wake,
Kila kitu kifanyike kwa kiasi, Ni asili yetu binadamu kutokuridhika!
Hata ikitokea tukapewa hiyo absolute freedom, kutatokea sababu nyingine ya kupinga mambo Na kulumbana Na mamlaka.[emoji1549]
 
Baada ya kichapo cha fine ya million Tano za yule Mchungaji na na kiti cha Naibu mini subwoofer..... Pampa oyeee
 
Hivi aliyemuweka jela ya nyumbani marehemu Jumbe ni nani? Kutaka serikali 3 ni kosa? Na udikteta ni nini?
Harafu mbona aliacha katiba ya mwaka 77 wakati aliruhusu vyama vingi 92..... aliacha NEC inayo chaguliwa na captain wa timu pinzani, katiba ya chama kimoja bila kufanya mabadiliko makubwa.... kwa haya huwa simwelewi baba wa Taifa... japo mengi nampa big up, JKN alikuwa anaona mbali sana....
 
Kuna 1 waliweka ya ukabila,.ati hatumpi kwa sababu ni mkara? Yani kiukweli ndo tunayaona haya, mbaya zaidi hii ya jana anasema hasa viongozi wa africa
 
Bado mnamuamini Mwl Nyerere na demokrasia?
Ambaye yy mwenyewe demokrasia yake ilikuwa ya mdomoni tu
Mwl hakuweka demokrasia kwenye practical
Alicho mfanya Mzee Jumbe ni unyama mbaya sana
Anayemsikiliza hadi leo Mwl Nyerere na porojo zake anapoteza tu muda wake
Ukimpinga Nyerere kwa hoja uliishia jela akikuhurumia sana kizuizi cha nyumbani ufe taratibu
Kama kuna JEHANAM nitashangaa sana nisipomkuta Mwl Nyerere huko
Nyerere na hotuba zake zipuuzwe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…