Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,315
- 33,111
Serikali imeshauriwa kutunga sheria maalum ya kushughulikia matatizo yanayotokana na unyanyapaa, ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto na wanaoishi na VVU.
Aidha, imeombwa kuweka misingi bora itakayowezesha kuanzishwa kwa mahakama za kifamilia ili kuwezesha matukio mengi yanayohusu familia kujadiliwa badala ya kila tukio kupelekwa katika mahakama za kawaida.
Changamoto hizo zilitolewa mwishoni mwa wiki na wakili Keregero Keregero wakati akitoa mada katika mafunzo ya kuwajengea uelewa waandishi wa habari juu ya kuandika habari zinazohusu unyanyapaa na ukatili dhidi ya wanawake, watoto na wanaoishi na VVU.
Keregero ambaye pia ni Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, alisema endapo hatua ya kuanzishwa kwa mahakama za kifamilia itafikiwa, bila shaka matatizo mengi yanayotokana na unyanyapaa yana ukatili vitapungua.
"Hivi sasa kuna matoleo zaidi ya kumi ya sheria mbalimbali, ikiwemo ya ndoa ya mwaka 1971, ya watoto, ya ardhi ya mwaka 1999 na ile mpya kabisa ya Ukimwi ya mwaka 2008 ambazo zote zimeshindwa kukabiliana vilivyo na ongezeko la vitendo vya unyanyapaa na ukatili dhidi ya wanawake, watoto na wanaoishi na VVU," alisema.
Alisema karibu katika kila kabila nchini matatizo ya kuongezeka kwa vitendo vya unyanyapaa na ukatili vimekuwa vikiripotiwa, lakini kutokana na wingi wake imekuwa vigumu kutatuliwa katika mahakama za kawaida.
Hata hivyo, wakili Keregero alisema wakati mwingine inakuwa vigumu kwa mahakama kupata majibu ya moja kwa moja kutokana na wanawake wengi kutokuwa tayari kutoa ushahidi pale wanapohitajika kutoa maelezo ya uhakika.
"Hali hiyo inachangiwa na baadhi ya makabila kudhani kupigwa au kukandamizwa na waume zao ni sehemu ya kuboresha mapenzi yao jambo ambalo ni kinyume na linasumbua wakati wa kutafuta haki," alisema.
Mafunzo hayo yameratibiwa na Chama cha Waandishi wa Habari za Ukimwi Tanzania (Ajaat) na kudhaminiwa na Watu wa Marekani (USAID) kupitia Futures Group International chini ya mradi wa Health Policy Initiative (HPI).
CHANZO: NIPASHE
Aidha, imeombwa kuweka misingi bora itakayowezesha kuanzishwa kwa mahakama za kifamilia ili kuwezesha matukio mengi yanayohusu familia kujadiliwa badala ya kila tukio kupelekwa katika mahakama za kawaida.
Changamoto hizo zilitolewa mwishoni mwa wiki na wakili Keregero Keregero wakati akitoa mada katika mafunzo ya kuwajengea uelewa waandishi wa habari juu ya kuandika habari zinazohusu unyanyapaa na ukatili dhidi ya wanawake, watoto na wanaoishi na VVU.
Keregero ambaye pia ni Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, alisema endapo hatua ya kuanzishwa kwa mahakama za kifamilia itafikiwa, bila shaka matatizo mengi yanayotokana na unyanyapaa yana ukatili vitapungua.
"Hivi sasa kuna matoleo zaidi ya kumi ya sheria mbalimbali, ikiwemo ya ndoa ya mwaka 1971, ya watoto, ya ardhi ya mwaka 1999 na ile mpya kabisa ya Ukimwi ya mwaka 2008 ambazo zote zimeshindwa kukabiliana vilivyo na ongezeko la vitendo vya unyanyapaa na ukatili dhidi ya wanawake, watoto na wanaoishi na VVU," alisema.
Alisema karibu katika kila kabila nchini matatizo ya kuongezeka kwa vitendo vya unyanyapaa na ukatili vimekuwa vikiripotiwa, lakini kutokana na wingi wake imekuwa vigumu kutatuliwa katika mahakama za kawaida.
Hata hivyo, wakili Keregero alisema wakati mwingine inakuwa vigumu kwa mahakama kupata majibu ya moja kwa moja kutokana na wanawake wengi kutokuwa tayari kutoa ushahidi pale wanapohitajika kutoa maelezo ya uhakika.
"Hali hiyo inachangiwa na baadhi ya makabila kudhani kupigwa au kukandamizwa na waume zao ni sehemu ya kuboresha mapenzi yao jambo ambalo ni kinyume na linasumbua wakati wa kutafuta haki," alisema.
Mafunzo hayo yameratibiwa na Chama cha Waandishi wa Habari za Ukimwi Tanzania (Ajaat) na kudhaminiwa na Watu wa Marekani (USAID) kupitia Futures Group International chini ya mradi wa Health Policy Initiative (HPI).
CHANZO: NIPASHE