ITV inahujumiwa na startimes?!

ITV inahujumiwa na startimes?!

mwanza_kwetu

JF-Expert Member
Joined
Mar 2, 2011
Posts
693
Reaction score
182
This is clear now nafikiri hata tcra wanajua ila kwa sababu pia ni shm ya tbc.
Poor signal wakati tbc na zingine ziko sawa
 
This is clear now nafikiri hata tcra wanajua ila kwa sababu pia ni shm ya tbc. Poor signal wakati tbc na zingine ziko sawa
Mkuu, mbona jambo hilo liko wazi. Toka mwanzo tulipoingia kwenye kuanza kutumia visimbizi ITV ilikuwa haipatikani. Baadaye ikawa inapatikana nyakati nyakati lakini inakatakata. CHADEMA walipotoa tamko lao la kuwata watu wasusie TBC utafikiri StarTime ndiyo wameambiwa washughulikieni ITV. Juzijuzi CHADEMA waliporudia mwito wao wa kuwataka watanzania waisusie TBC, ITV ndiyo inahujumiwa sana. Nimewahi kuwapigia simu StarTimes kuhusu kutoipata ITV wanamajibu ya ajabu ajabu na longolongo fulani. wakasema watawasiliana na technical person wao aje kwangu nikakubaliana na; lakini utekelezaji wake ni kama kumwona tembo mweupe hadi leo. Ila kitu cha ajabu ni hiki, nilimwambia hata mchukua picha za video wakiwa na mtangazaji wakati wanawahoji watu kupata maoni yao kuhusu wali la KIPIMAJOTO, kuwa wanajua kwamba StartTimes wanawahujumu sana? Hawa kuwa na majibu ya maana seems hawajui. Nikwawaeleza kile kinachotokea kwetu, nikapata support ya bwana mwingine nay kwao they do experience the same. Nikawaambia wakawajulishe wakuu wao ikibidi hata kuwashitaki maana hizo ni hujuma za wazi katika biashara. Cha ajabu hadi sasa ITV kimyaaa.
 
umefanya uchunguzi, mimi natumia Star time ITV EATV nazipata vizuri, cha msingi uza Star time nunua Digtech.
 
Nilikuwa naangalia ITV Kupitia Startime, Baada ya kuchshwa na Chenga zao.
Nimefunga Free to air Dish nakamua ITV Freely bila mizengwe
 
Kweli. Natumia decoder ya startimes. Zaidi ya wiki sasa itv kwangu chenga na scratch kibao. Chanel nyingine zote ziko poa. Hii nahisi ni hujuma!
 
Nipo kimara signal mbovu mbaya alafu ni kwa ITV tu uko kwingine fresh,hizi hujuma kama wameshindwa watuambie tutupe startimes..
 
Sitaki kuamini kwamba, hii inaweza ikawa hujuma....itakuwa mbaya sana kama itakuwa hivyo....

Ila nakubaliana kwa issue ya ITV kukatika katika wakati nyingine zipo poa kabisa !....Ijumaa juzi nimepata taabu sana kuangalia kipindi cha kipima joto....

This is clear now nafikiri hata tcra wanajua ila kwa sababu pia ni shm ya tbc.
Poor signal wakati tbc na zingine ziko sawa
 
Ni hujuma,isingekua hivyo startimes wangetoa ufafanuzi haraka sana,lakini wameuchuna kimya!

Sitaki kuamini kwamba, hii inaweza ikawa hujuma....itakuwa mbaya sana kama itakuwa hivyo....

Ila nakubaliana kwa issue ya ITV kukatika katika wakati nyingine zipo poa kabisa !....Ijumaa juzi nimepata taabu sana kuangalia kipindi cha kipima joto....
 
Sitaki kuamini kwamba, hii inaweza ikawa hujuma....itakuwa mbaya sana kama itakuwa hivyo....

Ila nakubaliana kwa issue ya ITV kukatika katika wakati nyingine zipo poa kabisa !....Ijumaa juzi nimepata taabu sana kuangalia kipindi cha kipima joto....
Nafikiri ni wao wenyewe ITV pia wana uzembe wa aina fulani. Sidhani Kama hawafahamu matatizo ya matangazo Yao kukatika katika kwenye startimes. Hakika inakera na ni kwa nini ni mbaya zaidi kwenye taarifa ya habari?
 
binafsi tangu jana siipati kabisa imeamua kufutika mara ya mwisho niliiona ITV siku ya alhamisi kipima joto !
 
nimeshidwa kuangalia news itv leo yaani inakatakata sana
 
Nimejaribu kuichunguza kiufundi ili kujiridhisha kuwa tatizo halipo upande wa mteja. Kwangu mimi, ITV signal status inaonyesha kuwa Signal Strength ni 64% na Signal Quality ni 69%. Hivi ni viwango vya kuridhisha kabisa na tafsiri yake ni kwamba wateja tunapokea signal kwa kiwango cha juu karibu sawa na iliyosafirishwa. Sasa kama iliyosafirishwa inakuja na pixels (mabox box yanayokwama), basi ina maana aliyesafirisha signal ndio amesafirisha signal mbaya. Kwa mfumo wa sasa wa digital kwa watumiaji wa antenna, Star Times ndio wanaosafirisha signal ya contents za ITV, kwa hiyo wameamua kutuletea good but corrupted signal
 
Mi naangalia STAR TV maana ITV ndo hivyo tena inahujumiwa na ninahisi hii ni mbinu ya kuwalazimisha watu kuangalia TBC
 
Kweli. Natumia decoder ya startimes. Zaidi ya wiki sasa itv kwangu chenga na scratch kibao. Chanel nyingine zote ziko poa. Hii nahisi ni hujuma!
Nenda continental, startimes inapewa amri kutoka kwa wazir anayeongea na mwenye mbwa
 
eneo ninaloishi tangu jana kama saa1.30 hivi jioni channel zote zilikata mpaka
sasa , hajujarudishiwa huduma hii nikaribu mtaa mzima,
 
Kweli kabisa haiwezekani station moja tu ITV iwe na bad signals tena inazid kuwa mbaya wakati wa taarifa kama star TV hawataki kuwa na ITV wawatoe sisi tuachane nao tufuate king,amuzikitakachoonyesha ITV clearly bila kuhujumiwa
 
Back
Top Bottom