EINSTEIN112
JF-Expert Member
- Oct 26, 2018
- 21,713
- 35,525
Israeli imefanya mashambulizi kadhaa alfajiri ya leo katika Ukanda wa Gaza, baada ya wanamgambo wa Palestina kurusha makombora ya roketi katika miji iliyopo kusini mwa Israeli.
Mashambulizi ya alfajiri ya Jumatatu ni makubwa zaidi tangu mapambano yaanze wiki moja iliyopita.
Israeli inasema imeshambulia majengo yanayomilikiwa na wanamgambo wa Hamas pamoja na nyumba kadhaa za makamanda wa kundi hilo, hata hivyo barabara kuu kadhaa na nyaya za umeme pia zimeharibiwa.
Mashambulio hayo yanatokea wakati jumuiya ya kimataifa ikitaka pande zote mbili katika mgogoro huo kusitisha mashambulizi.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UN) lilifanya mkutano wa dharura jana Jumapili na Katibu Mkuu wa UN António Guterres ameonya kuwa mapambano zaidi "yanaweza kusababisha hali mbaya ya kiusalama na kibinaadamu."
Guterres pia ametaka mapambano hayo "mabaya" yasitishe haraka iwezekanavyo.
Rais wa Misri Abdul Fattah al-Sisi ameeleza leo Jumatatu kuwa nchi yake "imepiga hatua kubwa katika kutafuta kusitishwa kwa mapambano...na matumaini bado yapo."
Lakini mpaka sasa hakuna dalili za hilo kutokea huku mapambano makali yakiingia wiki ya pili
Ghasia hizo ni zao la wiki za hamaki na wasiwasi baina ya Israeli na Palestina katika eneo la Jerusalemu Mashariki ambapo hali hiyo iliishia katika mapambano katika eneo takatifu kwa Waislamu na Wayahudi.
Kundi la Hamas, ambalo linaongoza Ukanda wa Gaza, likaanza kurusha makombora ya roketi baada ya kuionya Israeli iondoke katika eneo hilo la Jerusalemu, na hapo ndipo Israeli ilipoanza kufanya mashambulizi ya anga ya kulipiza.
Jeshi la Israeli linasema zaidi ya ndege 50 za kivita zimefanya mashambulizi ya dakika 20 muda mfupi kabla ya alfajiri ya leo.
Ndege vita hizo zimepiga na kuteketeza "maeneo ya kigaidi" 35 na kuharibu zaidi ya kilomita 15 za mfumo wa mahandaki yanayomilikiwa na Hamas, linadai jeshi la Israeli.
Jeshi hilo pia linadai kuwa limezipiga nyumba tisa za makamanda "wa ngazi ya juu" wa Hamas.
Hata hivyo hakujakuwa na idadi rasmi kufikia sasa ya watu waliofariki na kueruhiwa, lakini mamlaka za Palestina katika Ukanda wa Gaza zinasema kuwa mashambulizi hayo yamesababisha umeme kukatika katika maeneo mengi na kuharibu mamia ya nyumbana majengo mengine.
"Hakujawahi kuwa na mashambulizi ya ukubwa huu,"mkaazi mmoja wa Gaza ameliambia shirika la habari la kimataifa la AFP . Mad Abed Rabbo, 39, amesema alihisi "woga mkubwa na kutishika" wakati mashambulio hayo yakiendelea.
Kabla ya mashambulizi ya alfajiri ya leo, maafisa wa Palestina walitangaza kuwa mashambulio ya jana Jumapili yaliyosababisha vifo vya watu 40 ndiyo yalikuwa mabaya zaidi.
Mashambulizi ya alfajiri ya Jumatatu ni makubwa zaidi tangu mapambano yaanze wiki moja iliyopita.
Israeli inasema imeshambulia majengo yanayomilikiwa na wanamgambo wa Hamas pamoja na nyumba kadhaa za makamanda wa kundi hilo, hata hivyo barabara kuu kadhaa na nyaya za umeme pia zimeharibiwa.
Mashambulio hayo yanatokea wakati jumuiya ya kimataifa ikitaka pande zote mbili katika mgogoro huo kusitisha mashambulizi.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UN) lilifanya mkutano wa dharura jana Jumapili na Katibu Mkuu wa UN António Guterres ameonya kuwa mapambano zaidi "yanaweza kusababisha hali mbaya ya kiusalama na kibinaadamu."
Guterres pia ametaka mapambano hayo "mabaya" yasitishe haraka iwezekanavyo.
Rais wa Misri Abdul Fattah al-Sisi ameeleza leo Jumatatu kuwa nchi yake "imepiga hatua kubwa katika kutafuta kusitishwa kwa mapambano...na matumaini bado yapo."
Lakini mpaka sasa hakuna dalili za hilo kutokea huku mapambano makali yakiingia wiki ya pili
Ghasia hizo ni zao la wiki za hamaki na wasiwasi baina ya Israeli na Palestina katika eneo la Jerusalemu Mashariki ambapo hali hiyo iliishia katika mapambano katika eneo takatifu kwa Waislamu na Wayahudi.
Kundi la Hamas, ambalo linaongoza Ukanda wa Gaza, likaanza kurusha makombora ya roketi baada ya kuionya Israeli iondoke katika eneo hilo la Jerusalemu, na hapo ndipo Israeli ilipoanza kufanya mashambulizi ya anga ya kulipiza.
Jeshi la Israeli linasema zaidi ya ndege 50 za kivita zimefanya mashambulizi ya dakika 20 muda mfupi kabla ya alfajiri ya leo.
Ndege vita hizo zimepiga na kuteketeza "maeneo ya kigaidi" 35 na kuharibu zaidi ya kilomita 15 za mfumo wa mahandaki yanayomilikiwa na Hamas, linadai jeshi la Israeli.
Jeshi hilo pia linadai kuwa limezipiga nyumba tisa za makamanda "wa ngazi ya juu" wa Hamas.
Hata hivyo hakujakuwa na idadi rasmi kufikia sasa ya watu waliofariki na kueruhiwa, lakini mamlaka za Palestina katika Ukanda wa Gaza zinasema kuwa mashambulizi hayo yamesababisha umeme kukatika katika maeneo mengi na kuharibu mamia ya nyumbana majengo mengine.
"Hakujawahi kuwa na mashambulizi ya ukubwa huu,"mkaazi mmoja wa Gaza ameliambia shirika la habari la kimataifa la AFP . Mad Abed Rabbo, 39, amesema alihisi "woga mkubwa na kutishika" wakati mashambulio hayo yakiendelea.
Kabla ya mashambulizi ya alfajiri ya leo, maafisa wa Palestina walitangaza kuwa mashambulio ya jana Jumapili yaliyosababisha vifo vya watu 40 ndiyo yalikuwa mabaya zaidi.
Source: BBC