Ukitizama kwa umakini taarifa ya ITV wakati Lowasa anachukua form na anaporudisha form wahudhuriaji ni wale wale na aina ya mkao ni uleule na nguo walizovaa ni zilezile wakati ni matukio mawili tofauti yaliyofanyika siku tofauti, hivyo naamini hizi ni picha za kuengeneza.
Ukitizama picha zilizochukuliwa na wapita njia nakurushwa kwenye whatsap na facebook, msafara wa Lowasa ulikuwa na gari tatu tu Nissan patrol moja nyeusi na noah mbili nyeupe huku kundi dogo la waendesha bodaboda na wapiga debe wakilifuata kwa nyuma. Kumbuka siku za nyuma Lowasa alitoa fedha nyingi kwa hawa waendesha bodaboda na walikopeshana pikipiki hivyo kutoa fadhila ya kumpigia mahoni sio jambo geni.
Kama ndo staili hizi za kutengeneza picha sidhani kama zitazaa matunda ya maana, bora mambo yaachwe yafanyike kwa uhalisia wake. Kumbuka kule mwanza aliwafadhili wamachinga 30m wakaanzisha saccos na dio hao hao kila akija mza wanabebana kumpokea ili awaongezee mkwanja zaidi.