Samatime Magari
Senior Member
- Feb 10, 2017
- 103
- 388
.
Yule jamaa wa parking kumbe akiona gari ndogo anaziita zipark kwenye mchanga ili wakati wa kutoka zinase then wapate kazi ya kuzinasua na vile mtu akishafika coco akigonga ulabu network sehemu za kuwa mchumi inakata basi wakawa wanacharge 2000 -10000 kuwanasua kwa mchanga..
.
Basi Jamaa akapark gari alikua yuko na mtoto flani chocolate color hafu katupia mikato ya beach, Binti amepanda juu, katikati ana kila sababu za kumfanya Ngoswe atupe kishkwambi cha serikali aachane na sensa Basi wazee wakaona hapa Pesa ipo mwamba akikwama lazima awatoe tu..
.
.
Jamaa akashuka akafanye yake yaliyomleta Coco mpaka jioni, Ile anakuja aondoke Jamaa kumbe wanamsubiri, Mzee akaingia kwa gari akatekenya ikawaka Akatia R akageuza gari, machine ikatoka kiulaini kama tonge lenye mlenda kooni Jamaa wakabaki wanatoa macho tu wasijue nini kilichoendelea hapo..
.
Kuja kugundua kumbe ile gari ni AWD so tyre zote nne zinapeleka moto Mzee Na hii imenifanya leo nikugusie hii mifumo ya AWD, 4WD, FWD na RWD cause kuna wadau huwa wanauliza tofauti zake, Na naweza sema ni moja ya swali ambalo linaulizwa sana na wadau..
.
.
Sasa mambo yasiwe mengi ndani ya dakika 1 ijayo utakua umeshajua maana na tofauti zake ni ipi ni nzuri zaidi kwa matumizi, AWD ni short term ya All wheel drive yani ni system ambayo tyre zote nne zinapata mwendo/zinavuta kwa kujitegemea [zina gain traction independently]..
.
All wheel drive inawekwa kwenye gari kwa kuipa gari three differentials [angalia picha hapo chini kupata uelewa zaidi], Sasa hizi differential utaziona mbele, katikati na nyuma na hii inazifanya tyre kujitegemea zenyewe zinapozunguka na hii ni safi sana kwa utelezi..
.
.
4WD hii ni four wheel drive ambayo engine inazipa mzunguko tyre zote 4 mzunguko kwa usawa [evenly], Sasa hii ni nzuri kwa gari za shughuli nzito nzito [heavy duty] na Ndio maana mara nyingi ipo kwenye gari za kazi na mara nyingi inakua engaged pale inapohitajika tu ingawa kuna gari ndogo pia zimeandikwa 4WD..
.
Kwa gari za 4WD unakuta pale kwa gear stick kuna ki gear pembeni kidogo dogo flani maalumu kwa ajili ya hii kazi. Kwa gari za kisasa siku hizi wanaweka button tu yani ukihitaji 4WD unabofya tu mambo yanakaa sawa. . Na kuna zingine zinaji engage automatic zenyewe napohitajika..
.
.
Sasa hizi system mbili AWD na 4WD uzuri wake unatokana na uhitaji kwa wakati huo, Mfano AWD ni nzuri sana ukiwa highway na gari ikiwa speed sababu tyre zote zinapeleka moto So gari inashika barabara na stability inakua vizuri pamoja na handling ya gari..
.
Pia AWD kwenye utelezi Wa mjini mjini huu au mchanga kama wa beach hivi ni rahisi kuchomoka, Pia tope ambazo gari haichimbi unatoka vizuri na huyo mwenzake 4WD yeye ni maporini kwa Maporini huko kwenye vichaka au milima mikali na sehemu zenye tope nzito ambazo gari inachimba ndo anafaa.. .
.
.
Pia kuna 2WD sema hii inaweza kuwe tyre za mbele au za nyuma, Ikiwa za mbele tunasema ni FWD [Front Wheel Drive], Hapa gari inazungusha tyre 2 za mbele tu na Ikiwa nyuma ni RWD [Rear wheel drive], gari inazungusha tyre za nyuma tu..
.
Hii FWD [Front wheel Drive] ndo gari Nyingi zenye engine ndogo za ujazo wa chini ya cc 2000 na mid SUV baadhi kama kina harrier inazo, Ni system moja poa sana sababu inakupa traction nzuri ukiwa unaendesha hasa kwenye utelezi na milima, Nikisema traction nzuri namaanisha uwezo wa tyre kushika barabara..
.
Na inakua nzuri sababu kama dereva unaweza direct tyre iguse wapi ili uchomoke mahali.. . Kama ulishawahi kuona mtu kakwama then anazungusha zungusha tyre za mbele ili zishike mahali ili atoke ndo nachomaanisha hapa.. .
.
RWD [Rear Wheel Drive] hii ni nzuri kwenye acceleration/kuchomoka Na unaikuta kwenye gari kama crown/tezza hivi na Pickups, Hii inakua nzuri sababu inasukuma gari mbele tofauti na FWD ambayo inavuta gari na ni nzuri katika kuanzisha mwendo na kubeba mizigo..
.
.
Sema RWD kwenye mchanga hua haina ujanja hasa ikiwa kwenye sedan/saloon cars Kama Brevis, Mark X, Crown and the like, Yani ukiingia kwenye mchanga tu jua kwamba ndo ushataga hapo Mpaka waje wakunasue ndo unatoka, so niwakumbushe madereva wa gari hizi ukiona mchanga tu pita mbali kabisa, kama una site yako Mikwambe unaacha chuma unakula TZ11..
.
.
Unaweza ukajiuliza kati ya hizi mifumo upi ni mzuri [AWD, RWD, FWD ,4WD], Kikubwa hakuna mfumo mzuri zaidi ya mwingine matumizi yako ndo yatafanya maamuzi Na tayari nimeshakupa picha na ufanyaji kazi wa hii mifumo so ni wewe kuangalia tu mahitaji yako na kufanya maamuzi..
.
Hopefully umejifunza kitu basi usisahau kushare na wengine wajifunze, Na kama unahitaji ushauri au kuagiza gari/kununua showroom au mkononi wasiliana nasi Tunafanya kazi na dealers wa Japan, UK, Singapore na hapa nchini, dealers wanaotupa gari nzuri kwa ajili yako..
.
.
Gari zenye ubora na bei nzuri tukitumia advantage ya discounts kama dealers kwa faida yako., Kwa BF, SBT, Enhance, Nikkyo, Autocom tuko na massive discount kwa September na October. Simply njoo WhatsApp [0714547598]au ofisini Posta Phoenix House mkabala na Mkapa tower tutaku assist..
.
.
Kama uko mkoani na unahitaji kuagiza gari karibu pia, utatupa hitaji lako tutakupa ushauri, Then tutakutumia options za gari ukishachagua utapewa invoice na utafanya malipo at cost [no extra cost] As long as kuna banks unaweza fanya miamala huko huko ulipo na gari ikaja..
.
Ukilipa gari itakua shipped then utakua unapewa updates on the same, Gari itafika then utakuja kuichukua au utaletewa pia mpaka nyumbani kwako, Natumaini umejifunza kitu kama jibu ni ndio basi usisahau kushare na wengine wapate haya madini..
.
.
Pia unaweza tembelea kurasa zetu za jamii kwa madini zaidi katika facebook, Instagram, twitter, telegram na whatsapp @samatimecardealers/samatimemagari..
.
Samatime Car Dealers Co Ltd
0714547598