ITV inahujumiwa na startimes?!

ITV inahujumiwa na startimes?!

Huu ni Ugoro wa waTanzania kujifanya wanajua kila jambo!!! Hivi ukimpelekea Startimes Weak Signal as input kwako ..: wewe (startimes ndio unatakiwa kuifanya iwe quality)? You can only blame startimes kama station zote zinaonyesha weak signal at same time!!!

Poor Tanzanian... God gave us brain for thinking and not otherwise!
 
Nimegundua kuwa hili issue inahitaji ufafanuzi wa kiufundi kwani tunaweza laumu watu bure tu.
 
Kwenye soko huria bado mnahangaika tu na star times, hameni.
 
Mambo mengine ni uzushi wa hali ya juu. Mimi kwangu ITV, EATV, StarTV na nyingine zote nazipata vizuri sana. Hapo mwanzo kulikuwa na tatizo la ITV na StarTv watu walizusha kuwa ITV wanafanya hivyo ili watu waichukie startimes na wanunue digitek kumbe ha hyo haikuwa sawa
 
Nimejaribu kuichunguza kiufundi ili kujiridhisha kuwa tatizo halipo upande wa mteja. Kwangu mimi, ITV signal status inaonyesha kuwa Signal Strength ni 64% na Signal Quality ni 69%. Hivi ni viwango vya kuridhisha kabisa na tafsiri yake ni kwamba wateja tunapokea signal kwa kiwango cha juu karibu sawa na iliyosafirishwa. Sasa kama iliyosafirishwa inakuja na pixels (mabox box yanayokwama), basi ina maana aliyesafirisha signal ndio amesafirisha signal mbaya. Kwa mfumo wa sasa wa digital kwa watumiaji wa antenna, Star Times ndio wanaosafirisha signal ya contents za ITV, kwa hiyo wameamua kutuletea good but corrupted signal
Huu ndio ukweli. fanyeni utafiti kwanza mjue tatizo limeanzia wapi.
 
Mbona mengi na king'amuzi chake cha digtech wamefungia tbc au hamulioni hilo
 
Humu wengi mmeegemea upande mmoja kutokana chuki tunazomezeshwa, zinatufanya tuwe wavivu wakujaji mambo na kutoa hukumu ya upande mmoja, ITV charnel zake hawapendi zionekane kwingine. Je ye hawawezi fanya hujuma hujuma zidi ya Star time ili muichukie kama mfanyavyo hapa ili Digtech iuze maana kwa Startime kazi ni kujaza cheneli tena zinopendwa ili wauze wakihujumu wamejihujumu.
 
Nenda continental, startimes inapewa amri kutoka kwa wazir anayeongea na mwenye mbwa

itv,eatv na capital zimeondoshwa EasyTv na AzamTv hazipo,hivi ving'amuzi viwili Mengi anajihujumu

c.c. TCRA
 
Last edited by a moderator:
sawa tu mr. Mengi nae namuona kama mtu mwenye hinda na chuki tofauti na anavyojionesha kama mtu wa watu,free to air AZAMTV hataki waoneshe chanel zake.
 
Afadhali wadau mmenijuza...mimi nilidhani ni decoder yangu tu! kumbe! Kweli inawezekana ni hujuma....Tunangojea maelekezo kutoka kwa rais wa mioyo waTanzania..akisema tuzichome startimes ..leoleo naenda kuzipiga kibiriti
 
Back
Top Bottom